Social Icons

Ijumaa, 30 Mei 2014

TANAPA NA NSSF WATOA UFAFANUZI DHIDI YA TUHUMA ZA CHADEMA KWA ZITTO KABWE


Baada  ya msemaji  wa   kambi  ya  Upinzani  Bungeni  ambaye  ni  waziri  kivuli  wa  wizara  ya  Habari,Michezo, Vijana  na  utamaduni  kumtuhumu  Zitto  Kabwe   kuhusika  na  kinachoitwa  ufisadi  katika  shirika  la  TANAPA  na  NSSF, mashirika  haya  yameamua  kutoa  ufafanuzi  kuhusiana  na  tuhuma  hizi  ili  kuweka  mambo  sawa......

Meneja Uhusiano wa TANAPA, Paschal Shelutete  ameliambia  gazeti  la  Mwananchi  toleo  la  leo ( May 30)  kuwa    shirika  hilo  linakitambua  kiasi  hicho  kilichotajwa  na  wapinzani  na  kwamba  fedha  hizo  zilikuwa  ni  malipo  ya  wasanii  wa   Leka Dutigite   ambao  walifanya  kazi  ya  kuitangaza   Hifadhi ya Saadan...

“Leka Dutigite ilifika Hifadhi ya Saadan na kuitangaza kupitia kazi za sanaa... sikumbuki ni lini lakini walifanya kazi na DvD zake zipo. 

“Ifahamike si Leka Dutigite pekee, tunafanya kazi na wasanii mbalimbali kutangaza vivutio, mbuga na hifadhi zetu,” Shelutete  ameliambia  gazeti  la  Mwananchi


Naye  Meneja Kiongozi wa Idara ya Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa NSSF, Eunice Chiume ameliambia  gazeti  hilo  kuwa pesa walizozitoa kwa kundi hilo zilikuwa malipo ya kutengenezea wimbo maalumu wa shirika hilo na nyingine ni za udhamini wa onyesho lililofanyika mwaka jana mkoani Tanga.
 
“Kweli mara ya kwanza tuliwalipa Sh25 milioni wasanii wa kundi hilo ili watutengenezee wimbo na Sh56 milioni zilikuwa za udhamini wa onyesho lao, lakini kwa masharti ya kututangaza jambo ambalo lilikuwa na mafanikio kwetu kwani tumefanikiwa kupata wateja wapya 30,000 kutoka sekta isiyo rasmi,” alisema Chiume.
 
Alisisitiza kuwa wametumia kiwango hicho cha pesa ili kujitangaza kwa kuwa hata mashirika ya kijamii yanapaswa kufanya hivyo ili kuvutia wateja wengi zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates