Social Icons

Jumamosi, 28 Desemba 2013

ANGALIA PICHA YA MTOTO WA MCHEZAJI MPIRA MKUBWA DUNIANI AMBAYE NI ADIMU KUONEKANA KATIKA VYOMBO VYA HABARI.

ron2

article-0-1A1FF1B500000578-234_634x409
article-2526363-1A20036000000578-481_634x999

Huyo ndio mtoto wa Cristiano(Cristiano Jr)akiwa na familia yao katika uzinduzi wa jumba la makumbusho nchini kwao Ureno, sehemu iitwayo Madeira,nyumba hilo ni kwa jili kubwa ya Ronaldo na historia yake katika mpira.

Ni adimu sana mtoto huyo kuonekana katika Media na baba yake huwa hapendelei kabisa mwanae mwanae kuonekana katika vyombo hivyo.

Ijumaa, 27 Desemba 2013

SOMA HIII...MSICHANA ALIYEKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI CHINA WAUMIZA VICHWA VYA WENGI NCHINI TANZANIA

 
 Msichana wa Tanzania aliyekamatwa na madawa ya kulevya akiwa amesimama karibu na meza yalipowekwa madawa yaliyotolewa kutoka kwenye mwili wake
 
Ni msichana gani wa Tanzania aliyekamatwa na madawa ya kulevya nchini China? Hilo ni swali gumu ambalo kila mmoja amekuwa akijiuliza bila kupata jibu la uhakika. Mtandao wa chinadaily.com.cn umeandika habari na kuweka picha za kukamatwa kwa msichana huyo mwenye umbo refu, mwenye nywele ndefu na mweupe. Mtandao huo umeandika: Msichana mwenye miaka 28 kutoka Tanzania alikamatwa kwa tuhuma za kumiliki madawa ya kulevya huko -Macao, Dec 19, 2013. Alikuwa ameficha kilo 1.1 za heroin zenye thamani ya $137,720 ( sawa na zaidi ya shilingi milioni 85) ndani ya mwili wake na kuchukua ndege kutoka Thailand hadi Macao. Alisema alikuwa akielekea Guangzhou, mji mkuu wa jimbo la Kusini mwa China Guangdong.

Madawa yaliyotolewa kwenye mwili wa msichana huyo mwenye miaka 28 yakioneshwa mbele ya waandishi wa habari
 
 
Msichana wa Tanzania aliyekamatwa na madawa ya kulevya na aliyefunikwa uso wake akiwa chini ya ulinzi
Tunafahamu kuna majina tayari yanayotajwa kuwa huenda wakawa ndio msichana huyo lakini hatuwezi kuyataja wala kuthibitisha kwa sasa ili kuepuka kuripoti habari zisizo na ukweli. www.onaviews.blogspot.com

SOMA HIII.......TAULO ZA IVO MAPUNDA MARUFUKU GOLINI


Tabia ya kipa wa Simba, Ivo Mapunda kutundika taulo katika nyavu za golini sasa inaelekea kufikia ukomo kwa kuwa licha ya waamuzi kadhaa kumkataza kufanya hivyo wakati wa mechi, mwamuzi mwingine wa kimataifa ameliambia gazeti hili kuwa ni marufuku kutundika taulo golini.


Ivo amekuwa na kawaida ya kutundika taulo kwenye nyavu kisha kuendelea na mchezo, lakini kwenye Michuano ya Kombe la Chalenji, mwamuzi mmoja aliitoa na kumtaka kuiweka chini na iwe nje ya goli, pia katika mechi ya Simba dhidi ya Yanga, mwamuzi wa kati, Ramadhani Ibada wa Zanzibar alimkataza kuining’iniza kwenye nyavu wakati mechi ikiendelea.

Mwamuzi Oden Mbaga amesema ni kosa kutundika taulo kwenye nyavu kwa kuwa inaweza kuwachanganya wachezaji wakati wa mchezo.

“Kimsingi hairuhusiwi kabisa kuingia na taulo labda aliweke kwa nje lakini siyo ndani ya lile goli tena siyo taulo tu bali na vitu vingine vyovyote,” alisema Mbaga.

Wakati Ivo akiambiwa hivyo, makipa kadhaa wa Ulaya wamekuwa na kawaida ya kutundika taulo kwenye nyavu na hawazuiliwi na waamuzi.

Wakati huohuo, Ivo amesema ana mpango wa kuchapisha taulo zitakazo kuwa na nembo yake ili aweze kujiongezea kipato. "Fursa hiyo nimeona siku nyingi. Nitakutana na kampuni mbalimbali kuona uwezekano huo," anasema Mapunda.

 Alisema hivi sasa taulo anazotumia kujifuta jasho pindi anapokuwa uwanjani zina nembo mbalimbali lakini atakoma kuzitumia pindi zenye nembo yake zitakapoanza kutoka.

RAGE ANENA.............Yanga haitufungi hadi tuhujumiane.


Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage ametoa kali baada ya kuifananisha timu ya Yanga na kikosi cha vijana wa Simba wenye umri chini ya miaka 20 (Simba B).

Akizungumza katika kipindi cha 'Hot Mix' kilichorushwa na EATV juzi jioni, Rage alisema kikosi cha Yanga kwa sasa ni sawa na Simba B, hivyo hakina uwezo wa kuifunga Simba.

"Yanga ni Simba B, itawachukua muda mregu sana kuja kutufunga. Wamejaza wachezaji wengi waliotoka kwetu (Simba) ambao lazima walipe fadhila kutokana na mazuri ambayo Simba iliwafanyia," alisema Rage.

"Kwa sasa Simba inaweza kufungwa na Yanga pale tu mmoja ama baadhi wa viongozi wetu wataamua kuihujumu timu yetu. Hawana uwezo wa kutufunga pasipo sisi (Simba) wenyewe kuhujumiana," alisema zaidi Rage.

Aidha, Rage alitumia muda huo kujibu hoja 'maiti' za 'waasi' wa Simba waliokuwa wakidai kwamba hajahusika hata kidogo katika kufanikisha ushindi wa timu yao dhidi ya Yanga Jumamosi.

"Kuna vitu visivyo na maana vinazungumzwa juu yangu. Naambiwa sijashiriki katika kufanikisha ushindi dhidi ya Yanga. Mchezaji aliyefunga bao la tatu (kiungo Awadh Juma) nilimsajili nyumbani kwangu na ndiye aliyechangia pia bao la kwanza," alisema.

Mbunge huyo wa Tabora Mjini (CCM) alibainisha kuwa watu wanaompinga wanasumbuliwa na ukata wa fedha, hivyo wanatafuta namna ya kumng'oa madarakani ili wahujumu mali za klabu hiyo.

"Wanasumbuliwa na njaa, ni njaa tu inawasumbua hao. Zipo njia sahihi za kikatiba za kuutoa madarakani uongozi. Wasubiri uchaguzi mkuu wa Simba," alisema kiongozi huyo anayesifika kwa lugha ya vijembe.

Siwataji walioficha mabilioni Uswisi ng’o, Zitto


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amevunja ukimya na kusema hayuko tayari kwa sasa kuwataja Watanzania wenye mabilioni huko Uswisi na kuitaka Serikali ifanye uchunguzi.
Zitto ndiye aliyeibua hoja bungeni kuwa kuna Watanzania walioficha Sh315 bilioni katika taasisi za fedha nchini Uswisi.
Katika taarifa yake aliyoitoa jana, Zitto alisema anasita kutaja majina hayo sasa ili kuepusha kile alichosema majina hayo kutumiwa vibaya bila kujali kama Watanzania walizipata fedha hizo kihalali au la na kuzihifadhi nje ya nchi.
Alisema ameshauri mchunguzi wa kimataifa anafaa kufanya kazi hiyo.
Mbunge huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), amesema wastani wa Sh729.3 bilioni hutoroshwa kila mwaka kwenda nje ya nchi.
Alisema kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema kwamba yeye (Zitto) hakutoa ushirikiano wa kamati inayochunguza sakata hilo si ya kweli.
“Nataka niwahakikishie, nimekutana mara nne na kamati hii. Nimewapa mpaka jina la mchunguzi wa kimataifa atakayeweza kuwasaidia katika uchunguzi huu, leo naambiwa sitoi ushirikiano,” alisema Zitto.
Alisema mchunguzi huyo wa kimataifa ana uzoefu katika uchunguzi wa suala kama hilo na angeweza kuwatambua kwa majina na kiasi cha fedha na pia uhalali na uharamu wa fedha hizo.
Alisema ameshangazwa na hatua ya Serikali kumbeza pale alipopendekeza suala la kutafutwa mchunguzi wa kimataifa lakini siku chache baadaye ikatangaza magazetini nafasi ya kazi hiyo.
Tangazo hilo lilichapwa Desemba 17, mwaka huu siku ambayo Zitto alisema kwamba angesoma maelezo binafsi kujibu kauli ya Jaji Werema. Hata hivyo, alisema alikosa nafasi. Zitto amesema hashurutishwi na azimio la Bunge kutaja majina hayo kwa sababu yeye siyo chombo cha uchunguzi ambacho kinapaswa kuwa na mkono mrefu.
Alisema wakati akikabidhi majina ya Watanzania hao, angependa ushahidi huo uwe umefanyiwa uhakiki na vyanzo vyake vya kimataifa na vyombo vya usalama vya Serikali nchini.
“Siko tayari kutaja kwa sasa. Narudia tena kwa sasa hayo majina maana naweza kusababisha wahukumiwe na umma bila kupitia utaratibu uliowekwa na sheria zetu hapa nchini,” alisema Zitto.
Alisema inawezekana pengine shinikizo hili linatoka kwa watuhumiwa wenyewe baada ya kuona watu wengine waliokumbwa na kashfa nyingine walitajwa majina na hakuna hatua zilizochukuliwa.
“Mimi kama kiongozi makini na kama wasiwasi huu nilionao utakuwa wa kweli basi siko tayari kurudia makosa yaleyale ya kutaja majina halafu ikaishia hapo bila wahusika kushughulikiwa,” alisema.
Alisema suala la utoroshaji wa fedha nje ya nchi ni kubwa kuliko Watanzania wa kawaida wanavyolifahamu na kusema hilo ni janga la kitaifa na kimataifa na si la Zitto pekee.
Akitoa mfano, Zitto alisema uchunguzi unaonyesha mwaka 2010 pekee, kiasi cha Sh2.1 trilioni kilitoroshwa hapahapa nchini na mwaka 2011 kiasi cha Sh1.3 trilioni kilitoroshwa kwenda nje.
Alisema taarifa za mashirika ya kimataifa zinaonyesha kuwa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, kiasi cha fedha kilichotoroshwa hapa nchini na kupelekwa nje ya nchi ni Sh7.3 trilioni.
Zitto alisema hali hiyo si nzuri hata kidogo kwani inatokea wakati kuna Watanzania wanaoishi katika lindi kubwa la umaskini na kutahadharisha kuwa ipo siku kundi hilo linaweza kuchukua hatua.
“Nawaomba wenzangu waifanye vita hii kama ya Watanzania wote, wafahamu wale wenye masilahi na fedha hizi hawataacha kufanya kila njia kubeza vita hiyo. Mimi ni mpuliza filimbi tu katika vita hii na Watanzania wajue sina uwezo wa kuishinda vita hii peke yangu bila kuungwa mkono na wabunge, wananchi na hata Serikali.”

Watatu mbaroni kwa tuhuma za kumteka, kumtesa Absalom Kibanda


Absalom Kibanda, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)

Watu watatu wametiwa mbaroni kwa tuhuma za kumteka, kumtesa na kumjeruhi Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda.
Katika tukio hilo, Kibanda aling'olewa meno pamoja na kutobolewa jicho na watu wasiojulikana.

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Kamishna wa Polisi, Isaya Mngulu, alisema kuwa watu watatu wanashikiliwa mpaka sasa na wanahusishwa na tukio hilo.

Mngulu alisema kinachoendelea kwa sasa ni kwa Jeshi hilo kujiridhisha ikiwa ni pamoja na kukusanya ushahidi wa kutosha kuhusu watuhumiwa hao kuhusika kwenye tukio hilo ili wafikishwe mahakamani.


“Jeshi limefanikiwa kuwakamata watu watatu kwa tuhuma za kuhusika na tukio hilo, lakini kwa sasa upelelezi unaendelea kwani bado tunakusanya ushahidi wa kutosha ili tujiridhishe kwa watuhumiwa hao kuhusika na tukio hilo kabla hatujawafikisha mahakamani,” alisema Mngulu.

Kauli ya DCI inakuja baada ya kuwapo kwa kauli tofauti na tata zilizowahi kutolewa na jeshi hilo na serikali tangu kutokea kwa tukio hilo juu ya matukio ya Kibanda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk. Steven Ulimboka.

Moja ya kauli iliyowahi kutolewa na Jeshi la Polisi ni ile ya kivihusisha vyombo vya habari kuwa vilichangia upelelezi wa matukio hayo kuzorota kutokana na kuandika sana ikiwamo wanaohusika na upelelezi (vyombo vya usalama) kushutumiwa.

Novemba, mwaka huu, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa na Rais hivi karibuni, Dk. Emmanuel Nchimbi na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, walilazimika kulizungumzia suala hilo baada ya waandishi wa habari kutaka ufafanuzi kutoka kwao.

Waandishi walihoji iweje upelelezi wa tukio la kuvamiwa, kujeruhiwa na kuporwa kwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, marehemu Dk. Sengondo Mvungi, ukamilike na watuhumiwa kukamatwa haraka huku matukio hayo mawili yakiwa kimya.

Wakati Dk. Nchimbi na Kova wakisema hayo, Oktoba 14, mwaka huu, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, (DCI) mstaafu Robert Manumba, aliliambia NIPASHE kuwa uchunguzi wa uhalifu nchini wa kuteka, kutesa na kujeruhi raia pamoja na matukio mengine ya kumwagiwa tindikali upo njia panda kutokana na kukosekana kwa vifaa vya kisasa kuwabaini wahusika.

Manumba alisema katika kupeleleza matukio hayo, polisi wanakabiliana na changamoto za kubaini wahusika kutokana na kutumia teknolojia duni pamoja na kukosa wataalam.

Alishauri kila taasisi ikiwamo misikiti, makanisa na sehemu nyingine zenye mikusanyiko ya watu wengi, kufunga kamera (CCTV) ili kusaidia kubaini namna uhalifu unavyotokea. Hata hivyo, ushauri wa Manumba wa kufunga kamera kwenye nyumba za ibada, hauwezi kubaini uhalifu ambao umeshatendwa siku zilizopita.

KAULI YA KOVA
Akijibu hoja hiyo, Kamanda Kova alisema kila tukio lina mazingira yake na hakuna linalofanana na lingine kwa asilimia 100, hivyo matukio hayo (ya Kibanda na Dk. Ulimboka) na la Dk. Mvungi, hayafanani kimazingira na kinyakati.

“Safari hii (katika tukio la marehemu Dk. Mvungi), media (vyombo vya habari) vimekuwa kimya hata tulivyowaomba wasiandike walikubaliana nasi, ndiyo maana upelelezi ukawa rahisi…matukio ya Kibanda na Ulimboka, yaliandikwa sana na wanaopeleleza walituhumiwa,” alisema.

Aidha, aliviomba vyombo vya habari kunyamaza kunapokuwa na tukio linalohitaji upelelezi ili kutoa nafasi kwa Idara ya Upelelezi kufanya kazi vizuri.

“Tukio la Dk. Mvungi liwe fundisho jema kwa vyombo vya habari kuwa kunapotokea tukio watuachie Polisi na vyombo vingine vya usalama tupeleleze ndipo tuwape taarifa,” alisisitiza Kova.

Hata hivyo, alipobanwa aeleze upelelezi umefikia wapi na iwapo kuna wanaoshikiliwa, Kova alisema: “Tusiyazungumzie ya Kibanda na Ulimboka jibu tulilotoa awali linatosha.”

KAULI YA NCHIMBI
Dk. Nchimbi aliwahi kusema kuwa upelelezi wa matukio hayo (la Kibanda na la Dk. Ulimboka), unaendelea na hata kama utachukua muda mrefu kiasi gani ni lazima waliohusika wakamatwe.

“Ninaandaa semina kwa waandishi wa habari niwaonyeshe mikanda ya matukio ya uhalifu nchi mbalimbali duniani na jinsi upelelezi ulivyofanyika …tunaweza kutumia miaka mitatu hadi minne na tukawakamata watuhumiwa,” alisema.

Dk. Nchimbi alisema kabla ya Desemba 31, mwaka huu, itaundwa Kurugenzi ya Intelijensia na itakuwa na Kamishna ikiwa ni pamoja na kuwa na mafunzo ili kuharakisha upelelezi.

Mara kadhaa, Jeshi la Polisi limekwepa kuzungumzia tukio la kutekwa, kupigwa na kuteswa kwa Kibanda huku kukiwa na kurushiana ‘mpira’ kati ya Kova, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), na Mkuu wa Jeshi hilo, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema.

Kibanda ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited ambayo ni wachapishaji wa magazeti ya Rai, Dimba, Mtanzania, Bingwa na The African, alivamiwa na watu hao, wakati akirejea nyumbani kwake, Mbezi Juu, jijini Dar es Salaam Machi 5, mwaka huu.

Katika tukio hilo, watu hao walimng’oa meno, kumkata kidole, kumjeruhi kwa kitu kizito kichwani na kumharibu jicho la kushoto.

Mara baada ya tukio hilo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso, alimkariri IGP Mwema, akisema kuwa ameunda timu ya wapelelezi wazoefu kufanya uchunguzi ili kuwabaini waliohusika katika uhalifu huo na kuwatia mbaroni. Timu hiyo ya makachero wanne kutoka makao makuu ya polisi iliunganisha nguvu na makachero wa Jeshi hilo Kanda Maalum ya Dar es Salaam, ambayo hadi sasa haijatoa matokea ya uchunguzi huo, licha ya kuwapo kwa ahadi za kufanya hivyo mara kadhaa.
Jukwaa la Wahariri Tanzania kwa kushirikiana na Baraza la Habari Tanzania (MCT), waliunda timu kuchunguza tukio hilo na kutoa taarifa iliyohusisha tukio hilo na sababu mbalimbali ikiwamo kazi yake ya uandishi wa habari.

Dk. Ulimboka alikutwa na tukio hilo Juni 27, mwaka 2012 na baada ya muda mfupi polisi walimkamata raia wa Kenya, Joshua Gitu Mulundi (31), kwa madai ya kuhusika na tukio hilo na kufikishwa mahakamani.

Baada ya kitambo, Mwendesha Mashitaka wa Serikali aliamua kufuta kesi dhidi yake na aliachiwa huru kabla ya kukamatwa tena na polisi na kushtakiwa kwa kosa la kuwadanganya Polisi na kuhukumiwa kulipa faini ya Sh. 1,000 au kifungo cha miezi sita. Alilipa faini hiyo.

Aidha, Jeshi la Polisi mpaka sasa bado halijafanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wa matukio mawili ya mabomu yaliyotokea jijini Arusha na kusababisha vifo vya watu kadhaa.

Matukio hayo ni yale ya bomu lililotokea kwenye mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata tano wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Juni 14, mwaka huu na kuua watu wawili. Lingine ni lililotokea katika Kanisa Katoliki Parokia ya Olasiti Mei 5, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu wanne pamoja na kujeruhi watu kadhaa.

Matukio ambayo hata hivyo, Mngulu aliiambia NIPASHE wiki iliyopita kuwa Jeshi lake bado linaendelea na upelelezi na kwamba mpaka sasa limefanikiwa kumtia nguvuni mtu mmoja kwa tuhuma za kuhusika kwenye tukio la Olasiti na kesi yake iko mahakamani.

Alhamisi, 26 Desemba 2013

MKOANI MOROGORO GARI LILILOKUWA LIMEBEBA MAITI LAKAMATWA LIKIWA NA DAWA ZA KULEVYA

 

Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro,Faustine Shilogile akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).
Hizi ndio baadhi ya Pipi zilitolewa tumboni mwa Marehemu Khalid Kitala.
Baadhi ya Makachero wa Polisi wakijadiliana jambo baada ya kuona Mwili huo.
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro limefanikiwa kukamata gari dogo aina ya Toyota Spacio likiwa limebeba mwili wa mtu aliefari ambaye alitambulikwa kwa Jila la Khalid Kitala (47) na kukutwa na kete kadhaa za Madawa ya Kulevywa tumboni.

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Faustine Shilogile amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa walipata taarifa za kuwepo kwa gari  hilo toka kwa wasamalia wema ambao waliliona njiani, ambapo inasemekana lilikuwa linatokea Mkoani Mbeya kuelekea Dar.

Polisi wa mkoa wa Morogoro waliweka mtego wao kwenye kituo cha Mikumi na hatimaye kufanikiwa kukamata gari hilo likiwa na watu watatu ndani (majina yao yamehifadhiwa),pipi saba za vitu vinavyosadikiwa kuwa ni dawa za kulevya.

Mwili huo ulipelekwa hospitali na kufanyiwa uchunguzi na kukutwa na pipi nyingine kumi na saba tumboni mwa Marehmu huyo na inasemekana mtu huyo alifariki akiwa Mbeya.

Watu wote watatu ambapo wawili wanahusika na gari hilo na mmoja ni mfanyabiashara wa Kariakoo wanashikiliwa na polisi huko Morogoro.

WEMA,DIAMOND SIELEWI????? KATIKA SHOW YA ...........25 PATA HABARI NA PICHA.

sdd    

Hii ilikuwa jana pale Leaders club kwenye show ya Diamond ambapo Wema Sepetu alipanda kwenye stage na kuongea na mashabiki waliofika kwenye show hiyo.
Kwenye hiyo show Diamond aliuliza,”Mnataka kumjua mchumba wangu”?
 
Show ilivyoendelea Diamond alitaka kuimba wimbo wa ukimwona akasema, “Naskia ninayetaka kumuimbia wimbo huu yupo humuhumu ndani”.
Wema Sepetu akapanda kwenye stage wakaimba na kucheza wote.

379719_654725334570888_100223854_n
 

MCHEZAJI WA CHELSEA SAMUEL ETOO NA MKEWE WAKIFANYA YAO X-MASS...!


 

Jumatano, 25 Desemba 2013

BAADA YA RUBEN,FALCAO NAYE ATETA YAKE: RONALDO NI MCHEZAJI BORA ZAIDI YA LIONEL MESSI

Mshambuliaji wa Monaco  Radamel Falcao anaamini kwamba mshambuliaji wa Real Madrid  Cristiano Ronaldo ni mchezaji mzuri kuliko staa wa klabu ya Barcelona Lionel Messi.

Mchezaji huyo wa Colombia anawakubali wachezaji wote wawili, ingawa Falcao anaamini Cristiano ni bora zaidi ya Messi.

"Messi na Cristiano ni wachezaji muhimu na wakubwa duniani leo hii lakini, kwangu mimi naamini Ronaldo ni bora zaidi," alisema mchezaji huyo mwenye miaka 27 alipoongea na El Tiempo.

Falcao pia amesema ni Cristiano Ronaldo anayestahili kuwa mchezaji bora wa dunia katika tuzo za Ballon D'or zitakazotolewa mwezi ujao ambapo Ronaldo anapambana na Ribery pamoja na Messi.

MAMBO AMBAYO WANAUME WANAKOSEA WAKATI WA KUTONGOZA MWANAMKE

 


1.PAPARA
wanaume wengi tumekuwa na haraka sana tunapokuwa tukitaka kuaproach hali inayomfanya mwanamke akuwekee ugumu.mfano umekutana na dada mzuri mmesalimiana hapo hapo unamuomba namba yake.mjomba hata akikupa ujue utasumbuka sana kumpata coz atakufikiria sana juu ya uharaka wako.
 
2.KUJIFAKE
wanaume wengi tumekuwa tukijipandisha au kujionyesha tofauti na hali zetu.ukiwa unaaproach jaribu kuwa real.huwezi kumwambia mdada unafanya kazi benki afu uko na techno
 
3.KUTOSOMA MOOD YA MWANAMKE
unapomuaproach mwanamke lazma usome mood yake coz sometime unaweza kutoswa coz hujamsoma mwanamke.unamtongozaje mwanamke asubuhi?,,
 
4.KUMPONDA UR EX LOVER
mwanamke anakuuliza kwanini uko single,unaanza kumponda ex wako kwa maneno ya kashfa hali kama hii inaweza kumtisha kisaikolojia umtongozae.
 
5.KULALAMIKA
Unamtongoza mwanamke huku unalalamika juu ya mapenzi oooh mara sijawahi kupendwa.mjomba hapo unaonyesha udhaifu wako.

KOCHA SIMBA AFARIKI

                                                                                      

James Kisaka enzi za uhai wake.
Aliyekuwa kocha wa makipa wa Klabu ya Simba, James Kisaka amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Burhan, Dar es Salaam. Kisaka aliyewahi kuwa kipa wa timu hiyo miaka ya nyuma, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kichwa, macho na miguu kwa muda mrefu..

Ijumaa, 13 Desemba 2013

MAJESHI YENYE NGUVU ZAIDI AFRICA

The Global Fire Power ranking, or GFP, measures countries’ military strength and assigns a power index number in order to compare them to other countries. Many factors are taken into consideration, and smaller countries can compete with larger ones due to points given for refinement and technological advancement.
Just seven African countries are ranked by the GFP. An inadequate amount of information is available to compare other countries that are not included. Based on available information, the following countries represent the most powerful militaries on the African continent in 2013, according to GlobalFirepower.com.
Numbers reflect each country’s power index, derived from a unique algorithm developed by GFP. A perfect score is a 0.0000. The lower the number, the stronger the military, and bonuses and penalties are added to country scores as needed.

1. Egypt – Power Index: 0.7569

Egypt is put over the top with regard to military strength due to the sheer size of its armed forces. Nearly 500,000 personnel serve on its active frontline force, far surpassing all of its African neighbors, as well as its nearly 10,000 armored fighting vehicles, 60,000 logistical vehicles, 900 aircraft, and large oil reserve from which to draw. Again, the military has been somewhat undermined in the wake of the Egyptian Revolution, but some argue that its increased role in government has made it stronger than ever. Whether or not this is a cause for celebration or concern will remain hotly debated for some time to come.

2. Ethiopia – Power Index: 1.1725

As a landlocked country, Ethiopia has focused its resources on developing its army and air force to an impressive degree (the GFP doesn’t penalize landlocked countries for not having a naval force). Several hundred thousand personnel make up its current force, and they have significant numbers of land and air systems at their disposal. Furthermore, an enormous population that is fit for service allows Ethiopia to maintain the capacity to turn out an even larger fighting force, and gives the country one of the greatest militaries on the continent.

3. South Africa – Power Index: 1.2582

As it hasn’t been embroiled in an international military conflict for some time, South Africa uses its highly advanced military for more peacekeeping and international cooperation purposes. Its aircraft and naval vessels are notoriously well-equipped with the latest technology, and though the country has less than 100,000 active frontline personnel, it has the capabilities and manpower for much more. Add to that a vast array of land system technology, and the South African military is indeed a force to be reckoned with.

4. Nigeria – Power Index: 1.3441

Due to its size, it’s no surprise that several hundred thousand troops comprise the Nigerian Armed Forces, through its army, navy, and air force. Like Algeria, an abundant domestic oil supply eases the financial burden to be involved in military conflict, and it has more than 1,400 armored vehicles, 360 tanks, and 6,000 logistical vehicles at its disposal, as well as nearly 300 aircraft and 25 high-powered naval vessels.

5. Algeria – Power Index: 1.4107

As Algeria has a large maritime border, it has developed all of its military capabilities to an impressively modern degree, including its land, sea, and air forces. Algeria’s active frontline personnel numbers more than 127,000 troops and it has nearly 2,000 armored fighting vehicles at its disposal. Algeria also has the added benefit of its own oil reserves, allowing it to use its own fuel to power tanks, aircraft carriers, naval vessels, and more.

6. Kenya – Power Index: 1.6237

Kenya has established itself as a vital participant in international peacekeeping missions, and is able to do so due to a high merchant marine strength and an enormous labor force – resulting in high available manpower. Though it doesn’t possess as much of its own equipment, its role as a member of international teams allows the Kenyan military to share resources with other countries, strengthening its own capabilities at the same time.
7. Libya – Power Index: 1.8428
The strength of Libya’s military comes mainly from its large cache of equipment, despite a relatively small number of active troops. Further hampering Libya’s abilities is the continuing violence and unrest stemming from the revolution begun in 2011 which has yet to see a stable government emerge from it. Regardless, the country still has available 2,500 armored fighting vehicles, 500 tanks, 600 towed artillery pieces, 6,500 logistical vehicles, and much more.

Jumatatu, 2 Desemba 2013

Misri yaandaa rasimu ya katiba mpya

Mkuu wa rasimu mpya ya katiba ya Misri Amr Moussa (Kushoto), mjini Cairo, Dec. 1, 2013.

Jopo la wajumbe 50 limepitisha pendekezo la rasimu ya  katiba mpya ya Misri itakayopigiwa kura na wananchi mapema mwakani.
 
Pendekezo hilo ni hatua ya awali katika juhudi za kurejesha utawala wa kidemokrasia baada ya kutimuliwa mwezi Julai kwa rais Mohamed Morsi. Pia itachukua nafasi ya katiba yenye utata iliyoidhinishwa na rais wa Kiislam Morsi.

Katiba mpya inataka uchaguzi wa rais na bunge kufanyika ndani ya kipindi cha miezi sita baada ya wapiga kura kuipitisha.

Lakini itakuwa ni chaguo la rais wa mpito Adly Mansour kuamua ikiwa uchaguzi utafanyika kwanza.

Tamko la Chadema Kigoma na kuhusu ziara ya Dr. Slaa na tishio la usalama.

chadema 
Hii ni taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo Dec 2 2013 likiwa ni tamko la kikao cha mkoa Chadema Kigoma.

Ni kuhusu Kikao kilichofanyika ofisi ya Mkoa Ujiji kilibeba AGENDA ya Kujadili na Kuboresha ujio wa ziara ya Katibu Mkuu (T) Dr. P. Slaa Mkoani Kigoma 5/12/2013 ambapo atatembelea majimbo yote 8 ya mkoa Kigoma kwa mikutano si chini ya miwili kwa kila jimbo na baadae mkutano wa mwisho, jioni Mkutano ufanyike makao Makuu ya 

Jimbo lengo likiwa ni kuangalia uhai wa chama.
Mambo makuu na muhimu yalizingatiwa ambapo usalama kwa Kiongozi huyo kufutia sakata la Maamuzi ya kamati kuu dhidi ya Mhe.Zitto na mapokeo ya wanachama wetu.

Kutoa taarifa rasmi kwa majimbo na kupokea hali ilivyo au inavyoonekana katika maeneo yao.
Baada ya Tafakuri ya kina na ya Hekima na Busara pevu katika ujio huo iliazimiwa ifuatavyo

i.Mkoa uliomba Taifa lihairishe na kusogeza mbele tarehe ya ziara hiyo muhimu kwa mkoa wetu ili Mkoa kama ngazi ya chini ya Kanda na Taifa uweze kwenda katika majimbo hayo na kuwaelimisha wanachama na wapenzi wetu juu ya kuheshimu na kuwa na nidhamu na maamuzi yatolewayo na ngazi ya juu yetu hata kama yanamaumivu ….katiba ifuatwe katika kutatua tatizo – Maoni ya Wengi Mkoani na Viongozi wa Chama ni kuudhiwa na maamuzi ya k/kuu ambayo dhahiri yalilenga Zitto – Kisiasa.

ii.  Mkoa ulitishika na vitisho baada ya kupokea taarifa toka kwa baadhi ya viongozi wa majimbo ya mkoa kwamba hali ya usalama si nzuri kwa ujio wa kiongozi Dr. Slaa kufika Kigoma kwa kipindi hiki wakati wanachama na wapenzi wakitafakari na kwa kauli tofauti zisizolenga kuwepo usalama.

 iii.           Kwa hekima ya kikao kilijiridhisha kwa kupata maoni toka katika majimbo 6 kuwa hali ni mbaya kabisa wakishauri Katibu mkuu asogeze mbele ziara yake kupisha mtafaruku huu na kwa usalama wa Chadema na viongozi wake Kitaifa.

iv.          Hivyo Mkoa kupitia kikao hicho ikaonekana ni bora kuzuia kuliko kutibu, tayari sintofahamu zimeonekana, viongozi na hasa wa majimbo kutofautiana mitazamo ni HATARI katika hali hiyo, mkoa ulijiridhisha usalama hautakuwepo kwa ujumla hata kama baadhi ya majimbo yakisema wao wapo salama tu.

v.            HOFU/TAHADHARI -   Endapo hali haitokuwa salama Mungu apishe mbali.
Mkoa hautokwepa lawama na uzembe wa makusudi kwani wajibu wa ngazi ya chini ni kutoa ushauri kwa ngazi ya juu hivyo mkoa unatoa ushauri kwa Makao Makuu (T) Chadema kusogeza mbele ziara hiyo hadi hali itulie na mkoa upite majimboni kujiridhisha na usalama kwa viongozi wake na hasa wa Taifa.

LENGO KUU:   NI KUHAKIKISHA CHADEMA TUNAPITA SALAMA KATIKA WAKATI HUU MGUMU KWETU – CHADEMA
 ALHAJ. JAFARI KASISIKO                                           MSAFIRI WAMALWA
M/KITI MKOA                        01/DEC.2013                KATIBU MKOA
 
 
Blogger Templates