Social Icons

Alhamisi, 30 Januari 2014

M4C:AFANDE SELE ATISHA MOROGORO(CHADEMA).


Maelefu ya wakazi wa mkji wa Ifakara, wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mweneyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jana.
Mwenyekiti wa Chama ch Demokrasia na Mendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwahutubia maelfu ya wakzi wa mji wa Mtibwa katika mkutano wa Operesheni M4C pamoja Daima jana.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akimtambulisha mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Afande Sele, wakati wa mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Dama, uliofanyika katika Kata ya Tungi mjini Mororgoro jana.
Baadhi ya wa mji wa Ifakara wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali, wakati wa mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana. 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokreasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee wakiondoka baada ya kuhutubia mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika mjini Ifakara jana.
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akiwahutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mtibwa, katika mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, uliofanyika jana, ambao pia ulihutubia na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe,
Sehemu ya maelfu ya wakazi wa mji wa Ifakara, wakitawanyika baada ya mkutano wa Operesheni M4C Pamoja Daima, ambao ulihutubiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe jana.

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya, Afande Sele akiwahutubia wananchi wa Kata ya Tungi mjini Morogoro leo, katika mkutano wa hadhaa wa Operesheni M4C Pamoj Daima. Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe alihutubia pia

Makunga, Kibanda washinda kesi ya uchochezi

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru Meneja Uendelezaji Biashara wa Kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Theophil Makunga, Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006), Absalom Kibanda na Samson Mwigamba katika kesi ya makala ya uchochezi iliyokuwa ikiwakabili.
Makunga na wenzake hao, walikuwa wakikabiliwa na kesi ya uchochezi dhidi ya askari wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kuchapisha makala kwenye Gazeti la Tanzania Daima iliyokuwa ikidaiwa kuwa na maneno yaliyolenga kushawishi askari majeshi ya ulinzi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM), Polisi na Magereza wasiwatii viongozi wao.
Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema alisema kwa mtu yeyote mwenye kutafakari kwa makini hawezi kuita makala hayo ya Novemba 30, 2012 yaliyoandikwa na Mwigamba kwenye gazeti hilo yakiwa na kichwa cha habari ‘Waraka maalumu kwa askari wote’ kuwa ni uchochezi.
Hakimu Lema alisema hayo baada ya kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi watatu wa upande wa mashtaka ambao ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo-Usajili wa Magazeti), Raphael Hokororo, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza (ACP), George Mwambashi kutoka Kitengo cha Sheria cha kikosi hicho na Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP), David Hizza.
Alisema kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi hao, upande wa mashtaka umeshindwa kueleza jinsi washtakiwa hao walivyoshiriki kwenye makala yanayodaiwa kuwa ni ya uchochezi na kwamba walishtakiwa kwa hisia ambazo haziwezi kumtia mtu hatiani.
Hakimu Lema alieleza kuwa sheria ya jinai haihusishi kampuni, bali mtu hivyo upande wa mashtaka ulipaswa kuithibitishia Mahakama namna washtakiwa hao kila mmoja kwa wakati wake, alivyoshiriki kutenda kosa hilo kwa kuwa walikuwa na watu wengi waliokuwa wakiwasaidia katika kazi zao.
Alisema ushahidi huo hakuonyesha wala kuunga mkono namna Kibanda au Makunga walivyohusika kuchapa au kuhariri makala hayo yanayodaiwa kuwa ya uchochezi na kwamba ushahidi huo pia haujaonyesha kuwa ni ya uchochezi.
Alisema hata mashahidi wa upande wa mashtaka waliiambia Mahakama hiyo kuwa hakuna kitu chochote wala madhara yaliyowahi kutokea kwenye majeshi yao ya ulinzi ambayo ndiyo yaliyokuwa walengwa wa makaa hayo.
Upande wa mashtaka ulidai kuwa makala hayo yalikuwa ya uchochezi na kuwa yaliwashawishi askari wasiwatii viongozi wao ukiegemea Kifungu cha 32 (1)(c) na Kifungu cha 31(1)(a) cha Sheria ya Magazeti ambacho kinasema endapo litatokea kosa kwenye gazeti, mtu yeyote aliyeandika, kuchapisha na kusambaza atakuwa ametenda kosa.
“Machapisho ya uchochezi ni lazima yaonyeshe athari au madhara kwa kuleta uvunjifu wa amani, chuki, uhasama...” alisema Hakimu Lema.
Alisema SSP Hizza alikuwa mpelelezi wa kesi hiyo na mlalamikaji lakini katika ushahidi na hata uchunguzi wake, hakuwahi kuiambia Mahakama jinsi ambavyo kila mshtakiwa alivyohusika na kwamba Hokororo aliona hakuna tatizo lolote kwenye makala hayo ndiyo maana hakuchukua hatua yoyote dhidi yao.
Hakimu Lema alisema makala hayo hayakuwa na kitu chochote cha ajabu na kwamba Mwigamba alikuwa akijaribu kutumia haki yake ya kikatiba ya uhuru wa kujieleza na huku akisisitiza kuwa hayakuwa na nia ovu, bali maelezo binafsi na kuongeza kuwa upande wa mashtaka uliifungua kesi hiyo kwa hisia.
Alisema wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo, SSP Hizza alimhoji mhariri lakini hakupeleka mahojiano hayo mahakamani kama kielelezo cha ushahidi.
Kwa upande wa ushahidi wa mshtakiwa Mwigamba, Hakimu Lema alisema ushahidi unaonyesha kwamba aliandika makala hayo kutokana na tukio la vurugu zilizotokea mkoani Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu.
Alisema ili makala yathibitike kuwa ya uchochezi ni lazima kuwepo ama chuki au uvunjifu wa amani mambo ambayo hayakuonekana kwenye ushahidi wote wa upande wa mashtaka.
“Kutokana na hayo nashawishika na ninaamini kuwa upande wa mashtaka pasipokuacha shaka waliifungua kesi hii kwa hisia na mshtakiwa Kibanda na Makunga hawahusiki katika kuchapa wala kuhariri na kwa upande wa Mwigamba hakuandika makala kwa nia ovu,” alisema na kuongeza kuwa anawaachia huru washtakiwa wote.
Makunga
Akizungumza baada ya hukumu hiyo, Makunga alisema miaka miwili ya kesi hiyo ilikuwa ya usumbufu kwake kwa kukosa uhuru binafsi katika shughuli zake za uandishi wa habari ikiwamo zuio la kutoka nje ya Dar es Salaam bila ruhusa ya Mahakama huku hati yake ya kusafiria ikishikiliwa.
Alisema akiwa mwandishi analazimika kwenda sehemu mbalimbali ikiwamo nje ya nchi lakini yote hayo yalikuwa yakishindikana kutokana na kukosa uhuru binafsi.
Alimshukuru Mungu na Mahakama kwa kutenda haki na kuwaachia huru huku akikumbuka tukio la Agosti 2013, aliponyimwa ruhusa ya kusafiri kwenda Kenya kuhudhuria mahafali ya binti yake.
Alisema hukumu hiyo imempa nguvu ya kufanya kazi kwa bidii na kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Kibanda
Kwa upande wake, Kibanda alisema haki ni lazima ishinde hata kama kuna nguvu za kiutawala. Alisema hilo limedhihirika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Alisema vyombo vya habari vimekuwa vikifanya kazi zake hususan kuandika habari kwa shaka na kwamba sasa uhuru wa habari umethibitika na wanahabari wanapaswa kusonga mbele.
“Mahakama imeweka alama ya kipekee, siyo Tanzania tu, bali kimataifa, vyombo vya habari bado vina alama ya kushinda,” alisema Kibanda.
Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Tido Mhando aliwataka waandishi wa habari kuzingatia misingi ya sheria na maadili ya uandishi wa habari. Alisema kilichoandikwa kwenye makala hayo kilikuwa kinaelimisha jamii.
Mhariri Mtendaji Mkuu wa MCL, Bakari Machumu alisema matukio yaliyotokea hivi karibuni yaliwatia hofu waandishi wa habari kwa kuingiliwa uhuru wao na kwamba hukumu hiyo imetoa nuru na kuwatia moyo kusonga mbele kujenga nchi.
Wakili Nyaronyo Kicheere ambaye pia alikuwa akimtetea Makunga alisema hukumu ya kesi hiyo ni ushindi kwa waandishi wa habari.
Kicheere alisema makala ya Mwigamba yalikuwa na lengo la kutoa elimu kwa vyombo vya dola kwa jinsi vinavyopaswa kuwajibika kwa wananchi.
“Nadhani hukumu hii itatoa fursa kwa waandishi wa habari kuchambua vyombo vya dola vinavyofanya kazi,” alisema.
MWANANCHI

Makunga, Kibanda washinda kesi ya uchochezi

Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru Meneja Uendelezaji Biashara wa Kampuni ya Mwananchi Communications (MCL), Theophil Makunga, Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006), Absalom Kibanda na Samson Mwigamba katika kesi ya makala ya uchochezi iliyokuwa ikiwakabili.
Makunga na wenzake hao, walikuwa wakikabiliwa na kesi ya uchochezi dhidi ya askari wa majeshi ya ulinzi na usalama kwa kuchapisha makala kwenye Gazeti la Tanzania Daima iliyokuwa ikidaiwa kuwa na maneno yaliyolenga kushawishi askari majeshi ya ulinzi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM), Polisi na Magereza wasiwatii viongozi wao.
Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema alisema kwa mtu yeyote mwenye kutafakari kwa makini hawezi kuita makala hayo ya Novemba 30, 2012 yaliyoandikwa na Mwigamba kwenye gazeti hilo yakiwa na kichwa cha habari ‘Waraka maalumu kwa askari wote’ kuwa ni uchochezi.
Hakimu Lema alisema hayo baada ya kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi watatu wa upande wa mashtaka ambao ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo-Usajili wa Magazeti), Raphael Hokororo, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Magereza (ACP), George Mwambashi kutoka Kitengo cha Sheria cha kikosi hicho na Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP), David Hizza.
Alisema kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi hao, upande wa mashtaka umeshindwa kueleza jinsi washtakiwa hao walivyoshiriki kwenye makala yanayodaiwa kuwa ni ya uchochezi na kwamba walishtakiwa kwa hisia ambazo haziwezi kumtia mtu hatiani.
Hakimu Lema alieleza kuwa sheria ya jinai haihusishi kampuni, bali mtu hivyo upande wa mashtaka ulipaswa kuithibitishia Mahakama namna washtakiwa hao kila mmoja kwa wakati wake, alivyoshiriki kutenda kosa hilo kwa kuwa walikuwa na watu wengi waliokuwa wakiwasaidia katika kazi zao.
Alisema ushahidi huo hakuonyesha wala kuunga mkono namna Kibanda au Makunga walivyohusika kuchapa au kuhariri makala hayo yanayodaiwa kuwa ya uchochezi na kwamba ushahidi huo pia haujaonyesha kuwa ni ya uchochezi.
Alisema hata mashahidi wa upande wa mashtaka waliiambia Mahakama hiyo kuwa hakuna kitu chochote wala madhara yaliyowahi kutokea kwenye majeshi yao ya ulinzi ambayo ndiyo yaliyokuwa walengwa wa makaa hayo.
Upande wa mashtaka ulidai kuwa makala hayo yalikuwa ya uchochezi na kuwa yaliwashawishi askari wasiwatii viongozi wao ukiegemea Kifungu cha 32 (1)(c) na Kifungu cha 31(1)(a) cha Sheria ya Magazeti ambacho kinasema endapo litatokea kosa kwenye gazeti, mtu yeyote aliyeandika, kuchapisha na kusambaza atakuwa ametenda kosa.
“Machapisho ya uchochezi ni lazima yaonyeshe athari au madhara kwa kuleta uvunjifu wa amani, chuki, uhasama...” alisema Hakimu Lema.
Alisema SSP Hizza alikuwa mpelelezi wa kesi hiyo na mlalamikaji lakini katika ushahidi na hata uchunguzi wake, hakuwahi kuiambia Mahakama jinsi ambavyo kila mshtakiwa alivyohusika na kwamba Hokororo aliona hakuna tatizo lolote kwenye makala hayo ndiyo maana hakuchukua hatua yoyote dhidi yao.
Hakimu Lema alisema makala hayo hayakuwa na kitu chochote cha ajabu na kwamba Mwigamba alikuwa akijaribu kutumia haki yake ya kikatiba ya uhuru wa kujieleza na huku akisisitiza kuwa hayakuwa na nia ovu, bali maelezo binafsi na kuongeza kuwa upande wa mashtaka uliifungua kesi hiyo kwa hisia.
Alisema wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo, SSP Hizza alimhoji mhariri lakini hakupeleka mahojiano hayo mahakamani kama kielelezo cha ushahidi.
Kwa upande wa ushahidi wa mshtakiwa Mwigamba, Hakimu Lema alisema ushahidi unaonyesha kwamba aliandika makala hayo kutokana na tukio la vurugu zilizotokea mkoani Arusha na kusababisha vifo vya watu watatu.
Alisema ili makala yathibitike kuwa ya uchochezi ni lazima kuwepo ama chuki au uvunjifu wa amani mambo ambayo hayakuonekana kwenye ushahidi wote wa upande wa mashtaka.
“Kutokana na hayo nashawishika na ninaamini kuwa upande wa mashtaka pasipokuacha shaka waliifungua kesi hii kwa hisia na mshtakiwa Kibanda na Makunga hawahusiki katika kuchapa wala kuhariri na kwa upande wa Mwigamba hakuandika makala kwa nia ovu,” alisema na kuongeza kuwa anawaachia huru washtakiwa wote.
Makunga
Akizungumza baada ya hukumu hiyo, Makunga alisema miaka miwili ya kesi hiyo ilikuwa ya usumbufu kwake kwa kukosa uhuru binafsi katika shughuli zake za uandishi wa habari ikiwamo zuio la kutoka nje ya Dar es Salaam bila ruhusa ya Mahakama huku hati yake ya kusafiria ikishikiliwa.
Alisema akiwa mwandishi analazimika kwenda sehemu mbalimbali ikiwamo nje ya nchi lakini yote hayo yalikuwa yakishindikana kutokana na kukosa uhuru binafsi.
Alimshukuru Mungu na Mahakama kwa kutenda haki na kuwaachia huru huku akikumbuka tukio la Agosti 2013, aliponyimwa ruhusa ya kusafiri kwenda Kenya kuhudhuria mahafali ya binti yake.
Alisema hukumu hiyo imempa nguvu ya kufanya kazi kwa bidii na kukabiliana na changamoto mbalimbali.
Kibanda
Kwa upande wake, Kibanda alisema haki ni lazima ishinde hata kama kuna nguvu za kiutawala. Alisema hilo limedhihirika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Alisema vyombo vya habari vimekuwa vikifanya kazi zake hususan kuandika habari kwa shaka na kwamba sasa uhuru wa habari umethibitika na wanahabari wanapaswa kusonga mbele.
“Mahakama imeweka alama ya kipekee, siyo Tanzania tu, bali kimataifa, vyombo vya habari bado vina alama ya kushinda,” alisema Kibanda.
Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, Tido Mhando aliwataka waandishi wa habari kuzingatia misingi ya sheria na maadili ya uandishi wa habari. Alisema kilichoandikwa kwenye makala hayo kilikuwa kinaelimisha jamii.
Mhariri Mtendaji Mkuu wa MCL, Bakari Machumu alisema matukio yaliyotokea hivi karibuni yaliwatia hofu waandishi wa habari kwa kuingiliwa uhuru wao na kwamba hukumu hiyo imetoa nuru na kuwatia moyo kusonga mbele kujenga nchi.
Wakili Nyaronyo Kicheere ambaye pia alikuwa akimtetea Makunga alisema hukumu ya kesi hiyo ni ushindi kwa waandishi wa habari.
Kicheere alisema makala ya Mwigamba yalikuwa na lengo la kutoa elimu kwa vyombo vya dola kwa jinsi vinavyopaswa kuwajibika kwa wananchi.
“Nadhani hukumu hii itatoa fursa kwa waandishi wa habari kuchambua vyombo vya dola vinavyofanya kazi,” alisema.
MWANANCHI

N/WAZIRI WA FEDHA MH;MWIGULU NCHEMBA AAGIZA TRA KUHAKIKISHA HUDUMA ZOTE ZINAPATIKANA MKOA WA NJOMBE

Naibu Waziri wa Fedha Mh;Mwigulu Nchemba hii leo akiwa kwenye Ziara yake ya Kikazi Mkoani Njombe ameagiza Bodi na Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) Kuhakikisha Wanajenga Ofisi ndani ya Mkoa wa Njombe(M) haraka sana ilikuondoa Usumbufu Kwa Wafanyabiashara na Wananchi wanapohitaji huduma muhimu kama Leseni,Tin Number n.k.

 
Akizungumza na Wafanyabiashara Mkoa wa Njombe hii leo (30/01/2014) kwenye Ukumbi wa TURBO,Mh:Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa Ofisi yake imedhamiria kuhakikisha Njombe inapatiwa huduma zote zinazohusu TRA ilikuondoa usumbufu wanaoupata Wananchi hivi sasa kusafiri nje ya Mkoa kupata huduma.

Kwa muda mrefu Njombe kumekuwa na Ofisi ya TRA ambayo inatoa baadhi ya huduma kama Malipo ya Kodi,Kwenye Ulipaji wa Leseni,Tin No, n.k Wananchi wamekuwa wakilazimika kwenda Mikoa ya karibu kama Mbeya na Iringa kwaajili ya Kushughulikia huduma hizo.

Jumapili, 19 Januari 2014

MAWAZIRI WAPYA HAWA HAPA.

Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue.akitangaza baraza la mwaziri leo.
Hakuna Mabadiliko Ofisi ya Rais
Ofisi ya Makamu Wa Rais - Naibu Waziri Kitwanga amehamishwa na nafasi yake imejazwa na Mhe. Ali Mwalimu
Mwigulu Nchemba amekuwa Naibu Wizara ya Fedha (Sera). Aliyekuwa nafasi hiyo sasa ni Waziri Kamili
Uchumi na Mapato sasa anatoka Janet Mbene na inajazwa na Adam Malima
Dr. Asha rose Migiro sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria
Kwenye Ulinzi na Kujenga Taifa ni Dr. Hussein Mwinyi
katika Mambo ya Ndani - Mathias Chikawe
Afya na Ustawi wa Jamii - Naibu wake sasa ni Waziri Kamili; naibu wa sasa ni Dr. Kebwe S. Kebwe
Waziri Mulugo amepigwa chini rasmi . Nafasi yake imejazwa na Jenista Muhagama
D. Sophia Simba amebaki na naibu wake akiwa ni Pindi chana katika wizara ya Jinsia na watoto.
Katika wizara ya Mifugo na Maendeleo yake ni Dr. Titus Kamani mbunge wa Busega atakuwa Waziri mpya. Naibu wake ni Saning'o Kaika Telele na hivyo Wizara nzima imepata mawaziri wapya
Mhe. Ole Medeye Amepigwa chini na nafasi yake kuchukuliwa na George Simbachawene katika wizara ya Ardhi ila bado waziri wake ni Prof. Tibaijuka)
katika kilimo na Chakula waziri ni yule yule na Naibu wake ni Godfrey Zambi.
Wizara ya Habari na michezo waziri ni yule yule Dr. Fenella Mukangara ila naibu wake ni mpya , Mtangzaji wa zamani na mbunge wa Singida Bw. Juma Nkamia.
Maliasili na Utalii Nyalandu amekuwa Waziri Kamili. Naibu ni Mahmood Hassan Mgimwa
Katika Nishati na Madini ni Prof. Sospeter Muhongo na Naibu wake ni Charles Kitwagwa akiichukua toka kwa Simbachawene



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com
    press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425


    PRESIDENT’S OFFICE,                          THE STATE HOUSE,
         DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL                         COMMUNICATIONS,
           P.O. BOX 9120,  
            DAR ES SALAAM.
                 Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
______________________________________________
            Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-
1.0              OFISI YA RAIS
Hakuna mabadiliko.
2.0              OFISI YA MAKAMU WA RAIS
2.1  Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko
2.2   Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)
            Waziri wa Nchi (Mazingira).
2.3    Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)
                                                Naibu Waziri                            
3.0              OFISI YA WAZIRI MKUU
Hakuna mabadiliko
            4.0       WIZARA
           
                        4.1  WIZARA YA FEDHA
4.1.1        Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb)
            Waziri wa Fedha
                                    Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb)           
                        Naibu Waziri wa Fedha
4.1.2        Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Fedha
                       
4.2              WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Hakuna mabadiliko
           
4.3       WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
4.3.1    Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)
                        Waziri wa Katiba na Sheria
4.3.2        Naibu Waziri - Hakuna mabadiliko
4.4      WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
Hakuna mabadiliko
            4.5       WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA
           
4.5.1    Waziri - Hakuna mabadiliko
4.5.2    Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
            4.6       WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA
            Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)
                                                Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
           
4.7        WIZARA YA UJENZI
Hakuna mabadiliko
4.8       WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
4.8.1    Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)
                        Waziri wa Mambo ya Ndani
                       
4.8.2        Naibu Waziri - Hakuna Mabadiliko
           


4.9       WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
4.9.1        Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.9.2        Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.10     WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
4.10.1  Waziri:  Hakuna mabadiliko
4.10.2  Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
14.11   WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
14.11.1  Waziri: Hakuna mabadiliko
14. 11.2 Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
14.12  WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
14.12.1 Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb)
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.12.2 Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.13      WIZARA YA KAZI NA AJIRA
Hakuna mabadiliko
                                                              
14.14      WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Hakuna mabadiliko
14.15   WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
14.15.1  Waziri - Hakuna mabadiliko
14.15.2  Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb)
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
14.16   WIZARA YA MAJI
14.16.1  Waziri - Hakuna mabadiliko
14.16.2  Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)
Naibu Waziri wa Maji
14.17  WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA
14.17.1  Waziri - Hakuna mabadiliko
            14.17.2   Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb)
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
            4.18     WIZARA YA UCHUKUZI
            Hakuna mabadiliko
4.19     WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
4.19.1  Waziri -  Hakuna mabadiliko
4.19.2  Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb)
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
4.20     WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
4.20.1 Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)
Waziri wa Maliasili na Utalii
                        4.20.2 Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)
                                                Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
4.21     WIZARA YA NISHATI NA MADINI
4.21.1    Waziri - Hakuna mabadiliko
4.21.2    Naibu Waziri (Madini) - Hakuna mabadiliko
4.21.3  Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)
Naibu Waziri (Nishati)
           
Balozi Ombeni Y. Sefue
KATIBU MKUU KIONGOZI

Jumamosi, 4 Januari 2014

WATU 9 WAPOTEZA MAISHA KWENYE TUFANI YA THELUJI ILIOANGUKA DMV,PA, NY, CT NA MA.

Pendera ikionekana imechanika kwenye ufukwe wa Scituate Massachusetts baada ya tufani ya theluji iliyoanguka siku ya alhamisi Jan 2, 2014 na kusababisha vifo vya watu 9 mji wa Boston imeanguka theluji ipatayo futi 2 na kusababisha kufunga barabara kuu inayounganisha Pennsylvani, New York na Boston, viwanja vya ndege, Mssachusetts, New York vilisitisha safari za ndege mpaka hapo theluji itakapokwanguliwa na hali kuwa salama kwa ndege kuruka. Meya wa New York ilibidi atangaze hali ya dharura (State of Emergency) kwa wakazi wa jiji hilo lisilolala. Picha na Michael Dwyer
mpiga picha akipata ukodak moment kwa sananmu iliyotengenezwa kwa theluji karibu na Capitol Hill mjini Washington, DC. ambapo theluji ilianguka ipatayo inchi 3 mpaka 5 kwa maeneo mengine ya Virginia na Maryland. picha na Evan Vucc
Daraja la RFK New York lilivyokua likionekana siku ya Ijumaa Jan 3, 2014 baada ya theluji kuanguka siku ya alhamis jioni na kusababisha shule na ofisi za serikali kufungwa. Picha na John Minchillo
Watembea kwa miguu wakivuka barabara siku ya alhamisi kwenye jiji lisilolala la New York wakati theluji ilipokua ikidondoka. picha na John Minchillo
Maeneo ya Time Square yalivyoakua yakionekana wakati theluji ilivyokua ikianguka

CHADEMA YATOA MAELEZO KUHUSU PINGAMIZI ALILOWEKA MBUNGE WA KIGOMA KASKAZINI-CHADEMA ZITTO KABWE MAHAKAMA KUU.

 
 Mmoja wa wanachama watatu wa CHADEMA waliovuliwa nafasi zao za uongozi ndani ya chama, Zitto Kabwe kupitia kwa Wakili wake, Alberto Msando,jana ameanza kufanya ‘FORUM SHOPPING’ kwa kupeleka maombi Mahakama Kuu ya Tanzania, akiomba Kamati Kuu isijadili na kuamua jambo lolote kuhusu uanachama wake, kwenye kikao maalum kinachofanyika leo.

Awali muombaji kwa namna ambayo inaweza kuitwa kuwa ni kuvizia, alitaka Mahakama Kuu hiyo itoe amri kutokana na ombi lake hilo, bila upande wa chama kuwepo mahakamani, lakini kwa bahati nzuri mawakili wa chama, Mwanasheria Mkuu wa chama, Tundu Lissu na Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu, Peter Kibatala; wakafanikiwa kuwepo kortini, hivyo wakawa-served maombi hayo kisha mahakama ikalazimika kusikiliza Preliminary Objections (PO) kutoka kwa mawakili wa CHADEMA dhidi ya waleta maombi.

Maombi hayo ya wakili Msando kwa niaba ya Zitto yamefunguliwa mahakamani dhidi ya Baraza la Wadhamini CHADEMA na Katibu Mkuu wa Chama.

Hoja za mawakili wa CHADEMA katika PO zilikuwa ni katika maeneo matatu ambayo ni vifungu vya kisheria ambavyo waombaji walikosea;

1. Vifungu vya sheria walivyotumia waombaji kuomba court injunction, haviipatii Mahakama Kuu mamlaka ya kufanya maamuzi hayo wanayoomba ifanye. Kwa sababu kwa ujumla ukikosea vifungu hasa vinavyohusu msingi wa kesi, ni sawa na kwamba hakuna kesi.

2. Hati ya kiapo ya waleta maombi haikuwa na facts kama inavyotakiwa badala yake ilikuwa imejaa maneno ya ubishi ubishi.

3. Mahakama haiwezi ku-entertain kusikiliza migogoro ya ndani katika vyama vya hiari mf; vyama vya siasa, dini na michezo (ambavyo uanachama wake ni wa hiari), kwa sababu mojawapo ya principle ni kwamba ili mtu awe mwanachama anakuwa amekubaliana na katiba, kanuni, taratibu na makatazo ya chama husika.

Aidha katika maombi yake kuna vitu vingine ‘muhimu’ ambavyo mleta maombi amejikuta akivionesha kuwa anakubaliana na taratibu za chama lakini wakati huo huo tena anataka mahakama imsikilize;

· Amekiri kuwa amevuliwa nafasi za uongozi na amekata rufaa

· Amekiri kuwa ameandikiwa mashtaka kwa maandishi na yeye amejibu

· Amekiri kuwa ameandikiwa kuitwa mbele ya kikao cha Kamati Kuu ili asikilizwe utetezi wake kwa mdomo.

Kwa maneno yake hayo ni kwamba anakubaliana na na process ya chama na kwamba anajua atasikilizwa lakini tena wakati huo huo anataka mahakama imsikilize. Huo ndiyo msingi wa Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA kusema kuwa kuhangaika huko ni sawa na kufanya ‘FORUM SHOPPING’.

Mleta maombi angeweza kuwa na hoja katika maombi yake iwapo angeona kuna breach of natural justice kwenye suala lake. Kitu ambacho hakijatokea na hata yeye kwenye maelezo yake anakiri hivyo.

Uamuzi wa Mahakama Kuu

Katika uamuzi wake, Jaji Utamwa amesema chama kitaendelea na shughuli zake kama kawaida.

Hivyo kikao maalum cha Kamati Kuu kilichopangwa kufanyika kesho Januari 3, 2014, kitafanyika na kitajadili agenda zote (kama zilivyotolewa awali) na masuala yote yanayohusu uendeshaji wa chama, isipokuwa hakitajadili na kuamua kuhusu uanachama wa Zitto pekee, hadi Mahakama Kuu itakaposikiliza ombi lake kesho saa 3 asubuhi.

Imetolewa na-


Kurugenzi ya Habari-Chadema
 
 
Blogger Templates