Social Icons

Jumamosi, 30 Novemba 2013

RAIS KIKWETE APOKEA KOMBE LA DUNIA JIJINI MWANZA JANA

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akilifunua Kombe la Dunia katika uwanja wa michezo Kirumba mjini Mwanza jana jioni.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akianza kulinyanyua Kombe la Dunia katika uwanja wa michezo Kirumba mjini Mwanza jana jioni. Kombe hilo limerejea jijini Dar es Salaam na leo wananchi watapata fursa ya kupiganalo picha.


 

Hapa ni furaha tu

Rais Jakaya Kikwete Apewa Rasmi Uchifu(Chifu Ng’humbu Banhu)Bariadi

 
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amekalia kigoda cha Uchifu wa Bariadi baada ya kuwa Chifu Ng’humbu Banhu mjini Bariadi Mkoa mpya wa Simiyu jana .Rais Kikwete yupo katika Ziara ya Kikazi Mkoa mpya wa Simiyu
Mmoja wa machifu wa Kisukuma eneo la Bariadi ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge akimvika vazi la kijadi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kumpa uchifu Rais Kikwete iliyofanyika mjini Bariadi,Mkoa mpya wa Simiyu  jana .Rais Kikwete alipewa jina la kisukuma la Chifu Ng’humbu Banhu lenye maana ya Anayekumbuka na kuthamini Watu.

EAC Heads Sign the Protocol Monetary Union


D92A8753
 
D92A8856
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete together with his East African Heads Of States Counterparts shortly after they signed the Protocol on the Establishment of the East African Monetary Union at Speke’s Bay Resort Munyonyo in Kampala this afternoon.Others from Left Presidents Pierre Nkurunzinza of Burundi, Yoweri Kaguta Museveni of Uganda, The new EAC chairman Uhuru Kenyatta of Kenya, and Paul Kagame of Rwanda.  

Ijumaa, 29 Novemba 2013

HON.DR.MAKONGORO MAHANGA,DEPUTY MINISTER FOR LABOUR&EMPLOYEMENT,AZINDUA YOUNG PROFESSIONALS& ENTERPRENEURS FORUM.




HON.DR MAKONGORO MAHANGA DEPUTY MINISTER FOR LABOUR EMPLOYEMENT,amelezea kwamba vijana tufikirie kujiari badala ya kufikilia kuajiriwa ingawa kunachangamoto nyingi
.
MR.KEVIN LUANDE,MD-GOLDEN WAVES LTD,ambaye ndio mwanzilishi wa young profesionals&Entrepreneurs forum.
 CEO-ENTERPRISE GWROTH MARKET ADVISERS(EGMA),alielezea jinsi ya kutafuta mikopo kwa jiri ya wajasiamari na pia jinsi ya kuiweka biashara yako katika hali sahiii
Wauzuriaji wakipata mda wakuuliza maswali.
Muheshimiwa,Dr,Makongoro Mahanga-aliye shika kipaza sauti akijibu baadhi ya maswali alio ulizwa na pia alibainisha kuwa anatamani siku moja tanzanie kusiwe na tatizo la ajira
Wauzuriaji wakifwatilia kiumakini FORUM inavyo endelea sio kitu cha kutamani kukosa akikisha next time,mwezi wa pili 2014 nafika enderea kufwatilia www.onaviews.blogspot.com itakujulisha ni tarehe ngapi.
Baada ya FORUM kumalizika watu wakiji patia chakula Forum hii ilifanyika ukumbi wa           makumbusho ya taifa jana jioni ni bure,kwa maana ulipii chochote na unapata elimu safi na kutengeneza networking na watu mbalimbali karibu.






RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI WA OFISI YA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS

 

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akizungumza na Uongozi wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais,katika kikao cha kujadili utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo,wa mwaka wa fedha 2013-2014 na robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2013-2014,katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar,(kulia) Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad,(kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza  wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji,(kusho) na Katibu Mkuu  Kiongozi DSk.Abdulhamid Yahaya Mzee.
Baadhi ya Viongozi mbali mbali wa Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais,wakiwa katika cha  kujadili utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo,wa mwaka wa fedha 2013-2014 na robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2013-2014,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,(hayupo pichani) katika Ukumbi wa Mikutano Ikulu Mjini Zanzibar jana.

Alhamisi, 28 Novemba 2013

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA SHEREHE ZA MAADHIMISHO MIAKA 10 YA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA (TCRA), DAR ES SALAAM.

 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hituba yake ya uzinduzi rasmi wa sherehe za maadhimisho ya miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Miaka 10 ya Mapinduzi katika Sekta ya Mawasiliano Tanzania, yaliyozinduliwa rasmi leo katika Ukumbi wa Mliman City,jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Prof. John Nkoma, wakati alipotembelea katika chumba cha Mtambo wa Kufuatilia Mawasiliano ya Simu (Telecommunicatins Traffic Monitoring System) baada ya kufungua rasmi Sherehe za uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi msaidizi Chumba cha Mtambo wa Kufuatilia Mawasiliano ya Simu (Telecommunicatins Traffic Monitoring System) Sunday Richard, wakati alipotembelea chumba hicho baada ya kufungua rasmi Sherehe za uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa (wa pili kulia) ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Prof. John Nkoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (katikati) akizungumza na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), Prof. John Nkoma (kulia) na Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia, Prof.Makame Mbarawa, nje ya Jengo la Mawasiliano baada ya kutembelea Chumba cha Mtambo wa Kufuatilia Mawasiliano ya Simu (Telecommunicatins Traffic Monitoring System) baada ya kufungua rasmi Sherehe za uzinduzi wa Maadhimisho ya Miaka 10 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo katika ukumbi wa Mliman City jijini Dar es Salaam..

Jumanne, 26 Novemba 2013

Kwa wale wapenzi wa ndondi dunia yasubiri Pacquiao V/s Floyd Mayweather pata habari na picha.

Manny Pacquiao sasa yupo tayari kupigana na Floyd Mayweather lakini anasema ni juu ya bondia huyo wa Marekani kuamua lini anataka pambano hilo.

Pacquiao, kutokea Philippines,hapo jana amepata ushindi wake wa kwanza baada ya miaka miwili  baada ya kumshinda Brandon Rios na kunyakuwa taji la WBO uzito wa welter.

Anasema kazi yake ni kupigana kwahiyo yupo tayari kupigana na Mayweather.


Mapambano 10 yaliyopita ya Manny Pacquiao

  • 23 Nov, 2013: v Brandon Rios (US), won (pts)
  • 8 Dec, 2012: v Juan Manuel Marquez (Mex), lost (KO 6th)
  • 9 Jun, 2012: v Timothy Bradley (US), lost (pts)
  • 12 Nov, 2011: v Juan Manuel Marquez (Mex), won (pts)
  • 7 May, 2011: v Shane Mosley (US), won (pts)
  • 13 Nov, 2010: v Antonio Margarito (Mex), won (pts)
  • 13 Mar, 2010: Joshua Clottey (Gha), won (pts)
  • 14 Nov, 2009: v Miguel Cotto (Pue), won (stoppage, 12th)
  • 2 May, 2009: v Ricky Hatton (GB), won (KO, 2nd)
  • 6 Dec, 2008: v Oscar de la Hoya (US), won (retired, 8th)

JIJINI MBEYA PICHA : UZINDUZI WA MAONESHO YA KIMATAIFA YA BIASHARA MKOANI MBEYA MAPOKEZI YA MGENI RASMI WAZIRI WA UCHUKUZI DR. MWAKYEMBE

 Mgeni Rasmi Waziri wa Uchukuzi Dr. Mwakyembe  akisalimiana na Mkurugenzi wa NMB Kanda za nyanda za juu kusuni Mama Makirie

 

 Mgeni Rasmi Waziri wa Uchukuzi Dr. Mwakyembe  akiendelea kusalimiana na wadau mbalimbali 




Wadau mbalimbali wakiwa wanampokea Mgeni Rasmi Waziri wa Uchukuzi Dr. Mwakyembe
 DR.  Mwakalukwa akiwa anazungumza jambo wakati wa kumpokea Mgeni Rasmi Waziri wa Uchukuzi Dr. Mwakyembe
 Meza kuu ikiwa imeongozwa na Mgeni Rasmi Waziri wa Uchukuzi Dr. Mwakyembe

MALIKIA WA NYUKI AJITOA SIMBA,MAJUNGU NA MIGOGORO YACHANGIA.

MALKIA wa Nyuki ameandika barua ya kujiondoa kwenye Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Simba kutokana na kuchukizwa na migogoro.
 
Malkia ambaye jina lake halisi ni Rahma Al Kharusi, amethibitisha hilo na kusema aliamua kufanya hivyo kutokana na kukerwa na migogoro ndani ya kamati hiyo.
Akizungumza jana kutoka Oman, Malkia wa Nyuki alisema aliamua kujiondoa kwa mambo mawili makubwa ambayo ni migogoro na kukosa nafasi.
 
“Baada ya kumueleza Rage kwamba nimefikia uamuzi huo, ameniomba nibaki kwa kuwa ninahitajika Simba. Kanishauri kwamba niingie katika upande wa baraza la wadhamini. Kwangu naona si mbaya, maana sitakuwa na vikao vya mara kwa mara, lakini bado nasisitiza migogoro si sahihi,” alisema.
 
 “Kwani kama si kuteuliwa katika nafasi hii ya kusimamia mali za Simba, basi nilikuwa nimeshajiondoa kabisa Simba hadi hapo hali itulie maana sioni faida ya haya yaliyopo sasa.”
Malkia wa Nyuki, ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa mjumbe wa Bodi ya Udhamini ya Simba, ndiye alitoa zaidi ya Sh milioni 80, Simba ikaweka kambi ya siku 15 jijini Muscat nchini Oman.
 
Lakini aliahidi kuanza kushughulikia kujenga uwanja kwa ajili ya mazoezi, pia alifunga safari kwenda kufanya mazungumzo na Sunderland kuisaidia Simba, lakini amekuwa akilalama kwamba migogoro na utendaji mbovu ni tatizo.
 
Katika mkutano wa jana jijini Dar, Rage alitangaza kumteua Malkia katika nafasi hiyo na nafasi yake katika kamati ya utendaji akamteua Michael Richard Wambura aliyewahi kuwa katibu mkuu Simba.

WATANZANIA WAOMBWA KUMPIGIA KURA HISIA(TUSKER 12)TUSKER PROJECT FAME


Mshiriki pekee aliyebaki katika mashindano ya kusaka vipaji Afrika Mashariki kutoka Tanzania Elisha Maghiya(Hisia) akiwa katika jukwaa la Tusker Project Fame msimu wa sita nchini Kenya.  
Tuma neno TUSKER 12 kwenda namba 15324 na pia kupiga kura kupitia www.tusker.mob

Jumatatu, 25 Novemba 2013

Mh. Lowassa aongoza harambee ya Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Saranga,Kimara jijini Dar


 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiburudika kwa kucheza muziki sambamba na wakina Mama wakazi wa Kata ya Saranga,Kimara jijini Dar es Salaam,Mwishoni mwa wiki wakati alipokwenda kuendesha harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya pili ya Sekondari katika Kata hiyo.Zaidi ya Sh. Mil. 100 ziliweza kupatikana kwenye harambee hiyo.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akipena mikono na Wakazi mbali mbali wa Kata ya Saranga,Kimara wakati akiendesha harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya pili ya Sekondari katika Kata hiyo,iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisisitija jambo kwa wananchi wakazi wa Kata ya Saranga,Kimara jijini Dar es Salaam wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya pili ya Sekondari katika Kata hiyo,iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
 Diwani wa Kata ya Saranga (CHADEMA),Mh. Ephraim Kinyafu akizungumza machache wakati wa harambee hilo,iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Kata ya Saranga,Kimara jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe wa NEC (CCM) Wilaya ya Kinondoni,Kalist Lyimo akisisiza jambo kwa wakazi wa Saranga,Juu ya umuhimu wa kuchangia harambee hiyo.

LADY JAYDEE NA MH.JANUARY MAKAMBA.


Lady Jaydee

                                                     MH. January Makamba

PATA PICHA YA JEZI MPYA ZA BRAZIL...NA SCOLARI ASEMA PIGA UA KOMBE LITABAKI COPACABANA

KOCHA Luiz Felipe Scolari amezindua jezi mpya za Brazil zenye nembo ya Nike na amesema wenyeji wapo tayari kuipa nchi taji la sita la Kombe la Dunia mwakani. 
Nyota wa Barcelona na Brazil, Neymar ametokea kwenye picha ya bango la tangazo la jezi hizo mpya, pamoja na kiungo wa Wolfsburg, Luiz Gustavo wote walikuwa Copacabana wamevaa jezi maarufu ya njano. 
Na kocha Scolari amewaonya wapinzani wa Brazil kwamba mabingwa hao mara tano wanataka kufanya kweli sasa kushinda taji la sita na kuweka rekodi mpya.
Inaonekana imechangamka: Neymar akiwa na David Luiz (katikati kulia) na Thiago Silva (katikati kushoto)
"Jezi zina mwonekano mzuri, kitu pekee kinachokosekana ni nyota sita," alisema Scolari. "Tumedhamiria kuwa nayo hapo baada ya Kombe la Dunia,".
Uzinduzi wa nembo ya 2014 ni mwanzo wa kampeni za Nike. ambao jezi ya Brazil ndiyo huwapatia mauzo makubwa kimataifa. 
Nike inatarajiwa Brazil kuwa bidhaa ya tatu kwa ukubwa duniani hadi kufika mwaka 2017, nyuma ya Marekani na China.
Wapinzani wa Nike katika utengenezaji wa vifaa vya michezo ni Adidas.
Dapper: The Nike kit comes in the classic yellow with green trim
Dapper: The Nike kit comes in the classic yellow with green trim
Dapper: The Nike kit comes in the classic yellow with green trim and five stars 
Time to shine? Luiz Felipe Scolari believes his Brazil team can win a sixth trophy on home soil
Time to shine? Luiz Felipe Scolari believes his Brazil team can win a sixth trophy on home soil
 
 
Blogger Templates