Social Icons

Jumanne, 29 Oktoba 2013

Angalia picha Watuhumiwa wa mauaji ya bilionea wa madini ya Tanzanite wa jijini Arusha wafikishwa mahakamani jana


Mshitakiwa, Sharif Mohamed Athuman (31), ambaye ni mshitakiwa namba

moja katika kesi ya Mauaji ya Bilionea wa Madini ya Tanzanite, Erasto
Msuya mchimbaji mdogo wa madini na mkazi wa Kimandolu mkoani Arusha, akitoka nje ya Mahakama ya Hakimu mkazi Moshi, muda mfupi baada ya kesi hiyo kuahirishwa hadi Desemba 11, mwaka huu.
Mshitakiwa namba mbili, Shaibu Jumanne Saidi maarufu kama Mredi (38),

anayetuhumiwa na wengine saba, kumuua Mfanyabiashara Erasto Msuya kwa kumpiga risasi akitoka kwa taabu nje ya mahakama ya Hakimu mkazi
Moshi, baada ya kesi hiyo kuahirishwa hadi Desemba 11, mwaka huu.
Mmoja wa Washtakiwa katika kesi ya Mauaji, anayetuhumiwa kushirikiana

na wenzake saba, kumuua Mfanyabiashara Erasto Msuya kwa kumpiga risasi akisindikizwa na Maaskari kutoka katika mahakama ya Hakimu mkazi Moshi, muda mfupi baada ya kesi hiyo jana kuahirishwa hadi Desemba 11, mwaka huu.
Washitakiwa Joseph Damian "Chusa" na mwenzake Shaibu Jumanne Saidi

"Mredi", wakimsaidia Mshitakiwa mwenzao kupanda katika Gari la Polisi
muda mfupi baada ya kesi inayowakabili ya mauaji ya Bilionea wa Madini
ya Tanzanite, Erasto Msuya kuahirishwa hadi Desemba 11, mwaka
huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates