Social Icons

Featured Posts

Alhamisi, 3 Desemba 2015

Kenya yapanda nafasi 27 katika orodha ya FIFA

Image copyright
Image captionKenya yapanda nafasi 27 katika orodha ya FIFA
Licha ya kuondolewa katika kinyang'anyiro cha kufuzu kwa kombe la dunia Harambee Stars ya Kenya imepanda nafasi 27 katika orodha ya hivi punde ya Shirikisho la soka duniani FIFA.
Kenya iliyokuwa imeorodheshwa katika nafasi ya 125 iliwashangaza wengi ilipoilaza Cape Verde bao 1-0 katika mkondo wa kwanza wa mchujo wa kuwania kombe la dunia.
Kufuatia ushindi huo Kenya ilijizolea alama 345 na sasa inaorodheshwa katika nafasi ya 25 barani Afrika na 98 duniani.
Timu hiyo hata hivyo ililazwa 2-0 katika mechi ya marudiano na ikabanduliwa nje ya mchujo huo wa kufuzu kwa mashindanoa hayo.
Kichapo hicho kilifuatia purukushani iliyosababisha timu hiyo kukosa usafiri kwa zaidi ya saa 12 wakiwa katika angatua ya Wilson mjini Nairobi.
Kenya ilifika Cape Verde saa mbili tu kabla ya kuanza kwa mechi hiyo ya marudio na hivyo haikuwa ajabu ilipolazwa 2-0.

Pistorius apatikana na hatia ya mauaji

Pistorius

Image copyright
Pistorius aliondoka gerezani Oktoba mwaka huu
Mahakama ya Juu nchini Afrika Kusini imempata mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius na hatia ya mauaji.
Mahakama hiyo imekubali rufaa iliwasilishwa na upande wa mashtaka ikitaka Pistorius apatikane na hatia ya mauaji, ambayo adhabu yake ni kali zaidi kuliko ya kuua bila kukusudia.
Jaji Lorimer Leach amesema mwanariadha huyo anafaa kurejeshwa kwa jaji aliyemhukumu ili apokee adhabu ya kosa la mauaji.
Pistorius alimuua mpenzi wake Reeva Steenkamp Februari 2013 baada ya kufyatua risasi kupitia mlango wa choo.
Image copyright
Image captionPistorius akiwa na Reeva ambaye alikuwa mwanamitindo
Amekuwa akitumikia kifungo cha nyumbani baada ya kukaa mwaka mmoja gerezani kwa kosa la kuua bila kukusudia.
Awali, ilikuwa imeripotiwa kimakosa kwamba rufaa hiyo ilikuwa imetupwa na angeendelea kutumia kifungo cha kuua bila kukusudia.
Pistorius alifungwa jela miaka mitano mwaka 2014 baada ya kupatikana na kosa hilo la kuua bila kukusudia.

TFF yasimamisha mchakato wa uchaguzi Simba.

 
 Shirikisho la soka tanzania TFF limesimamisha mara moja mchakato wa uchaguzi wa klabu ya Simba hadi hapo kamati ya utendaji ya Simba itakapo unda kamati ya maadali.

Akizungumza na waandishi wa habari rais wa TFF Jamal Malinzi amesema TFF imepokea malalamiko kadhaa juu ya ukiukwaji wa maadili wa wagombea na wanachama kadhaa wa klabu ya Simba.

Malinzi amesema kwa mujibu wa katiba ya Simba ibara ya 16 kifungu (e) na ibara ya 30 kifungu (h) kamati ya utendaji ya Simba imeagiza iunde kamati ya maadili mara moja  na kwamba kamati hiyo ya maadili ikae mara tu baada ya kuundwa na kusikiliza mashauri yote ya kimaadili ambayo kwa sasa yamewasilishwa TFF na walalamikaji kadhaa.

Aidha Malinzi amesema kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za TFF ibara ya 2 kifunga cha (4) kamati ya utendaji ya Simba itaendelea kuwa madarakani hadi hapo mchakato wa uchaguzi wa Simba.

Washukiwa wauawa baada ya mauaji Marekani

Polisi
Image copyright
Image captionWashukiwa hao wawili wameuawa kwenye ufyatulianaji wa risasi kati yao na polisi
Polisi katika jimbo la California wametaja majina ya washukiwa wawili ambao wameuawa na polisi baada ya watu 14 kuuawa kwa kupigwa risasi katika mji wa San Bernardino.
Mwanamume Syed Rizwan Farook, 28, na mwanamke Tashfeen Malik, 27, wameuawa kwenye ufyatulianaji wa risasi na polisi.
Farook alikuwa ameajiriwa na baraza la mji kwa miaka mitano, mkuu wa polisi wa San Bernardino Jarrod Burguan amesema.
Shambulio hilo lilitokea wakati wa hafla katika afisi moja Jumatano. Maelezo kuhusu waliofariki bado hayajatolewa.
Kisa hicho ndicho kibaya zaidi cha ufyatuaji wa risasi dhidi ya umma Marekani tangu watu 26 wauawe katika shule moja mjini Newtown, Connecticut mwaka 2012.
Bw Burguan, amesema watu 17 walijeruhiwa na kwamba polisi wana kila sababu ya kuamini kwamba wawili hao pekee ndio waliohusika kwenye shambulio hilo.
Shambulio lilo lilitekelezwa katika kituo cha Inland Regional Center ambacho huwasaidia walemavu na watu wenye matatizo ya kiakili. Hata hivyo, ufyauaji risasi huo hauonekani kuwa na uhusiano na wagonjwa hao.
Image copyrightAP
Image captionMmoja ya ndugu wa wafiwa akifarijiwa.
Limetokea siku chache tu baada ya watu watatu kuuawa katika kliniki ya Colorado Planned Parenthood.
Rais wa Marekani Barack Obama ameshutumu shambulio hilo.
“Jambo moja tunalojua ni kwamba visa hivi vya ufyatuaji wa risasi humu nchini haviwezi kulinganishwa na kwingine duniani.”
Mkurugenzi Msaidizi wa Shirika la kijasusi la FBI David Bowdich anasema sababu kubwa ya mauaji hadi sasa haijafahamika.
"Kwa wakati huu ninaelewa moja ya maswali yenu ni kuhusu tukio hili la kigaidi. Ninawaeleza sasa kuwa hatujui kama hili ni tukio la kigaidi kwa hiyo tunaanzia mwanzo kufanya kazi na wenzetu waliopo katika eneo hili. Tunadhani inaweza kuwa, pia inaweza isiwe lakini tunafanya kazi bega kwa bega nao kuanzia mwanzo. Kama mambo yatabadilika tupo hapa na hakuna hatua yoyote itakayopotea wakati uchunguzi utakapokuwa unaendelea."

MCHAMBUZI MAHILI ACHAMBUA KWA NINI MAN U HAIPATI MABAO(MAGORI).

Klabu ya Manchester United imekuwa ikishindwa kufunga magoli ya kutosha kwenye michezo yke mbalimbali hali iyozua taharuki kwa mashabiki, wachezaji wa zamani na hata wachambuzi mbalimbali wa masuala ya yoka duniani wamekuwa wakikosa hali hiyo.
Mambo yameenda mbali zaidi hadi kufikia kukosoa mbinu na mfumo wa kocha mkuu wa klabu hiyo Lois Van Gaal wakidai haziendani au hazifit kwenye klabu ya United kwasababu mbinu hizo zimeshindwa kuzaa matunda kwenye kikosi hicho cha Old Trafford.
United ipo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa gili ikiwa na pointi 28 pointi moja nyuma ya vinara wa ligi hiyo Man City pamoja na Leicester City walio nafasi ya pili wakilingana kwa pointi na Man City lakini wakitofautiana wastani wa magoli ya kufungwa na kufunga.
Kikiwa kimecheza michezo 14 ya EPL, kikosi cha United kimefunga magoli 20 magoli 10 nyuma ya Man City na magoli tisa nyuma ya Leicester City.
Mchambuzi wa michezo hususan soka Shaffih Dauda yeye amefanya uchambuzi na kubaini ni kwanini timu ya Manchester United inashindwa kupata magoli mengi, ungana naye kwenye uchambuzi huu ili uelewe yeye mtazamo wake ni upi, je unaendana na wa kwako au mko njia mbili tofauti? Huyu hapa Dauda…
Kwanza kabisa mimi ambacho naweza kukizungumzia kutokana na namna ambavyo naifahamu klabu ya Manchester United katika kipindi cha miaka ya karibuni baada ya watu wengi kuanza kuifaatilia. Mimi nakumbuka kwenye miaka ya tisini (1990s) wakati yupo Eric Kantona, Mark Hughes Brian McClair walivyotoka hao wakaja akina Teddy Sheringham, Dwight Yorke Andy Cole, Ole Gunnar Solskjæ walikuwepo washambuliaji wengi sana.
United imekuwa na washambuliaji wengi sana hata kwenye zama za kina Ruud van Nisterlrooy, wanakuja akina Luis Saha, Cristiano Ronaldo, Carlos Tevez , Dimitar Berbatov. United ni klabu ambayo kwa kipindi cha muda mrefu imekuwa na hazina ya washambuliaji kitu ambacho kimekuwa ni utamaduni wa timu.
Wakati mwingine ilikuwa inawasaidia wao kwa wao kuweza kutengeneza ari ya ushindani kugombania namba na vitu kama hivyo. Kwa wenzetu hiyo ilikuwa ni changamoto chanya timu kuwa na wachezaji wengi kwenye nafasi moja tofauti na Bongo ambapo wakiwepo washambuliaji wanne wenye uwezo mkubwa wanaanza kupigana ‘misumari’ si dhani kama wenzetu wanafanya hivyo, Ulaya ni mtu kupambana kupata nafasi.
Ukirudi leo Manchester United, ina straiker gani ambao tunawazungumzia kwamba hawafungi? Wana mwangalia Wayne Rooney, lakini Rooney amebaki yeye kubebeshwa mzigo mkubwa, Antony Martial ni mchezaji mpya ambaye bado anahitaji muda wa kuzoea. Mchezaji mwngine mbaye yupo ni Memphis Depay naye yupo kwenye msimu wake wa kwanza hata nusu haujafika, nani mshambuliaji mwingine kwenye kikosi cha United? Ni Wayne Rooney tu, amekuja Jese Lingard ambaye wakati mwingine anatumika kama striker kipindi ambacho timu haina washambuliaji.
Kwahiyo mimi kiwepesi kabisa nasema Manchester United haifungi kwasababu haina washambuliaji na wakati Rooney anafunga magoli mengi alikuweo Ronaldo, Tevez Berbatov, hebu niambie Rooney anafanyaje kwa kiwango alichonacho Bebertov akigeuka huku kuna Tevez anapasha pembeni kuna Cristiano Ronaldo ananjaa, na yeye lazima ajitume uwanjani.
Lakini leo yeye ndiyo Captain nani anayempa changamoto kwenye kikosi cha United? Hiyo ilikuwa najaribu kuangalia tu kwa ujumla wake.
Ukirudi kwenye mambo ya mfumo ambayo watu wengi wamekuwa wakimshutumu Louis van Gaal kwamba mbinu zake haziwatengenezei mazingira rafiki washambuliaji wa Manchester United, unarudi palepale washambuliaji wapi? Hamna washambuliaji Manchester United.
Ukisema mbinu za Van Gaal ni mbaya kumbuka kocha huyu amefanya vizuri akiwa na vilabu vingi yeye hajifunzi pale United historia inambeba, amekuwa kocha wa Bayern Munich ikiwa na washambuliaji kama Mario Gomes na Luca Toni walikuwa wanafunga, na wale washambuliaji ni aina ya washambuliaji wasio na mambo mengi uwanjani lakini kwasababu kuna watu walikuwa wanatengezeneza nafasi wao wakawa wanaweka kambani.
Mpaka Luca Toni akaamua kundoka Bayern kutokana na competition ya namba kati yake na Gomes.
Lakini wakati Van Gaal yupo Ajax alikuwa na Patric Kluivert  akiwa anachipukia, Nwanko Kanu lakini akaenda Barcelona akakutana na na washambuliaji wengi na wote walikuwa wanafunga. Kwahiyo mimi nadha United inamatatizo kwenye kikosi kwenye idara ya ushambuliaji kwa kutokuwepo washambuliaji wa kutosha ambapo automatically wangeweza kutengeneza upinzani ndani yao.
Kwa hadhi ya klabu kama ya Manchester United ilitakiwa kuwa na washambuliaji kuanzi watatu hadi wanne wa kiwango cha dunia, lakini leo hii kuna straiker gani pale? Baada ya kuondoka kwa Falcao ambaye hakutengenezewa mazingira ya kuaminika akaonekana kama bidhaa ya ziada akashindwa ku-perfom lakini siamini kwamba Falcao sio mshambuliaji mzuri.

BAADA YA AGIZO LA ELIMU BURE, ADA ELEKEZI KWA SHULE BINAFSI KUJULIKANA DEC 15

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imewataka wazazi na walezi wenye wanafunzi wanaotegemea kuanza masomo au kuendelea na masomo katika shule binafsi mapema Januari mwezi ujao, kuvuta subira hadi Desemba 15, mwaka huu serikali itakapotoa maelekezo mbalimbali ikiwemo suala la ada elekezi.

Akizungumzia hatua zinazofanywa hivi sasa na serikali kuhusu ada elekezi kwa shule binafsi, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome, alisema timu mbili hivi sasa zinafanya kazi ya uchambuzi wa michanganuo ya ada kwenye shule hizo, na baada ya muda mfupi uamuzi utatolewa.

“Hili sasa tumeliundia timu mbili za kufanya uchambuzi wa masuala ya ada katika shule za msingi na sekondari binafsi, ili kuwa na ada ekelezi kwenye utozaji wa ada kuanzia Januari mwakani,” alisema Profesa Mchome.

Aidha, alisisitiza kuwa katika mchakato huo, na kwa muda uliopo hivi sasa hadi Januari ni kipindi kifupi, hivyo inawezekana ada elekezi zikaanza kutumika kwa baadhi ya shule za msingi binafsi, kama eneo la majaribio.

Aliongeza kuwa Tanzania ina shule za msingi 17,000, zikiwamo za binafsi karibu 1,000 na zile za serikali 16,000 na kwamba iwapo wataanza na ada elekezi kwa shule hizo binafsi, wanaweza kuona utekelezaji wake.

Kwa upande wa shule za sekondari, Profesa Mchome alisema ziko zaidi ya shule 4,700 na kati ya hizo shule binafsi ni karibu 1,400 huku za serikali zikiwa 3,300 na kwamba mchakato wa ada elekezi kwa shule hizo binafsi unaendelea pia.

“Timu yetu inaendelea kufanya kazi kwenye mchakato katika shule za sekondari binafsi, zina wadau wengi kwa vile ni nyingi pia, hivyo hatuwezi kutoa maekelezo ya harakaharaka bila kuangalia utekelezaji wake kwa kina,” alifafanua Katibu Mkuu.

Alisisitiza kuwa kwa kuanzia, serikali ilifuta michango yote kwa shule zote nchini na kwamba hatua hiyo inazihusu pia shule binafsi na kuzitaka kutotumia ujanja wa kuingiza michango hiyo kwenye ada kwa madai ya kupandisha ada kwa mwaka ujao wa masomo.


Ukweli kuhusu malezi



1. Malezi ni jukumu zito na linalohitaji kujitoa kwa hali ya juu sana, (labda tofauti na majukumu mengine mengi) bahati mbaya wazazi wengi hawayajui mapana na marefu ya jukumu hili. Kuzaa ni kazi ambayo wengi twaijua na twaiweza lakini malezi ni wachache wetu tunayajua, na wapo wengine hudhani wanajua kwa vile wanavyolea watoto wao kumbe wanachofanya sicho.

2. Kuwa mlezi inaenda mbali zaidi ya uwezo wako wa via vyako vya uzazi kuweza kutengeneza kiumbe kinachoitwa mtoto.
3. Matatizo mengi leo tunayokutana nayo katika mahusiano yetu, ndoa zetu, familia zetu na jamii zetu nikutokana na malezi mabovu wakati wa utoto. Wengi wetu tumekosa mapenzi ya wazazi wote au mzazi mmoja, tumekosa usalama na hali ya kujihisi kutosheka tukiwa na wazazi wetu, hali hizi zote huweza kuleta matokeo mabaya wakati wa makuzi yetu na hata tunapokuwa katika mahusiano yetu.
4. Kuwa mzazi au mlezi bora haimaanishi uwezo wa kuwapa watoto wako kila wanachohitaji na mara wanapokihitaji (hili ni wazo potofu). Haimaanishi kuhakikisha nyumbani kuna kilakitu wanachokifurahia watoto wakati wewe haupo kwa ajili yao, bali uwezo wa kuwepo nao, kuwajua na kuwafahamu vema hisia zao na kuwezakuingia katika maisha yao kila mara. Ni uwezo wakuwafanya watoto wako wafahamu kwamba sio tu kwamba unawapa vitu bali unajitoa kwa ajili yao ili tu kwamba wao na wewe mfurahi.
5. Wakati wote wazazi ndio vioo au mifano ya kuigwa (models) kwa watoto wao. Wengi wetu tumeharibika sio kwa jinsi ulimwengu ulivyotuathiri bali kwa jinsi ambavyo tulijifunza toka kwa walezi wetu. Baadhi ya misimamo yao na imani zao na namna ya utendaji wa mambo vimetuathiri vibaya katika maisha yetu leo. Kama mzazi jiulize leo wewe kama kioo unaakisi nini katika maisha ya watoto wako? Je wanachojifunza toka kwako au kwenu leo kitawafanya kujisifia au kuona aibu hapo baadae?
Mambo ya kuzingatia ili kumlea mtoto akue akiwa mwenye furaha
1. Mpe mototo wako muda na uhuru wa kucheza
Usipende kumpa mtoto wako ratiba ngumu iliyo jaa shuhuli za kufanya na majukumu ya kumfanya awebize wakati wote ukidhani ndo jinsi bora ya kumlea mtoto anayewajibika, Hapana!! Mtoto anayepewa ratiba chache na inayoruhusu muda wa uhuru binafsi huweza kuonyesha vitu anavyovipendelea na vile asivyovipenda, wazazi wengi hupata ugumu kujua vipaji vya watoto wao kwasababu ratiba zao kuanzia wakitoka shule zimejaa vitu ambavyo wazazi wamewapangia sio vitu ambavyo watoto wanavibuni wenyewe huku wakipewa msaada pale wanapohitaji. Sio kitu chema wazazi kulaazimisha watoto wao kufanya au kujua vile vitu ambavyo vi vipaji vya wazazi, kama mtoto atajua mwenyewe na kutamani basi haina shida lakini sio kulazimishwa au kushawishiwa.

2. Jali sana usingizi, mazoezi na chakula
Wakati wote wazazitukumbuke kuwa watoto wanapo lala ndio mchakato wa makuzi bora kiakili, kihisia na kimwili unapofanyika. Watoto pia wanatakiwa kufundishwa kutoona mazoezi kama jambo la anasa, hamu na kupenda kushiriki mazoezi ya viungo kuwe kitu cha kawaida kwao, hii itawasaidia sana katika makuzi ya kimwili na kuwaepusha na magonjwa yasiyoyalazima. Mazoezi huwapa ujasiri watoto wakiwa bado wadogo, kwahiyo kama mzazi unapenda kufanya mazoezi basi penda kumshirikisha mwanao hatakama sio kushiriki kiutendaji basi hata kuangalia na kumuelewesha kinachojiri. Kumbuka kumruhusu mtoto kuwa na muda wa kucheza kwasababu katika kucheza ndiko mazoezi ya viungo kwa watoto hufanyika. Hapa nazungumzia kucheza na sio kucheza kucheza.
3. Usiyachukue matatizo yao
Baadhi ya wazazi hupenda kuwasaidia watoto wao katika kilakitu, hata katika vile ambavyo watoto hao wangeweza kuvifanya wenyewe. Hata kama maranyingine inaonekana ni kitu kigumu basi waache wajaribu kwanza kwa njia zao wakipata shida taratibu watajifunza kuomba msaada (huku nako ni kujifunza), maranyingine utashangaa wanabuni njia ta kutatua tatizo hilo wao wenyewe na jambo linafanikiwa, mbinu hizi ni vema zianze watoto wakiwa wadogo kwasababu zinawasaidia sana hata katika maisha yao ya baadae. Pale unapokutana na watu wazima ambao hawawezi kuvumilia mara wanapokutana na matatizo madogo tu ujue hawakufunzwa jinsi ya kukabiliana na matatizo yao wenyewe, walitegemea msaada hata katika kitu kidogo. Kumbuka kuwa uwezo wa kuyashuhulikia matatizo na kuyatatua huanza tukiwa bado wadogo.
Jifunze kuziangalia changamoto za mtoto wako kama zawadi itakayomfanya ajifunze zaidi mbinu na ujuzi mpya. Changamoto hizi zitamfundisha kuwa mvumilivu na mstahimilivu. Zinamfundisha pia jinsi ya kuchukuliana na mazingira.

4. Check in “Jifunze kuingia kwenye maisha yao mara kwa mara”
Kama mzazi jifunze na jitahidi kuingia mara kwa mara kwenye maisha ya watoto wako. Usiwe mbali nao kihisia, lugha yako iwe inayoruhusu wao kujiachia kwako katika yote yanayowahusu. Tafuta sana kujua toka kwao, kwa mfano; uliza, “naonakama una huzuni leo vipi?” “hembu niambie shule yako ya jumapili ilikuwaje, ,lifundishwa nini?” Ikiwa atakukataa au kutokukubali katika jitiada zako zakuingia katika maisha yake basi jaribu tena baadae, usichoke haraka kumweka karibu.
5. Ruhusu hisia zao
Sio tu kwamba tunataka watoto wetu wawe na furaha bali pia tunatamani wafanye mambo kwa furaha pia, inasikitisha sana kuona mtoto wako analia na kugaragara sehemu wakati wenzake wote wana furaha, sasa famu kwamba suala hapa sio kumwambia acheke bali ni kushuhulikia kile kinachomfanya asionyeshe furaha. Mfundishe mtoto wako kuzigundua hisia zake na kuzielezea kwa maneno, kwa mfano; “Sijafurahi kwa sababu sijabembea mara ya pili kama wenzangu”. Mfundishe mtoto wako kufahamu kuwa ni sawa na nihaki yake kukasirika na sio dhambi wala kosa kwahiyo asiogope mradi tu hasira hizo ziwe zina maelezo bayana na yenye mantiki. Mtoto anapoweza kuzishuhulikia hisia ngumu itamsaidia kuwa na furaha ya kudumu katika maisha yake.


Kuumwa kwa kichwa wakati wa ujauzito


Wanawake wengi hupata tatizo la kuumwa kwa kichwa wakati wa ujauzito. Hili tatizo huweza kutokea wakati wowote wa ujauzito lakini mara nyingi hutokea wakati wa trimester ya kwanza (miezi mitatu ya kwanza) na trimester ya tatu (miezi mitatu ya mwisho) ya ujauzito.


Katika trimester ya kwanza kuumwa kwa kichwa mara nyingi husabababishwa na kuongezeka kwa hormone na damu inayosukumwa mwilini.

Kuumwa kwa kichwa kunaweza kuongezeka zaidi pale mwanamke mjamzito akiwa na stress, kukosekana kwa usingiziuchovu, mafua, kuwa na low blood sugar(sukari isiyotosha kwenye damu), ukosekanaji wa maji ya kutosha mwilini(dehydration),  kwa wale waliozoea kunywa kahawa kuacha kunywa kahawa kunaweza kusababisha kuumwa kwa kichwa.

Kuumwa kwa kichwa wakati wa trimester ya mwisho husababishwa na kuongezeka kwa uzito unaoweka stress kwenye mwili, mwili kutokuwa balanced, pamoja na wanawake wengine kuwa na high blood pressure wakati wa ujauzito(preeclampsia).

Mara nyingi mama mjamzito hashauriwi kunywa dawa zozote zile kwa kipindi hiki kwasababu kuna uwezekano wa dawa kupokelewa na mtoto na kumdhuru kwa namna moja au nyingine. Hii ni sababu maalaamu kujaribu kutumia njia natural kupunguza maumivu yoyote yale mama anayopatwa nayo kwa kipindi hiki.

Jinsi ya kupunguza au kuondoa maumivu ya kichwa wakati wa ujauzito.

Jaribu kutuliza misuli ya uso na kupumzika.

Uwe makini na madawa ya aspirin na jamii za dawa hii, kwa vile dawa yoyote uinywao inaweza kumuaffect mtoto.

Ukisikia maumivu jaribu kunywa maji glass 2 - 3, kwasababu wakati mwingine maumivu husababishwa na kukosa maji ya kutosha mwilini.

Fanya zoezi la kutembea halafu kunywa maji mengi ya kutosha.

Chunguza vyakula unavyokula unaweza ukawa unapata reaction.

Pumzika vya kutosha na kupata mazoezi ya relaxation.

Fanya mazoezi mara kwa mara kama unavyotakiwa kwa mama mjamzito.

Kula chakula chenye afya kwa mama mjamzito.

Unaweza kuweka kitambaa cha moto kwenye eneo la macho, pua na kichwa kama kuuma kwa kichwa kunasababishwa na mafua au weka kitambaa cha baridi kwenye sehemu inayouma kama ni maumivu ya kichwa ya kawaida.

Hakikisha unabalance kiasi cha sukari kwenye damu(blood sugar)yako kwa kula kiasi kidogo cha chakula kila baada ya muda mfupi badala ya kusubiri kwa muda mrefu halafu kula mlo mkubwa.

Ukipata massage ya shingo, mabega na uti wa mgongo itapunguza stress na kupunguza maumivu ya kichwa.

Pumzika kwenye chumba chenye giza halafu jaribu kuvuta pumzi na kuachia ili kuondoa stress mwilini.

Oga maji ya moto au baridi.

Baadhi ya vyakula vinaweza kuchangia kuumwa kwa kichwa. Unaweza kujaribu kuvitoa kwenye diet yako kuona kama vitasababisha kupunguza maumivu ya kichwa.

Hivi vyakula ni pamoja na:


Chocolate
Vinywaji vikali
Mtindi, jibini, sour cream
Karanga
Mikate yenye yeast
Nyama zilizowekwa kemikali ili kuzisaidia kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika.(processed milk)

Ongea na daktari kama umejaribu vitu hivi na bado maumivu yapo au yanazidi au kuumwa kwa kichwa kunaambatana na kizungu zungu, kuvimba kwa mwili, maumivu kwenye maeneo ya juu ya tumbo au
kuongezeka kwa uzito ghafla.

Jumatano, 2 Desemba 2015

Mwingereza Jermaine Grant afungwa jela Kenya


Image captionJermaine alikamatwa mjini Mombasa 2011
Mwanamume mmoja raia wa Uingereza, anayetuhumiwa kupanga mashambulio ya kigaidi, amefungwa jela miaka tisa na mahakama mjini Mombasa.
Jermaine Grant, anayetoka London, amefungwa jela kwa makosa tisa yanayohusiana na kujaribu kujipatia uraia wa Kenya kwa njia haramu.
Bado anakabiliwa na mashtaka ya "kupanga kuunda vilipuzi” kwenye kesi ambayo bado inaendelea mjini Mombasa. Grant amekanusha mashtaka hayo.
Mwingereza huyo alikamatwa 2011, pale betri na kemikali vilipopatikana nyumbani kwake Mombasa.
Polisi nchini Uingereza, ambao wamewasaidia maafisa wa Kenya katika uchunguzi, wanadai vifaa hivyo vilikuwa vya kutumiwa kuunda vilipuzi.
Samantha Lewthwaite, ajulikanaye sana kama "White Widow," (Mtawa Mweupe), ambaye anasakwa kuhusiana na mashambulio ya 7/7 nchini Uingereza pia anadaiwa kuhusika katika njama hiyo.
Hukumu dhidi ya Grant imetolewa baada yake awali kuondolewa mashtaka hayo tisa yaliyohusiana na kujaribu kujipatia uraia wa Kenya kinyume cha sheria mapema mwaka huu.
Hata hivyo, Jaji wa Mahakama Kuu ya Mombasa, alibatilisha uamuzi huo na akamhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kila kosa.

Uingereza kuamua kushiriki mapambano dhidi ya IS

Bunge la Uingereza hii leo linatarajia kupiga kura kuiruhusu nchi yao kujiunga na mapambano dhidi ya kundi la dola la kiisilamu la IS nchini Syria.

Russland Syrien Militärhilfe
Waziri mkuu wa Uingereza , David Cameron ambaye ari yake ya kuliangamiza kundi hilo la dola la kiisilamu imeongezeka zaidi hasa baada ya mashambulizi ya mjini Paris anatarajiwa kuongoza mjadala bungeni unaotarajiwa kuchukua zaidi ya saa kumi katika kuelekea upigaji kura huo.
Mawaziri nchi humo wanaimani kwamba wabunge watapiga kura ya ndiyo kuunga mkono hatua hiyo hali ambayo inaashiria kuwa ndege za kijeshi za Uingereza zitaanza mashambulizi kulilenga kundi hilo la dola la kiisilamu huko nchini Syria kabla ya kufikia mwisho wa juma hili.
Cameron amesisitiza ya kuwa hatua za kijeshi zinahitajika sasa ili kuzuia mashambulizi kama yale ya yaliyoua watu 130 mjini Paris mwezi uliopita, lakini pia akiongeza kuwa hatua hiyo itaenda sambamba na juhudi za kidiplomasia zinazoendelea sasa katika kushughulkikia mgogoro wa Syria.
" Nitajitahidi kujenga hoja na nina imani kuwa wabunge wengi kutoka katika vyama vyote wataniunga mkono " alisema waziri mkuu Cameron katika kuelekea kura hiyo:

Hata hivyo baadhi ya wataalamu wa masuala ya kisiasa na ya kivita, wanasema wabunge kadhaa na raia wa kawaida wanaonekana kuwa na mashaka. Makundi ya watu wanaopinga mambo yanayohusiana vita tayari wameandamana kuonyesha kutounga mkono hatua hiyo.

Baadhi ya wachambuzi wanauona hatua hii ya uingereza kutaka kushirika katika kampeni dhidi ya kundi hilo la dola la kiisilamu kama hatua moja wapo ya kuwaunga mkono bega kwa bega washirika wake ambao ni mataifa ya Marekani na Ufaransa.
Syrien Syrische Armee
Jeshi la Syria
" Cameron kwa sasa anaona ni lazima aiunge mkono Ufaransa katika kipindi hiki inachokabiliana na tatazo la ugaidi " alisema Ben Berry ambaye ni mmoja wa washauri katika siasa za kimataifa.
Tayari Uingereza imekuwa ikishiriki katika mashambulizi ya anga dhidi ya kundi la dola la kiisilamu nchini Iraq kampeni ambayo ilianza tangu mwaka jana.
Aidha inaarifiwa pia kuwa Uingereza imeombwa nawashirika wake yakiwemo mataifa ya Ufaransa na Marekani kujiunga kikamlifu katika kampeni hiyo ya mashambulizi dhidi ya kundi hilo la dola la kiisilamu.
Tayari kumekuwepo na maandamanao nchini humo kupinga hatua ya kivita dhidi ya kundi hilo la dola la kiisilamu kama anavyosema mmmoja wa watu walioshiriki katika maandamano hayo
Chama cha Labour chagawanyika kuhusiana na hatua
Hatua hii ya Cameron inakuja mnamo wakati chama kikuu cha upinzani cha Labour nchini humo kikiwapa uhuru wa kuamua wabunge wa chama hicho katika kuunga mkono au kutounga mkono uamuzi huo pasipo shinikizo lolote kutokana na msimamo wa kiongozi mkuu wa chama cha Labor Jeremy Corbyn anayeonekana kupinga hatua hiyo .
" Tunataka kuwaua watu nchini mwao kwa kutumia mabomu yetu , tafadhali pigeni kura ya kutounga mkono hatua hii ya serikali dhidi ya mashambulizi ya nchini Syria" alisema kiongozi huyo wa chama cha Labor
Hata hivyo hatua hii ya kutopata shinikizo kutoka katika chama chao inaonyesha kuwa wabunge wa chama cha Labour ambao wanataka hatua za kijeshi zichukuliwe dhidi ya kundi hilo la dola la kiisilamu watapiga kura ya ndiyo hali ambayo inaonesha kuwa waziri mkuu Cameron atapata ushindi mkubwa katika azima yake hiyo.
 
 
Blogger Templates