Social Icons

Jumanne, 30 Juni 2015

Muda wayoyoma kwa Ugiriki kulipa deni

Alexis Tsipras Waziri Mkuu wa Ugiriki

Bw Tsipras amepinga vikali masharti ya wakopeshaji wa nchi yake
Waziri Mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras amewaomba wapiga kura kukataa masharti ya wakopeshaji wa nchi hiyo wakati wa kura ya maoni hapo Jumapili.
Bw Tsipras amesema kwa kupinga kubana matumizi, Ugiriki itaweza kushauriana zaidi na kupata suluhu la mozozo wa sasa wa kifedha.
Siku ya mwisho kwa Ugiriki kugharamia madeni yake ni Jumanne wiki hii ambapo inatakiwa kulipa deni la Euro bilioni 1.6, kwa shirika la fedha duniani{IMF}.
null
Viongozi wa Eu wameonya huenda Ugiriki ikaondoka kanda ya sarafu ya Euro
Viongozi wa Muungano wa Ulaya wameonya hatua ya kukataa kulipa madeni yake ni sawa na Ugiriki kujiondoa kutoka kanda inayotumia sarafu ya Euro.
Hata hivyo Waziri Mkuu Tsipras amesema hataki nchi yake kuitema Euro.Mazungumzo kati ya Ugiriki na wakopeshaji wake yalivunjika wiki jana, hatua iliyosababisha benki za nchi hiyo kufungwa.

MAGAZETI YA LEO

 
























Dalili za mwanamke anayetoka nje ya ndoa


         


Wataalamu wa maswala ya mahusiano wanaamini kwamba, mwanamke anapotoka nje ya ndoa yake, inakuwa rahisi sana kubainika au kufumaniwa kuliko ilivyo kwa mwanaume.

Hii inatokana na ukweli kwamba, hisia zinakuwa na nafasi kubwa sana kwa mwanamke, kwani mwanamke huishi kwa hisia zaidi kuliko mwanaume. Bado nasisitiza kwamba, haipaswi na siyo sahihi mtu kuchukulia dalili hizi kama ushahidi wa mpenzi wake kutoka nje ya ndoa. Uchunguzi wa kina kufuatia dalili hizi ni muhimu sana.

Zifuatazo hapa chini ni baadhi ya dalili zinazoweza kuonyeshwa na mwanamke ambaye anatoka au yupo kwenye harakati za kutoka nje ya ndoa yake:

1.KUCHELEWA: Kuna wakati mwanamke anaweza kuaga kwamba anakwenda saluni au kusuka, badala ya kurejea kwa muda ambao umezoeleka, anachukua muda mrefu hata mara tatu zaidi. kuna wakati kwenda sokoni huchukua saa kadhaa bila kujali soko liko umbali gani. Kama ni mara moja sawa, lakini ikishakuwa zaidi ya mara moja huenda kuna tatizo la kukosa uaminifu.

2.KUBADILI MAENEO: Hebu chukulia kwamba, mwanamke amezoea kwenda soko fulani la karibu, hospitali fulani ya karibu, saluni fulani ya karibu na hata nyumba fulani ya ibada ya karibu. Unapoona anahama maeneo ya karibu ya huduma na kwenda ya mbali, bila sababu ya msingi, huna budi kuanza kutuhumu mwenendo mbaya.

Siyo lazima kuhama kokote kuwe na mwenendo mbaya, lakini kama kuhama kwenyewe kunatia shaka kwa sababu maelezo ya kuhama huko hayana msingi, mwanaume ana kila sababu ya kuchunguza kama hakuna usaliti unao anywa.

3.UNUNUZI USIO WA KAWAIDA: Kama mwanamke anatoka nje ya ndoa yake kwa ajili ya kupata fedha, basi atakuwa na mabadiliko makubwa katika mtindo wake wa manunuzi.
Atakuwa ananunua vitu vya thamani kubwa kuliko uwezo wake, atakuwa na fedha nyingi tofauti na ambazo angekuwa nazo na pengine kumiliki mali kama nyumba kwa siri.

4.KUANZISHA VURUGU: Kuna wakati mwanamke anayetoka nje ya ndoa huanzisha vurugu za makusudi na mumewe. Lengo la kuanzisha vurugu hizo ni ili apate nafasi ya kujifanya amezira na kuondoka nyumbani kwa muda.

Huo muda anapoondoka nyumbani kujifanya kakerwa na vurugu hizo ndiyo muda ambao anautumia kwenda kwa hawara yake.

5.KUSITISHA UAMINIFU: Mwanamke anayetoka nje ya ndoa, mara nyingi husimamisha kumwamini mumewe, yaani hayuko tayari kushiriki masuala ya siri, ambayo wanandoa huwa wanashiriki.

Husita kumshirikisha mumewe kwenye mambo yake mengi. Lakini pia husita kumuomba mumewe ushauri, kama alivyokuwa akifanya siku za nyuma.

6.KUACHA KUVAA PETE: Kuna sababu nyingi ni kwa nini mwanamke anaweza kuacha kuvaa pete yake ya ndoa. Moja ya sababu hizo ni kusalitiwa na mumewe au ndoa yake kuwa kwenye misukosuko mikubwa sana.
Lakini nje ya misukosuko mikubwa ya ndoa, sababu nyingine inayoweza kumpelekea mwanamke kuvua mara kwa mara au moja kwa moja pete yake ya ndoa, ni kuwa na uhusiano nje ya ndoa yake.

7.KUONESHA WASIWASI: Kama mwanamke anatoka nje ya ndoa yake , ni lazima atakuwa na wasiwasi na mashaka yasiyo na sababu mbele ya mume wake.

Anaweza kuonesha kutotulia kwa aina fulani kana kwamba, anahofia kuna siri itatoka au kuna kitu ambacho tayari mume wake anakijua dhidi yake. Mara nyingi wasiwasi na mashaka humtawala sana mwanamke anayetoka nje , hasa katika hatua zake za awali za kutoka nje.

8.KUZUNGUMZIA KUACHWA: Kuna wakati mwanamke anaweza kuwa anatoa kauli za kuonesha kwamba, kama mwanaume anaona vipi , wanaweza kuachana.

Kama kila penye ugomvi kidogo tu mwanamke anakimbilia kusema, “kama ni kuachana, tuachane tu” hiyo inaweza kuwa ni dalili mbaya kwa mwanamke anayetoka nje ya ndoa kwa sababu hana tena upendo na mumewe.

Jumatatu, 29 Juni 2015

Cameron asema IS ni tishio kubwa

Cameron
Waziri mkuu nchini Uingereza David Cameron amesema kuwa wapiganaji wa islamic state ni tishio kubwa mataifa ya magharibi.
Bwana Cameron amesema kuwa wapiganaji wa Islamic state nchini Syria na Iraq wamekuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya Uingereza na kwamba vita dhidi yao vitakuwa 'mapambano ya kizazi chetu'.
Ameapa kutekeleza mashambulizi makali dhidi ya kundi hilo la jihad.
Matamshi ya bwana Cameron yanajiri baada ya kubainika kuwa takriban watalii 38 waliuawa siku ya ijumaa katika eneo moja la mapumziko nchini Tunisia.

JE?WEWE UNAJITANBUA AU UNATAKA KUJUA ANAYE JITAMBAUA,UNATAKA KUJUA? SOMA HI...

Kuna dalili zenye uwezo wa kukusaidia kubaini mtu anayejitambua katika maisha yake. Unapokosa dalili hizi ujue kabisa kuwa bado hujafikia ngazi ya juu kabisa ya kujiweza kujitambua na kuweza kuleta mabadiliko makubwa katika maisha yako. Ninapozungumzia mabadiliko nikiwa na maana ni kuwa na uwezo wa kupanga malengo na kuyafanikisha na kuishi kwa amani na furaha bila kutegemea mambo ya nje.onaviews.blog

Huenda dalili hizi zinaweza zikawa nyingi zaidi lakini kwa leo nitakutajia chache tu baadhi ambazo zitaweza kukusaidia moja kwa moja. Ukiona una dalili hizi au jamaa yako ana dalili hizi, huna budi kuanza kujua kwamba, uko kwenye kiwango cha juu cha kuweza kutumia nguvu zako za ndani na kuweza kufikia mafanikio yoyote makubwa unayoyahitaji katika maisha yako ya kila siku.

Kwanza, ni mtu anayepokea mambo katika hali halisi. Haathiriwi na mazoea, bali kile kilichopo, kinachopaswa kuona na kuchambuliwa, ndicho anachokipokea. Ina maana huchambua, bila kujali mazingira au mazoea yanasema nini. Unapokuwa unaona mtu ana dalili kama hiyo, elewa kabisa  mtu huyo anajitambua katika maisha yake.



Pili, ni mtu anayejikubali yeye kama yeye, hataki wala hatamani kuwa kama wengine. Ameridhika na kukubaliana na alivyo na maisha yake yalivyo. Lakini pia ni mtu anayekubali wengine kama walivyo na kutokutaka wengine wawe kama yeye. Vilevile ni mtu anayekubaliana na maumbile na uhalisia wake katika maisha yake.


Tatu, ni mtu ambaye hahitaji sana usiri na faragha. Mtu anayejitambua huzidi sana kujiondoa kwenye hali ya kuhitaji faragha sana kama ndiyo jambo la lazima. Kwa kujitambua, mtu huwa huru zaidi na hakuna jambo ambalo linaweza kuhitaji faragha. Kama yapo ni machache sana ambayo ni ya maana na sio kila jambo ni usiri na faragha.onaviews.blog

Nne, ni mtu ambaye huridhika na kutambua mchango wa mwingine au wengine na kukubaliana na yale yenye kumtokea. Kwa hali hiyo ni mtu ambaye hahemkwi. Majibu yake kwa mambo yanayomtokea yametulia sana, hasa kwenye suala la hisia zake. Anayejitambua hudhibiti hisia, na siyo hisia kumdhibiti yeye.


Tano, ni mtu ambaye hayuko tayari kuwa mtiifu, ni mtu ambaye hayuko tayari kuwa mtiifu tu bila kujua sababu. Kama ni kufuata jambo, hajiulizi maswali mengi sana kabla hajaamua. Hii ina maana kwamba, haendeshwi na mazoea, bali hutumia tafakari kwanza.

Sita, ni mtu mwenye uwezo wa kujibainisha na binadamu mwingine.  Aliyejitambua huamini kwamba, kile ambacho kinamfurahisha yeye, kinaweza kumfurahisha binadamu mwingine hivyohivyo kama alivyo yeye kilimvyomfurahisha.

Saba, ni mtu ambaye anapata uwezo mkubwa wa ubongo, mawazo ya kufanikisha na kufanya hali iwe bora zaidi. Kwa hiyo, ni mtu ambaye ana uwezo wa kubuni na kufanya mabadiliko mahali. Siyo mabadiliko ya kuleta fedha tu, bali mabadiliko ya kuwafanya binadamu wengine kujisikia vizuri.

Kwa kifupi, hizo ndizo dalili ambazo mtu anayejitambua anaweza kuwa nazo katika maisha na kuzitumi kuweza kuleta mabadiliko chanya katika maisha yake na jamii kwa ujumla.

Gatlin aweka mda bora mita 200

Justin Gatlin
Mwanariadha wa mbio fupi Justin Gatlin ameweka mda bora zaidi katika mbio za mita 200 na kuwa wa tano duniani aliposhinda mbio hizo nchini Marekani.
Raia huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 33 ambaye amehudumia marufuku mbili za utumiaji wa dawa za kusisimua misuli aliweka rekodi ya mda wa sekunde 19.57 mjini Oregon.
Rekodi hiyo imeifuta ile ya sekunde 19.68 aliyoiweka mnamo mwezi May wakati huo ikiwa rekodi bora duniani.
''Nilitaka kutoka ili niweke historia,na hivyo ndivyo nilivyofanya'',alisema Gatlin.
Gatlin ndiye mwanariadha wa mbio fupi aliyetawala mwaka 2015 baada ya kuweka rekodi bora mwaka huu ya sekunde 9.74 katika mbio za mita 100.

Uchaguzi wa ubunge wafanyika Burundi

Uchaguzi wa ubunge unaendelea nchini Burundi licha ya wiki ya maandamano ya ghasia dhidi ya uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza wa kutaka kuwania muhula wa tatu.

Baadhi ya vituo vya kupigia kura vilifunguliwa kuchelewa baada ya maguruneti kurushwa.
Upinzani umesusia uchaguzi huo.Muungano wa Ulaya unasema kuwa uchaguzi huo utazidisha mgogoro uliopo.
Umoja wa Afrika umekataa kutoa waangalizi ukisema kuwa baadhi ya masharti yaliowekwa hayajaafikiwa kwa uchaguzi kuwa huru na haki.
Zaidi ya watu 70 wameuawa tangu mgogoro huo uanze.Karibu watu 130,000 wamelitoroka taifa hilo.

Jumamosi, 27 Juni 2015

Tevez arejea nyumbani Boca Juniors

Straika wa Argentina Carlos Tevez amekamilisha Uhamisho wake kwenda Boca Juniors kutoka kwa Mabingwa wa Italy Juventus.

Tevez, mwenye Miaka 31, alianzia Soka lake huko kwao na Klabu ya Boca ambayo aliihama Mwaka 2004 kwenda Brazil kuchezea Corinthians na kisha kukaa Miaka 9 akichezea Klabu za Ulaya.
Huko Ulaya alizichezea Klabu za England, West Ham, Mwaka 2006-2007, Manchester United, 2007-2009, na Manchester City, 2009-2013, na kisha kwenda Italy kuichezea Juventus ambako msimu uliopita aliisaidia tena kutetea Taji lao la Ubingwa kwa kupiga Bao 20.
Majuzi Juventus walimbadili Tevez kwa kumsaini Straika wa Atletico Madrid ya Spain, Mario Mandzukic ambae anatoka Croatia.
Akithibitisha Uhamisho huu, Rais wa Boca Juniors Daniel Angelici alisema: "Ni Siku ya furaha sana na ya kuridhisha. Kurudi kwa Tevez akiwa kwenye kilele cha mafanikio ni habari njema kwa Washirika na Mashabiki wote wa Boca na Soka la Argentina!"

Burundi:''Uchaguzi utafanyika Jumatatu''

Balozi wa Burundi katika umoja wa mataifa amekariri kuwa uchaguzi utaendelea mbele Jumatatu licha ya shinikizo uahirishwe
Balozi wa Burundi kwenye umoja wa mataifa amesema kuwa uchaguzi utaendelea jinsi ulivyopangwa siku ya jumatatu licha ya ombi kutaka uahirishwe kutoka kwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki moon.
Ban anasema kuwa ana wasiwasi kuhusu hali ya usalama nchini Burundi kufuatia mzozo wa kisiasa unaoendelea huko.
null
Balozi Albert Shingiro aliuambia mkutano wa usalama wa umoja wa mataifa kuwa watu wanataka uchaguzi ufanyike.
Balozi Albert Shingiro aliuambia mkutano wa usalama wa umoja wa mataifa kuwa watu wanataka uchaguzi ufanyike.
Vyama vya upinzani na mashirika yasiyokuwa ya serikali tayari yametangaza kuwa watasusia uchaguzi huo.
Waandamanaji wanapinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza wa kuwania urais kwa muhula wa tatu wakidai kuwa inakiuka katiba ya Nvhi hiyo.
null
Uchaguzi wa ubunge unatarajiwa kufanyika Jumatatu
Rais Nkurunziza naye anashikilia kuwa awamu ya kwanza aliteuliwa na wajumbe wala sio raia kama vile inavyohitajika kwenye katiba iliyoundwa baada ya makubaliano ya Arusha yaliyokomesha vita vya wenyewe kwa wenye nchini humo.
Takriban watu 50 wameuawa nchini Burundi tangu mwezi Aprili mwaka huu wakati rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwa atawania muhula wa tatu.
null
Maandamano yalitibuka mjini Bujumbura baada ya Pierre Nkurunziza kutangaza kuwa atawania urais kwa muhula wa tatu
Maelfu ya raia wengine wa Burundi nao wamehamia mataifa jirani kwa hofu ya kuzuka mamchafuko zaidi.
Uchaguzi wa ubunge unatarajiwa siku ya Jumatatu huku uchaguzi wa urais ukipangiwa kufanyika tarehe 15 Julai mwaka huu.

JONAS MKUDE AANZA KUKAMUA BONDENI KWA MADIBA

Kiungo mahiri wa ukabaji wa Simba na Taifa Stars, Jonas Gerard Mkude ameanza majaribio katika klabu ya Bidvest Wits inayoshiriki ligi kuu Afrika kusini.Mkude ameonekana mwenye kujiamini katika majaribio hayo, huku akiwa na matumaini ya kufuzu ili kutimiza ndoto yake ya kucheza soka la kulipwa.
Mkude akiwa amekaa kwenye benchi la uwanja wa Bidvest kabla ya kuanza mazoezi

Ulaya yakataa kuiongeza Ugiriki muda zaidi

Uchumi mbaya wazua wasiwasi Ugiriki
Mawaziri wa fedha wa mataifa ya ulaya wamekatalia mbali ombi la Ugiriki la kutaka iongezewa muda zaidi wa kulipa deni lake kutoka Jumanne ijayo.
Ugiriki ina hadi Jumanne ijayo kulipa deni lake la zaidi ya dola bilioni moja nukta saba.
Serikali ya Uigiriki chini ya Alexis Tsipras ilikuwa imeombamuda wa majuma mawili iliiandae kura ya maoni
kuhusu makubaliano yaliyopendekezwa na wakopeshaji wa kimataifa wa nchi hiyo.
Ikiwa itaidhinishwa kura hiyo itafanyika tarehe tano mwezi Julai.
Awali wagiriki walipiga foleni nje ya mabenki wakihofia kuwa watawekewa masharti dhidi ya kutoa pesa zao.
Mwandishi wa BBC mjini Athens anasema kuwa kulikuwa na uvumi kuwa kiwango kipya cha pesa ambacho mtu anaweza kutoa kwa benki kinaweza kuwa euro 80.
Bunge la Ugiriki nalo liliandaa kikao cha dharura kujadili pendekezo ya kufanyika kwa kura hiyo ya maoni.
Waziri mkuu nchini Ugiriki Alexis Tsipras, anasema kuwa masharti hayo yanayotaka kupunguzwa kwa matumizi ya umma hayawezi kustahimiliwa.
Baadaye atakutana na waziri wa fedha wa nchi za ulaya mjini Brussels kuomba kuongezwa muda zaidi wa kulipa kwa mkopo wa sasa wa Ugiriki.
Muda unazidi kuyoyoma kwa bwana Tsipras kuwa amelipa deni la dola mbilioni 1.7 kwa shirika la IMF ifikapo jumanne ijayo..

TAFAKARI YA LEO:

Kama umewahi kuwa kiti cha mbele cha gari wakati wa usiku wewe kama dereva au abiria utakumbuka kuwa pamoja na taa za gari kuwashwa, mwanga wake haufiki mbali kumulika njia yote, bali humulika hatua chache hapo mbele.

Hata hivyo hali hiyo ya kutoona mbele haizuii kufika mwisho wa safari yenu.
  
Je, iweje leo wewe uache kujishughulisha na mambo ya yatakayoboresha maisha yako, kisa tuu ni kuwa eti hauoni kama kweli hapo mbele utafanikiwa ?
Kumbuka hauihitaji kuona wazi wazi mafanikio yako yatakavyokuwa hapo baadae, la msingi ni 

JE UNAFANYA LILILO SAHIHI ? 
JE, UNAJITUMA VYA KUTOSHA ? 

JE, UNAENDELEA KUJIFUNZA SIKU HADI SIKU ILI KUBORESHA SAFARI YAKO YA MAFANIKIO?
 
Kama unahitaji kuanza shule anza, kama unahitaji kuanza biashara anza, kama unahitaji kuanza kuboresha chochote kile anza leo, usisite kwa kuwa eti mafanikio hayapo wazi.
Na kumbuka hata kama hautofanikiwa, bado utakuwa umejifunza kitu na utaweza kuboresha safari yako.ONAVIEWS.BLOG
 


 

 
 
Blogger Templates