Social Icons

Jumatatu, 29 Juni 2015

Gatlin aweka mda bora mita 200

Justin Gatlin
Mwanariadha wa mbio fupi Justin Gatlin ameweka mda bora zaidi katika mbio za mita 200 na kuwa wa tano duniani aliposhinda mbio hizo nchini Marekani.
Raia huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 33 ambaye amehudumia marufuku mbili za utumiaji wa dawa za kusisimua misuli aliweka rekodi ya mda wa sekunde 19.57 mjini Oregon.
Rekodi hiyo imeifuta ile ya sekunde 19.68 aliyoiweka mnamo mwezi May wakati huo ikiwa rekodi bora duniani.
''Nilitaka kutoka ili niweke historia,na hivyo ndivyo nilivyofanya'',alisema Gatlin.
Gatlin ndiye mwanariadha wa mbio fupi aliyetawala mwaka 2015 baada ya kuweka rekodi bora mwaka huu ya sekunde 9.74 katika mbio za mita 100.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates