Social Icons

Jumamosi, 3 Oktoba 2015

AIBU...............Soka ya Tanzania iko chini zaidi Afrika mashariki

Image captionTaifa Stars
Licha ya kupanda nafasi nne hadi nambari 136,Tanzania imeorodheshwa ya chini zaidi na shirikisho la soka duniani FIFA katika soka ya Afrika mashariki.
Kulingana na orodha ya FIFA iliotolewa siku ya Alhamisi,Uganda imeorodheshwa ya 75,ikifuatiwa na Rwanda katika nafasi ya 93.
Uganda na Rwanda zimeshuka nafasi 4 na 15 mtawalia.
Burundi nayo imerodheshwa nambari ya 113 ikiwa ya tatu ikifuatiwa na Kenya katika nafasi ya 131 ikiwa nambari 4.
Image captionTaifa Stars
Taifa Stars ya Tanzania ambayo ililazimu sare ya 0-0 dhidi ya timu ya Super Eagles kutoka Nigeria katika mechi za kufuzu kwa kombe la Afrika inashikila nafasi ya 5 na ya mwisho katika Afrika mashariki ikiwa katika nambari 136 duniani.
Kwengineko orodha hiyo mpya inaonyesha kuwa Liberia na Afrika Kusini ndizo zilizofanywa vyema.
Mataifa hayo mawili yameorodheshwa ya 95 baada ya kupanda kwa nafasi 65 na 144 baada ya kupanda kwa nafasi 54 mtawalia.
Image captionTaifa Stars
Kulingana na Shrikisho la FIFA,Ujerumani inaongoza ikifuatiwa na Argentina kisha Ubelgiji nafasi ya 3 na Ureno katika nafasi ya nne.

Walimu wasitisha mgomo Kenya


Image captionKatibu mkuu wa chama cha walimu nchini KNUT Wilson Sossion
Mgomo wa walimu nchini Kenya hatimaye umesitishwa.
Walimu sasa watarudi shuleni ili kuendelea kufunza siku ya jumatatu.
Katibu mkuu wa KNUT Wilson Sossion amesema kuwa muungano huo hatahivyo hautaondoa kesi ambapo tume ya huduma za walimu TSC imekataa rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama wa kuwapatia walimu hao nyongeza ya mishahara ya kati ya asilimi 50-60
Hatua hiyo ya muungango wa walimu nchini Kenya KNUT inatokana na agizo lililotolewa na Jaji Abuodha mnamo tarehe 25 mwezi Septemba.
Mgomo huo ulikwamisha masomo nchini Kenya huku walimu wakitaka nyongeza ya mishahara pamoja na ile ya marupurupu.
Walimu sasa wanaitaka tume ya kuajiri walimu TSC kuwapatia mishahara ya mwezi Septemba baada ya tume hiyo kusema kuwa haitawalipa kwa kuwa walikuwa katika mgomo.
Hatua hiyo inatoa afueni kwa wanafunzi wa shule za uma ambao walilazimika kukaa nyumbani kwa kipindi chote cha mgomo huo.
Image captionWalimu
Jaji wa mahakama ya wafanyikazi Nelson Abuodha aliwaagiza miungano yote miwili ya walimu kuahirisha mgomo huo ili kutoa fursa ya majadiliano.
''Kwa maslahi ya watoto wetu katika shule za umma na haki zao chini ya katiba mpya,mahakama imeagiza miungano hiyo ya walimu kuahirisha mgomo huo ulioanza terehe mosi mwezi Septemba kwa siku 90,ili wanachama wake waanza kazi mara moja'',alisema jaji Abuodha.
Mda mfupi tu baada ya agizo hilo kutolewaserikali ilitangaza kuwa shule zote zitafunguliwa sikuya jumatatu na kufungwa mnamo tarehe 20 mwezi Novemba
 
 
Blogger Templates