Social Icons

Alhamisi, 20 Agosti 2015

kaseja atua Mbeya city....jana.

Baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu golikipa mkongwe na mahiri Juma Kasejakuwa bila timu na kuhusishwa kujiunga na vilabu mbalimbali hatimaye uvumi huo umemalizika August 19 baada ya kusaini mkataba wa miezi sita wa kuitumikia klabu yaMbeya City kutoka Jijini Mbeya.
IMG-20150819-WA0008 (1)
Mkataba wa Juma Kaseja wa kujiunga na klabu ya Mbeya City umesainiwa August 19 mbele ya meneja wake mpya Athumani Tippo hivyo huo ni mwisho wa uvumi wa habari za Juma Kaseja atacheza wapi msimu ujao, taarifa hizo zinakuwa pigo kwa kocha waMwadui FC ya Shinyanga Jamhuri Kiwelu ambaye alikiri katika vyombo vya habari kuwa ana hitaji huduma ya Kaseja kikosini mwake.
Kabla ya kusaini mkataba na Mbeya City Juma Kaseja alikuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha zaidi ya miezi nane baada ya kuingia katika mgogoro wa kimkataba na iliyokuwa klabu yake ya zamani ya Yanga nakufanya kesi hiyo kutinga mahakamani.

Rais Nkurunziza aapishwa kwa muhula wa 3

Rais Nkurunziza aapishwa
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza anaapishwa kwa muhula wa tatu uliozua utata.
Mwandishi wa BBC Prime Ndikumagenge nchini Burundi anasema kuwa sherehe hiyo imefanyika kwa mshangao mkubwa kwa kuwa rais Nkurunziza alitarajiwa kuapishwa wiki ijayo.
Rais Nkurunziza
Takriban watu 10 wameuawa tangu Nkurunziza atangaze mnamo mwezi Aprili kwamba atawania muhula wa tatu wa urais.
Serikali inaushtumu upinzani ambao unasema kuwa muhula huo ni kinyume na sheria kwa kuzua ghasia.
Nkurunziza
Umoja wa Afrika,muungano wa Ulaya na wizara ya maswala ya kigeni ya Marekani wote wameonyesha wasiwasi wao kwamba uchaguzi huo wa mwezi Julai haukuwa huru na wa haki.

IS lakiri kutekeleza shambulizi Misri

Cairo
Bomu kubwa limelipuka karibu na makao makuu ya usalama kaskazini viungani mwa mji mkuu wa Misri, Cairo.
Watu 29 walijeruhiwa katika mlipuko huo ikiwemo maafisa sita wa polisi.
Bomu hilo lilisikika katika maeneo mengi ya mji huo na mwandishi wa BBC anasema kuwa hayakuwepo majeraha mengi kwa kuwa mlipuko huo ulitokea usiku.
Mlipuko Cairo
Eneo hilo kwa sasa limefungwa na kuna maafisa wengi wa polisi katika barabara za mji huo.
Kundi la wapiganaji wa Islamic State limekiri kutekeleza shambulizi hilo.

Pedro:Kwanini ni chaguo la Chelsea?

Pedro Rodriguez
Chelsea wanaonekana kuishinda kasi Manchester United katika kumsajili Pedro baada ya timu hiyo ya London kukubali kutoa kitita cha paund milioni 21 kwa mchezaji huyo mwenye miaka 28.
Pedro kwa sasa yupo katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wake huku mashabiki wa Chelsea wakiwa na msisimko mkubwa kumtizama mchezaji huyo akiwaruudhisha katika mbio za ubingwa wa mataji mbalimbali.
Pedro
Pedro anatazamiwa kujijengea umaarufu kwa mashabiki wa Chelsea kutokana na kuwa msikivu na mnyenyekevu huku pia akiwa na shauku ya kucheza ambapo mashabiki wa Uingereza hupenda watu kama hao.
Atapata ukaribisho mzuri pia katika vyumba vya kubadilishia nguo vya Chelsea kutoka kwa wachezaji wenzake kwa sababu sio mbinafsi,ni mpambanaji na mkarimu ambaye anaweka mahitaji ya timu mbele kuliko ya kwake binafsi.
Pedro wakati akiwa Barcelona, alikua akitumika zaidi kama mchezaji wa akiba licha ya kuifanyia makubwa timu hiyo.

MAGAZETI YA LEO





PICHA YA SIKU

KINGWENDU ACHUKUA FOMU YA UBUNGE

KIPINDUPINDU KIPO JIJINI DAR ES SALAAM TUWE MAKINI.


 Muuguzi Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Nusura Kessy (kushoto), akiwaelekeza wauguzi wa saidizi wake namna ya kuchanganya dawa maalumu ya kuondoa vijiji vinavyoweza kuwa vya ugonjwa wa kipindupindu katika kambi ya wagonjwa walioathiriwa na ugonjwa huo iliyopo Zahanati ya Mburahati Dar es Salaam leo asubuhi. Katika kambi hiyo kuna wagonjwa 21 kati yao watoto ni 7.
 Vyombo vikiwekwa kwenye dawa.
 Muuguzi Msaidi wa Zahanati ya Mburahati, Maimuna Pazi (kushoto) na Mlinzi wa Zahanati hiyo, Abdallah Mbagala wakisaidiana kuweka dawa maalumu ya kuzuia kuenea kwa vijidudu vya maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu katika vyombo walivyoletewa chakula na ndugu zao katika kambi ya matibabu kwa wagonjwa walioathiriwa na ugonjwa huo iliyopo katika Zahanati ya Mburahati Dar es Salaam leo asubuhi.
Dawa hiyo maalumu ikiwekwa katika vyombo vya kutumia.



HALI ya ugonjwa wa kipindupindu ulioikumba maeneo kadhaa ya jiji bado inaonesha ni tete kufuatia idadi ya wagonjwa huo kuongezeka kutoka watu 34 na kufikia 43.

Hayo yamebainishwa na Muuguzi Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni ambayo imeathiriwa na ugonjwa huo, Nusura Kessy wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi.

Kessy ambaye anasimamia kutoa huduma katika kambi ya wagonjwa iliyopo Zahanati ya Mburahati alisema mpaka jana asubuhi kulikuwa na wagonjwa 21 kati yao watoto ni saba na wagonjwa 10 wameruhusiwa kurudi majumbani mwao baada ya hali zao kuimarika.

"Hali bado sio nzuri kwani tunaendelea kupokea wagonjwa kutoka Hospitali ya Mwananyamala hata hivyo uwezo wa vyumba vya kulaza wagonjwa ni watu 16 tu" alisema Kessy.

Alisema kutokana na changamoto hiyo wameomba mahema ambayo yatafungwa nje ya zahanati hiyo kwa ajili ya kusaidia ongezeko hilo la wagonjwa.

Kessy alitunmia fursa hiyo kuwaomba wananchi kuzingatia usafi hasa baada ya kutoka kujisaidia kunawa kwa kutumia maji ya moto na kuto kula vyakula holela pamoja na kuchemsha maji ya kunywa.

Muuguzi huo pia alitoa mwito kwa wananchi pale wanapo muona mtu anatapika na kuharakisha kutoa taarifa mapema na kumpeleka mgonjwa hospitali kwa matibabu.

Alisema kuwa kati ya watu waliopoteza maisha kwa ugonjwa huo kati yao ni walifariki wakiwa majumbani na njiani wakati wakipelekwa hospitali wakiwa katika hali mbaya baada ya kucheleweshwa

Jumatano, 19 Agosti 2015

ZARI ASEMA WATAIONESHA SURA YA TIFFAH BAADA YA SIKU…


Shauku kubwa ambayo mashabiki wa Diamond Platnumz na Zari the Boss Lady wako nayo kwa sasa ni kuiona sura ya mtoto wao wa kike Latiffah Naseeb a.k.a Princess Tiffah.

Hii ni kutokana na maneno mengi ambayo yanaendelea hivi sasa kwenye mitandao ya kijamii, wengi wanahamu ya kujua mtoto anafanana na nani kati ya baba na mama yake.

Picha zote za Tiffah zilizowekwa kwenye mitandao ya kijamii zinamuonesha mikono, miguu, mdomo lakini amekuwa haoneshwi sura yake.

Shabiki mmoja alimuuliza swali Zari kupitia ukurasa wake, ni lini wana mpango wa kuionesha sura ya Tiffah, na jibu la Zari lilikuwa “Baada ya siku 40”.

Hadi sasa ukurasa wa Instagram wa Princess Tiffah una followers 87,650.

704 wahamia chadema,jimbo analo gombe mgombea wa CCM Nape.




Aliyekuwa mgombea wa kura za maoni kupitia chama cha mapinduzi jimbo la mtama SELEMANI METHEW amekihama chama hicho na kuondoka na wana CCM wapatao 704 na kuhamia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kwa kile anachodai hakutendewa haki katika mchakato mzima wa kura za maoni.

METHEW amesema kuondoka ndani ya CCM kumetokana na maamuzi ya wananchi ambao wameona haiwezekani na haitawezekana kiongozi wanayemuitaji kufanyiwa hila na mizengwe,kudhulumiwa haki yake ya msingi ya kuwaongoza wananchi wa jimbo la mtama.

Amesema jimbo la mtama halihitaji usanii bali linaitaji mgombea shupavu atakayeweza kupambana na mgombea wa CCM Nape Nnauye huku akisisitiza uwezo huo anao.

Mkutano huo umeudhuriwa na wanawake wengi ambao kwa sehemu kubwa ndiyo waliorudisha kadi za CCM.

Mkutano huo ulipambwa na vimbwanga mbalimbali likiwemo tambiko rasmi lililotumika kumzindika mgombea huyo ikiwa ni pamoja na kumpa nguvu na kumkinga na majanga ili aweze kufanikisha kampeni na kuibuka na ushindi.

UKAWA WAKINGAZA MAJIMBO WALIYOGAWANA KATIKA UCHAGUZI MKUU


 Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi,  Nderakindo Kessy (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho, Ilala Dar es Salaam jana, wakati akitangaza majimbo yaliyochini ya vyama vinavyounda Ukawa ambayo vyama hivyo vitasimamisha wagombea wao katika uchaguzi mkuu. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha NLD, Masudi Makunjunga.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Shaweji Mketo (wa pili kulia), akizungumza katika mkutano huo na waandishi wa habari. Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha NLD, Masudi Makunjunga, Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi,  Nderakindo Kessy na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika.
 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika, akizungumza katika mkutano huo.

Darron Gibson apigwa faini

wachezaji wa timu ya Everton
Mchezaji wa Everton ambaye ni raia wa Jamhuri ya Ireland nyota wa kabumbu Darron Gibson, amepigwa faini kwa kusababisha ajali na kukimbia; ajali iliyomuacha muendesha baisikeli na majeraha mwilini mwake.
Kiungo huyo mwenye miaka ishirini na saba aliwekwa kizuizini mwanzoni mwa wiki hii baada ya polisi kupokea taarifa za tukio la mwendesha baisikeli aliyegongwa na gari ambayo pia ilikwenda kugonga pampu ya kujaziamafuta kwenye kituo kimoja cha mafuta.Gibson anatuhumiwa kuendesha gari akiwa amelewa ,na kuhusika kwenye tukio lingine awali huko Altrincham, Manchester.
Daron Gibson
Inaelezwa zaidi kwamba mchezaji nyota huyo alikuwa akiendesha mwenyewe gari aina ya Nissan Skyline GT-R Nismo nyeusi na ajali hiyo imetokea mita chache kutoka kwenye makazi yake .
Polisi wa Greater Manchester wamesema kwamba Gibson ameshtakiwa kwa kuendesha bila uangalifu na bila kujali,kuendesha akiwa amekunywa pombe na pia kushindwa kusimama baada ya ajali hiyo.
Gibson mzaliwa wa Londonderry alianza kuonesha cheche zake katika klabu ya Manchester United kabla ya kujiunga na klabu ya Everton mnamo mwaka 2012 kwa gharama ya paundi milioni moja. Mchezaji huyo anaendelea kupona kutokana na ajali ya awali aliyoipata uwanjanai.Naye msemaji wa klabu hiyo Everton amekataa kuzungumza lolote kuhusiana na tukio hilo .

MAGAZETI YA LEO

 





Kuachiliwa kwa Pistorius kumepingwa

Mwanariadha Oscar pistorius
Waziri wa sheria nchini Afrika Kusini amepinga uamuzi wa kuachiliwa kwa mwanariadha Oscar Pistorius.
Michael Masutha amasema kuwa uamuzi wa kumuachilia mwanariadha huyo umechukuliwa mapema.
Oscar Pistorius na Reeva Steenkamp
Pistorius amekaa gerezani kwa muda wa miezi kumi baada ya kumuua kwa kumpiga risasi mpenziwe Reeva Steenkamp na alitarajiwa kuachiliwa ili atumikie kifungo chake cha nyumami siku ya Ijumaa.

Wanajeshi 8 wa Uturuki wauawa

Wanajeshi 8 wa Uturuki wauawa
Wanajeshi wanane wa Uturuki wameuawa kwenye shambulizi la bomu la kutegwa kando ya barabara kusini mashariki mwa nchi.
Hakuna kundi lililodai kuhusika kwenye shambulizi hilo lilitokea katika mkoa wa Siirt lakini maafisa wa usalama wamewalaumu waasi wa PKK au kundi la Kurdistan Workers Party.
Shambulizi hilo linafanyika wakati kuna ghasia kati ya PKK na wanajeshi wa Uturuki. Watu kadha wameuawa tangu usitishwaji wa mapigano wa miaka miwili uvunjike mwezi Julai.

Jumapili, 16 Agosti 2015

Vita vya Iraq:Bush na Clinton walaumiana

Clinton na Jeb Bush
Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Demokrat Hillary Clinton amemshtumu mpinzani wake kutoka chama cha Republican Jebb Bush kuhusu ni nani aliyesababisha msukosuko nchini Iraq.
Siku ya jumanne bwana Bush aliishtumu serikali ya rais Obama kwa kuyaondoa mapema majeshi ya Marekani mwaka 2011 swala analosema limesababisha madhara makubwa.
Lakini Bi Clinton alijibu kwa kusema ni nduguye George W Bush ambaye aliomba majeshi ya Marekani kuondolewa nchini humo.
Vita vilivyoanzishwa na Marekani nchini Iraq mwaka 2003 vimesababisha msukosuko nchini humo.
Bwana Bush alisema kuwa kuondolewa kwa vikosi vya Marekani nchini Iraq ilikuwa makosa yaliosababisha maafa makubwa ikiwemo msukosuko na hatimaye kuanza kwa kundi la wapiganaji wa Islamic State.
''Walitaka kuwa katika kumbukumbu za kihistoria badala ya kuleta amani'',Bwana Bush alisema akimshtumu rais Obama na Bi Hillary Clinton wakati Clinton alipokuwa katibu wa maswala ya kigeni mwaka 2009 na 2013.

IAAF lilihujumu utafiti wa dawa sisimuzi

Mashindano ya riadha mjini Daegu
Ripoti za vyombo vya habari kutoka nchini Uingereza na Ujerumani zimelilaumu shirikisho la riadha duniani IAAF kwa kuhujumu utafiti ambao uligundua kuwa thuluthi moja ya wanariadha walikiri kuvunja sheria za matumizi ya dawa za kusisimua misuli.
Kulingana na gazeti la Sunday Times na kituo cha ARD cha Ujerumani ni kuwa mamia ya wanariadha waliwaambia watafiti kuwa walitumia dawa za kuongeza nguvu zilizopigwa marufuku walipohojiwa miaka minne iliyopita.
Ukaguzi wa dawa sisimuzi
Chuo cha Ujerumani kilichoongoza utafiti huo kinasema kuwa IAAF imezuia kuchapishwa kwa takwimu hizo.
IAAF inasema kuwa bado mazungumzo yanaendelea.
Michezo ya riadha mjini Helsinki
Mapema mwezi huu IAAF ilikataa madai ya vyombo hivyo vya habari kuwa kuna matumizi makubwa ya dawa za kuongeza nguvu katika riadha.

JIONEE GHALIKA YA LOWASSA JIJINI ARUSHA






Jumamosi, 15 Agosti 2015

MAPOKEZI YA LOWASSA ARUSHA.









Kiongozi wa IS alidaiwa kum'baka mateka

Kayla Mueller
Mfanyikazi wa huduma za misaada kutoka Marekani ambaye aliuawa mnamo mwezi februari akiwa mateka wa kundi la Islamic State nchini Syria alinyanyaswa kijinsia na kiongozi wa kundi hilo Kulingana na maafisa wa Marekani.
Kayla Mueller mwenye umri wa miaka 26 aliripotiwa kubakwa mara kadhaa na Abu Bakr al Baghdadi.
Maafisa wa kukabiliana na Ugaidi walielezea familia yake mnamo mwezi Juni.
Mueller alitekwanyara wakati alipokuwa akifanya kazi mjini Allepo nchini Syria mwaka 2013.
Al Baghdad
Wapiganaji wa IS wanasema kuwa aliuawa katika shambulizi la angani lililotekelezwa na Jordan ,lakini Marekani inalilaumu kundi hilo kwa kifo chake.
''Tuliambiwa kwamba Kayla aliteswa na kwamba alikuwa mali ya Baghdadi. Tuliambiwa mnamo mwezi Juni na serikali'',wazazi wake Carl na Marsha waliliambia shirika la habari la ABC.
Inadaiwa kuwa Baghdad alimchukua afisa huyo wa misaada kwa nyumba ya mwanachama mwengine wa IS Abu Sayyuf ambaye alikuwa akisimamia kitengo cha mafuta na gesi hadi kifo chake katika oparesheni ya vikosi maalum vya Marekani mnamo mwezi May.
 
 
Blogger Templates