Serikali ya Iraq imeupinga mpango uliotangazwa na Marekani wa kutuma vikosi maalum kupambana na wanamgambo wa itikadi kali wa dola la kiislam-IS nchini humo.Kabla ya hapo wanamgambo wa kishiya wenye ushawishi mkubwa nchini humo walisema watapambana na vikosi hivyo vya Marekani vikiletwa Iraq.Waziri wa ulinzi wa Marekani Ashton Carter,alisema katika kikao cha masuali na majibu cha baraza la wawakilishi jana,vikosi maalum vya Marekani vitapelekwa Iraq.Lengo ni kuwasaidia wanajeshi wa Iraq na makundi ya wapiganaji wa kikurdi-Peshmerga katika juhudi zao za kupambana na wanamgambo wa itikadi kali wa dola la kiislam-IS.Kwa mujibu wa waziri wa ulinzi wa Marekani,wanajeshi hao maalum wa Marekani watakaowekwa Iraq wanaweza pia kusaidia nchini Syria.Wakati huo huo serikali ya Marekani inafikiria uwezekano wa kutuma vikosi maalum vyengine katika nchi jirani ya Syria.
VOA Express
-
VOA Express ni matangazo mapya yenye mwendo wa kasi yakiangalia habari mpya
za mchana na maelezo ya maswala yanayohusu vijana na wanawake. Matangazo
haya y...
Saa 1 iliyopita
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni