Social Icons

Jumapili, 17 Novemba 2013

JE? ZAHA KUTUA NEWCASTLE KWA MKOPO JANUARI .

zaha 2dc88
KLABU ya Newcastle imeanza mazungumzo ya kumchukua winga wa Manchester United, Wilfried Zaha kwa mkopo ifikapo Januari. Wawakilishi wa mchezaji huyo wa England walikutana na viongozi wiki iliyopita kujadili uwezekano wa mkopo wa miezi sita, na kocha wa United, David Moyes ametoa wazo la kumpatia Zaha timu atakayokuwa akipata naba kikosi cha kwanza katika Ligi Kuu.
Zaha, mwenye umri wa miaka 20, alikuwa mchezaji wa mwisho kusajiliwa na Sir Alex Ferguson kabla hajastaafu, lakini amecheza mechi moja tu ya Kombe la Ligi, maarufu kama Capital One chini ya Moyes.
Katika mazungumzo: Wilfried Zaha yupo katika mazungumzo na Newcastle United juu ya uwezekano wa kwenda kucheza kwa mkopo
Mchezaji huyo wa zamani wa Crystal Palace aliichezea mechi ya kwanza England dhidi ya Sweden mwaka jana, lakini kutokana na kukosa nafasi katika klabu yake, amejikuta akirejeshwa kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 21. Zaha amekataa kurejea Palace.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates