Social Icons

Jumatano, 25 Desemba 2013

BAADA YA RUBEN,FALCAO NAYE ATETA YAKE: RONALDO NI MCHEZAJI BORA ZAIDI YA LIONEL MESSI

Mshambuliaji wa Monaco  Radamel Falcao anaamini kwamba mshambuliaji wa Real Madrid  Cristiano Ronaldo ni mchezaji mzuri kuliko staa wa klabu ya Barcelona Lionel Messi.

Mchezaji huyo wa Colombia anawakubali wachezaji wote wawili, ingawa Falcao anaamini Cristiano ni bora zaidi ya Messi.

"Messi na Cristiano ni wachezaji muhimu na wakubwa duniani leo hii lakini, kwangu mimi naamini Ronaldo ni bora zaidi," alisema mchezaji huyo mwenye miaka 27 alipoongea na El Tiempo.

Falcao pia amesema ni Cristiano Ronaldo anayestahili kuwa mchezaji bora wa dunia katika tuzo za Ballon D'or zitakazotolewa mwezi ujao ambapo Ronaldo anapambana na Ribery pamoja na Messi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates