Social Icons

Ijumaa, 27 Desemba 2013

SOMA HIII...MSICHANA ALIYEKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI CHINA WAUMIZA VICHWA VYA WENGI NCHINI TANZANIA

 
 Msichana wa Tanzania aliyekamatwa na madawa ya kulevya akiwa amesimama karibu na meza yalipowekwa madawa yaliyotolewa kutoka kwenye mwili wake
 
Ni msichana gani wa Tanzania aliyekamatwa na madawa ya kulevya nchini China? Hilo ni swali gumu ambalo kila mmoja amekuwa akijiuliza bila kupata jibu la uhakika. Mtandao wa chinadaily.com.cn umeandika habari na kuweka picha za kukamatwa kwa msichana huyo mwenye umbo refu, mwenye nywele ndefu na mweupe. Mtandao huo umeandika: Msichana mwenye miaka 28 kutoka Tanzania alikamatwa kwa tuhuma za kumiliki madawa ya kulevya huko -Macao, Dec 19, 2013. Alikuwa ameficha kilo 1.1 za heroin zenye thamani ya $137,720 ( sawa na zaidi ya shilingi milioni 85) ndani ya mwili wake na kuchukua ndege kutoka Thailand hadi Macao. Alisema alikuwa akielekea Guangzhou, mji mkuu wa jimbo la Kusini mwa China Guangdong.

Madawa yaliyotolewa kwenye mwili wa msichana huyo mwenye miaka 28 yakioneshwa mbele ya waandishi wa habari
 
 
Msichana wa Tanzania aliyekamatwa na madawa ya kulevya na aliyefunikwa uso wake akiwa chini ya ulinzi
Tunafahamu kuna majina tayari yanayotajwa kuwa huenda wakawa ndio msichana huyo lakini hatuwezi kuyataja wala kuthibitisha kwa sasa ili kuepuka kuripoti habari zisizo na ukweli. www.onaviews.blogspot.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates