Social Icons

Jumanne, 13 Mei 2014

MZIGO WA UBELGIJI HUO KWENDA KOMBE LA DUNIA BLAZUKAAA,UNAYE MPENDA YUPO?

397383_heroa
KOCHA wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots ametaja kikosi chake kwa ajili ya kombe la dunia na kumujumuisha kinda wa Manchester United Adnan Junazaj.
Ubelgiji imepangwa kundi H na timu za Russia, Algeria na kurea kusini ambao wataanza kampeni zao juni 17 dhidi ya Algeria.
Wilmots ametangaza kikosi cha wachezaji 24 na wengine 6 wa ziada kama itatokea majeruhi katika kikosi chake.
Mbali na kinda huyo mwenye miaka 19 , Thibaut Courtois, Jan Vertonghen, Vincent Kompany Dries Mertens, Eden Hazard, Marouane Feillaini na Romelu Lukaku, Axel Witsel wamejumuishwa katika kikosi hicho.
Ajabu nyingine ni kujumuishwa kwa mshambiliaji wa Lille ya ufaransa mwenye miaka 19, Divock Origi, ambaye amefunga mabao matano katika mechi 29 alizocheza Ligue 1 msimu huu.
Kikosi kizima hiki hapa: 
Walinda Mlango: Thibaut Courtois, Simon Mignolet, Koen Casteels, Silvio Proto
Mabeki: Toby Alderweireld, Laurent Ciman, Anthony Vanden Borre, Vincent Kompany, Daniel Van Buyten, Jan Vertonghen, Thomas Vermaelen, Nicolas Lombaerts
Viungo: Axel Witsel, Steven Defour, Marouane Fellaini, Mousa Dembele, Nacer Chadli, Kevin De Bruyne
Washambuliaji: Eden Hazard, Romelu Lukaku, Divock Origi, Dries Mertens, Kevin Mirallas, Adnan Januzaj
Wachezaji wa akiba: Sebastien Pocognoli, Jelle Van Damme, Thorgan Hazard, Radja Nainggolan, Michy Batshuayi, Guillaume Gillet


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates