Social Icons

Ijumaa, 23 Mei 2014

Hati hati ya Suarez kutocheza kombe la dunia kutokana majeraha;wauruguay wamtishia Dummett

Mlinzi wa Newcastle Paul Dummett ametishiwa maisha yake na mashabiki wa Uruguay wanaomlaumu kwa kusababisha jeraha lililomlazimu Luis Suarez kufanyiwa upasuaji ambao sasa wanahofu huenda ikaathiri uwezo wake katika kombe la dunia .

Mashabiki hao walimtumia Dummett, 22 jumbe kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter wakimkaripia kwa kumchezea Suarez visivyo alipoonyeshwa kadi nyekundu liverpool ilipoilaza Newcastle 2-1 uwanjani Anfield.
Uruguay imeratibiwa kufungua kampeini yao kombe la dunia katika kundi D dhidi ya Costa Rica mnano Juni 14 na kisha kuchuana dhidi ya Uingereza siku tano baadaye.
Dummett ametajwa katika kikosi cha Wales kinachopangiwa kuchuana na Uholanzi katika mechi ya kujipima nguvu juma lijalo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates