Social Icons

Jumanne, 15 Julai 2014

WASANII WA BONGO PAMOJA NA WADAU WA SANAA NCHINI WASHIRIKI WARSHA ILIYOHUSISHA WASANII KUTOKA MAREKANI

 Muigizaji na Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha E! cha nchini Marekani, Terrence J akiongea mbele ya wasanii fani mbalimbali kutoka Tanzania leo.
Muigizaji na Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha E! cha nchini Marekani, Terrence J akisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikichangiwa na wasanii wa Tanzania waliohudhuria warsha hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu Jijini Dar Es Salaam.
Shaka Zulu akichangia mada kwenye warsha na wasanii wa bongo
 Baadhi ya wadau wa Sanaa wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Wasanii wa Muziki na Filamu kutoka Nchini Marekani ambao wameendesha warsha kwa wasanii wa bongo
 Mzee Yusuph akifuatilia Kwa Makini
 Izzo Business akiwa makini 
 Wadau wa sanaa kutoka nchini Tanzania wakifuatilia mada kwa makini
 

WASANII mbalimbali  na wadau wa sanaa nchini Tanzania leo wamepewa semina ya jinsi wanavyoweza kuanzisha soko thabiti la kazi zao kwa kuiga mfumo wa nchi ya Marekani.
Semina hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa Bank Kuu ya Tanzania (BOT) jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wasanii wa Bongo Fleva, Maigizo, Muziki wa Injili, Maprodyuza na wadau mbalimbali wa tasnia hiyo huku wageni waalikwa wakiwa ni Aliyekuwa meneja wa msanii wa muziki Ludacris na Prodyuza, Shaka Zulu. Mwana Hiphop na Prodyuza, David Banner na Terrence J ambaye ni staa wa Think Like A Man 2, mwingine ni  Liver Sheldon

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates