Social Icons

Jumanne, 15 Julai 2014

ANGALIA PICHA ZA MAPOKEZI YA TIMU UJERUMANI

Timu ya taifa imewasili nchini humo kwa kishindo

Maelfu ya mashabiki wa soka wamekuwa wakisubiri tangu asubuhi na mapema mjini Berlin kuwakaribisha wachezaji hao.

wa dada wakiwa wamevaa flana zenye nembo ya Dr.dree(beats) baada ya dree kutoa head phone za dhabu kwa timu ya ujerumani.

Sherehe zitafanyika katika eneo la Brandenburg Gate, ambako wachezaji wataonyeshea kombe lao, ambalo walilishinda katika fainali ya mashindano hayo dhidi ya Argentina.
Wengi wamepokea ushindi wa timu ya Ujerumani kwa shangwe kuu
Shangwe na vigelegele vimeshuhudiwa huku umati mkubwa wa watu ukitarajiwa kushuhudia kombe hilo ambalo litapitishwa mjini kote.
Watu wengi wamenunua jesi zenye nyota nne kuashiria ushindi wa nne wa nchi hiyo katika kombe la dunia.
Mashabiki wamepoke ushindi kwa shangwe
Wachezaji wa timu hiyo ambao huchezea timu ya Bayern Munich pia watapata ukaribisho mkubwa baadaye mjni Munich.
Mwandishi wa BBC Steve Evans ambaye yuko mjini Berlin anasema kuwa watu nusu milioni wanatarajiwa kukutana na wachezaji hao mjini Berlin.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates