Social Icons

Jumatano, 2 Julai 2014

Origi ni Liverpool, Tottenham Hotspurs na Arsenal.

Origi akunja mkwaju katika mechi ya Ubelgiji nchini Brazil

Oduor, ambaye ni mjomba wake Origi, anasema tofauti na maoni ya wengine kwamba mchezaji huyo angali mbichi kucheza ligi kuu ya England kwake yeye anaona yuko tayari kabisa.

''Asipoteze muda wake kwa sababu huu ndio umri mzuri kwake kushiriki ligi hiyo. Nitazungumza naye na babake baada ya kombe la dunia kwani singetaka tuanze kuzungumzia mengine wakati huu ila kombe la dunia tu.’’“Nimefuatilia mechi zote alizocheza kufika sasa katika kombe la dunia na sina shaka kijana huyu wa ndugu yangu(Mike Okoth) anaweza kucheza ligi kuu ya England bila tatizo kwa sababu ana mwili mzuri, nguvu, akili ya mshambuliaji na kasi itakikanayo kwa ligi kama hiyo,’’ asema Oduor.

Baadhi wanahisi kuwa Origi bado ni mbichi ingawa ameonyesha kipawa chake Brazil
Origi, mwenye umri wa miaka 19 ameonyesha mchezo mzuri kwenye mashindano ya kandanda ya kombe la dunia nchini Brazil, na kwa mara ya kwanza alicheza dakika zote tisini dhidi ya Marekani kwenye mechi yao ya raundi ya pili, na hatimaye Romelu Lukaku akaingia uwanjani naye Origi akapumzika.
Miongoni mwa timu za ligi kuu ambazo zimeonyesha nia ya kumsajili Origi ni Liverpool, Tottenham Hotspurs na Arsenal lakini kuna dalili Liverpool itamnasa kinda huyo ambaye alizaliwa Ubelgiji wakati babake Mike Okoth, raia wa Kenya, alipokuwa akicheza kandanda ya kulipwa nchini humo.
Origi mwenyewe anasema ana hamu sana ya kushiriki ligi kuu ya England bora apate klabu kitakachomfurahisha.
Babake Origi ni shabiki sugu wa Liverpool hivyo basi huenda akamshawishi mwanawe ajiunge na bingwa hao mara 18 wa ligi kuu ya England.
Lakini kabla mashindano ya kombe la dunia yaanze Okoth alisema atampa Origi uhuru wa kuamua ni klabu kipi anataka kuchezea England endapo atakiacha kile cha Ufaransa, Lille.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates