Social Icons

Jumatano, 4 Juni 2014

SAUDI ARABIA YAATILIA SHAKA CHOKLETI ZA CARDBURY, ZADAIWA KUWA NA VIRUTUBISHO VYA NYAMA YA NGURUWE


CadburyMamlaka nchini Saudia Arabia ipo kwenye zoezi la kupima chokleti za Cadbury zinazotengenezwa  Uingereza kufuatia kashfa juu ya kuwekwa kwa
virutubisho vya nyama ya nguruwe kwenye bidhaa hizo kugunduliwa nchini Malaysia ambapo wito wa mgomo uliotolewa kwa makampuni yanayodhalisha bidhaa hiyo.
Siku chache zilizopita Mamlaka nchini Malaysia iligundua uwepo wa nyama za nguruwe kwa kutumia DNA katika bidhaa hiyo ya Cardbury Daily Milk huku taarifa ikimnukuu makamu wa  Rais wa sekta ya Chakula(SFDA) akisema kwamba kufanya vipimo hakukuhusisha bidhaa nyingine za Cardbury zinazozalishwa katika viwanda vya Malaysia na zilikuwa zikiagizwa kutoka nchi nyingine kama vile Misri na Uingereza.
Ijumaa iliyopita  Taifa la Indonesia lenye wakazi wengi waislamu  nao pia walikuwa wakipima bidhaa hizo kwa kuangalia kama zinazingatia vigezo vya kiislamu. Kashfa ya masharika yanayotengeneza vyakula visivyo halali ilianzia kusini mwa bara la Asia ambapo mwaka 2001 baraza la maulamaa la nchini Indonesia liliishtaki kampuni kubwa ya kijapani Ajinimoto iliyokuwa inatengeneza bidhaa za kula kwa kutumia virutubisho vya nyama ya nguruwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates