Social Icons

Jumapili, 29 Juni 2014

Kocha wa Uholanzi Louis van Gaal anatarajia shirikisho la soka duniani FIFA litawaruhusu wachezaji wake kunywa maji.


Fortaleza ni eneo linaloshuhudia viwango vya juu vya nyuzi joto.

Ni dhahiri kuwa mwili wa binadamu yeyote unastahili maji kwa hivyo hawa wachezaji naamini kuwa wanastahili kunywa maji ilikuzuia wasishikwe na kisunzi .Kocha huyo wa Manchester United ya Uingereza anasema kuwa utafiti uliofanywa kabla ya mashindano haya yanasema kuwa wachezaji wanapoteza maji lita nne ama zaidi kwa kila mechi wanayocheza katika jimbo hilo la Fortaleza.

Van Gaal kiwango cha joto ni juu mno
Van Gaal alitishia kuwapa wachezaji wake maji kwa wingi kando kando mwa uwanja iwapo FIFA haitahalalisha kuwepo kwa dakika moja au mbili ambapo mechi zitasimamishwa iliwachezaji wake wapige kopo la maji.
Kiungo wao Leroy Fer, ambaye anauguza jeraha la goti anasema kuwa Uholanzi ilipata kionjo tu cha kucheza katika hali ya kiwango cha juu mno cha joto baada ya kuwasili huko wakitoka Rio de Janeiro.
Fer anasema kuwa japo Uholanzi imezoea kucheza katika maeneo ya Uropa yenye baridi kali,Uholanzi itajikaza kisabuni kwani ni hali ileile itakayoikumba timu pinzani ya Mexico.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates