Social Icons

Alhamisi, 19 Juni 2014

HOFU YA BOMU ILISHAWAHI TOKEA MLIMANI CITY

HUKU watu karibia 60 nchini kenya wakiuawa kwenye mashambulizi ya kigaidi, katika hali isiyo ya kawaida nchini Tanzania, walinzi wa Maduka ya Mlimani City jijini Dar wamejikuta wakipata mchecheto wa aina yake baada ya kitu kilichodhaniwa ni bomu kukutwa kwenye eneo la kuegeshea magari. 
Walinzi wa maduka ya Mlimani City jijini Dar wakikagua kitu kinachosadikika kuwa ni bomu.
Tukio hilo lilitokea Juni 16, mwaka huu ambapo kwa mujibu wa shuhuda aliyeomba kusitiriwa jina, aliona gari dogo jeupe likiangusha kifaa hicho kilichodhaniwa ni bomu kisha likatoweka.

Chanzo hicho kilizidi kudai kuwa baada ya gari kutoweka, dada mmoja alipita eneo hilo na kukuta kitu hicho kilichofungwa nyaya kikiwa ndani ya mfuko, akashtuka na kwenda kumtonya mlinzi wa eneo hilo ambaye alifika mara moja na kuwaita wenzake.
...Ukaguzi ukiendelea.
Taarifa za uwepo wa kifaa hicho ziliwafikia waandishi wetu waliokuwa wakipiga doria katika eneo hilo na haraka wakasogea karibu kuwashuhudia walinzi hao wa Kampuni ya Ulinzi ya Omega wakiwa wamekizunguka kifaa hicho kwa umakini mkubwa.
Walinzi hao walimuita kiongozi wao ambaye alifika na kukichunguza kifaa hicho ambapo alipokifungua aligundua ni betri bovu la pikipiki.Waliichukua betri hiyo na kuitupa huku wakitawanyika kurudi kwenye maeneo yao ya ulinzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates