Social Icons

Ijumaa, 13 Juni 2014

IRAQ INAHITAJI MSAADA: OBAMA

Rais wa Marekani Barack Obama amesema serikali yake inatazama "njia mbalimbali" ikiwemo nguvu za kijeshi kuisaidia Iraq kupambana na wanamgambo.
Obama amesema Marekani ina nia ya kuhakikisha wapiganaji hawachukui tena udhibiti wa Iraq.
Matamshi yake hayo yamekuja baada ya
miji ya Mosul na Tikrit kuchukuliwa na wapiganaji wa Ki- Sunni.
Kura ya bunge ya kumpa Waziri Mkuu Nouri al-Maliki madaraka ya dharura ilisuasua baada ya wabunge kutojitokeza.
Wabunge 128 tu kati ya 325 ndio walikuwepo.
Taarifa ambazo hazijathibitishwa siku ya Alhamisi zinasema majeshi ya Iraq yamevurumisha mashambulio ya angani dhidi ya wapiganaji katika miji ya Mosul na Tikrit.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates