Social Icons

Jumamosi, 11 Oktoba 2014

TIMES REDIO,TCRA YACHUKIZWA NA VIPINDI VYAKE ,SOMA HAPA KUJUA ZAIDI.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEia99w3O61qtQDX1qrtryQDmUCPUxwLg6slhc_wyFrcHrlW1D2ueGyrUabkNcizQ_dccV0O3B5u5Aaw58QyWnqDjzlVX_FJoJt30KBmGU0udAr-na-JXAZE2Ic-xq3JUG4FdJXK-9CFKDI/s1600/SAM_0783.JPG
Mwenyekiti wa kamati ya maudhui ya TCRA, Mhandisi Margaret Tabu Munyagi, akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa Habari picha na Maktaba

KITUO cha Redio Times FM,kimetakiwa kulipa faini ya shilingi milioni moja baada ya kukiuka sheria ya utangazaji kwa kurusha vipindi vya ngono muda ambao haurusiwi.
           Hukumu hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na kamati ya maudhui ya utangazaji, katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano na Mwenyekiti wa kamati hiyo, Margaret Munyagi.
           Munyagi alisema vipindi vilivyokiuka maadili hayo ni kile cha ‘Hatua Tatu’ kinachorushwa kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 5 na kipindi cha mitikisiko ya Pwani kinachorushwa saa 6 mchana hadi 10 jioni.

         Akifafanua zaidi makosa hayo, alisema katika kipindi cha ‘hatua tatu’, watangazaji katika kipengele cha hatua za afya walikuwa wakiongoza mjadala wa mada ya kufanya ngono mara mbili kwa wiki kunamwezesha binadamu kuishi muda mrefu.
           Huku yule anayefanya ngono mara moja kwa mwezi kuwa katika hatari ya kuishi muda mfupi.
               Katika mjadala huo, inaelezwa kuwa watangazaji walionekana wazi kushabikia ikiwemo kuulizana wenyewe kuwa huwa wanafanya ngono mara ngapi, kitu ambacho ni kinyume na maadili ya utangazaji kwa kuzungumza mambo hayo muda wa mchana.
            Mwenyekiti huyo alisema ni hatari kwa kuwa wakati huo wasikilizaji wengi ni watoto jambo ambalo linaweza kuchangia kuzalisha kizazi kisichokuwa na maadili.
           Wakati kwa upande wa kipindi cha Mitikisiko ya Pwani, Mtangazaji alikuwa akizungumzia mada ya msichana aliyefumaniwa baada ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mjomba wake.
          Kutokana na makosa hayo alisema walisikiliza ushahidi kupitia CD za vipindi hivyo baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wasikilizaji na kujidhirisha kuwa walikuwa wamekosea.
Pia alisema waliwaita upande wa walalamikiwa akiwemo Mkurugenzi wa Times FM, Richard Nyaulawa na Mkuu wa Vipindi wa kituo hicho, Hemes Joachim, ampapo wote walikiri makosa hayo.

           Kwa mujibu wa Munyagi faini hiyo watatakiwa wailipe ndani ya siku 30 kuanzia jana na imeenda sambamba na onyo kali dhidi ya kituo hicho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates