Social Icons

Jumamosi, 18 Oktoba 2014

MAHAKAMA YA KISUTU YAMZUIA DAVIDO KUPERFORM FIESTA


Mahakama ya Kisutu yamzuia Davido kuperform katika tamasha la Fiesta*
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam imemzuia msanii kutoka
Nigeria, Adedeji Adelek maarufu kama 'Davido' kuperform katika tamasha la
Fiesta linaloandaliwa na Clouds Fm na Prime Promotion, October 18,2014.
Amri hiyo imetolewa jana (October 17) na hakimu mkazi wa mahakama ya kisutu mheshimiwa D. Kisoka kufuatia maombi ya dharura yaliyowasilishwa
mahakamani hapo na Times Fm Radio na Times Fm Promotion.

Times Fm Radio na Times Fm Promotion walipeleka maombi ya dharura
mahakamani hapo wakiitaka mahakama kumzuia msanii huyo kuperform katika
tamasha hilo kwa kuwa licha ya BASATA (Baraza La Sanaa Tanzania) kukataa
kutoa kibali cha msanii huyo kwa maelezo kuwa tayari alikuwa
ameshachukuliwa kibali cha kuperform nchini November 1 kwenye tamasha
lililoandaliwa na Times Fm Radio,  Clouds Fm na Prime Times Promotion
waliendelea na taratibu zote bila kujali zuio hilo la BASATA.

Times Fm Radio na Times Fm Promotion waliiomba mahakama kuidhinisha madai
yao dhidi ya Clouds Fm, Prime Promotion na mkurugenzi wa kampuni
inayomsimamia Davido, HKN Music.
Madai hayo ni pamoja na kulipwa fidia ya gharama na usumbufu
waliosababishiwa na walalamikiwa kadiri Mahakama itakavyoona inafaa.
Mahakama imetoa amri kuwa msanii huyo amezuiwa kufanya onesho hilo October
18,2014 hadi pale ufumbuzi wa kesi hiyo utakapopatikana mhakamani hapo.
Awali, Davido alisikika katika matangazo ya Times Fm Radio akieleza kuwa
atakuja Tanzania November 1 kwa ajili ya kufanya onesho linaloandaliwa na
kituo hicho cha radio lililopewa jina la 'The Climax'.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates