Social Icons

Ijumaa, 15 Agosti 2014

Raisi wa Africa ya Kusini "Jacob Zuma" ajikuta katika shutuma nzito

Raisi wa africa ya kusini Jacob Zuma ameshutumiwa kwa kuwa  na mfumo wa upendeleo (Nepotism) baada ya kumteua mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka 25 kushikilia cheo kikubwa serikalini.



Thuthukile Zuma amehamishwa kutoka katika nafasi ya afisa uhusiano wa umma (Public Liaison officer) na kupandishwa cheo ndani ya miezi miwili akiwekwa katika nafasi muhimu na yenye nguvu " Mkuu wa wafanyakazi"  katika wizara ya huduma za posta na mawasiliano



Thuthukile ni mtoto wa mwisho katika watoto wanne wa Zuma, ambae alipokea degree ya heshima ya Anthropology na kukabidhiwa cheo hicho mwezi wa tano mwaka huu baadaya baba yake (Raisi Zuma)  baada yakuchagua baraza lake la mawaziri.

nafasi hiyo aliyopewa ambayo inasemekana kutokutangazwa kabla, itakuwa ikimuingizia paundi 55,764 karibu randi milioni moja ambayo ni sawa na shilingi 154,631,365.14 kwa mwaka

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates