Social Icons

Jumatatu, 4 Agosti 2014

BIBI WA MJINI SONGEA AJITENGENEZEA JENEZA ILI AKIFA AZIKWE NALO


scolastica
Bibi Scholastica akiwa kwenye jeneza alilojiandalia

Mkazi mmoja wa Kijiji cha Lundusi Kata ya Peramiho wilayani Songea Mkoa wa Ruvuma,Bibi Scholastica Mhagama amesema miaka mingi ameishi maisha dhiki na kunyanyaswa bila msaada kutoka kwa jamii anayoishi hali ambayo imemfanya amuombe Mungu amchukuwe ili azikwe kwenye jeneza alilojiandalia.

“Kila siku naomba Mwenyezi Mungu anichukue haraka ili nikapumzike kutokana na mateso ninayoyapata, lakini hofu yangu nikifa je, nitazikwa kama binadamu wengine? Ndiyo maana nimeamua kujitayarishia jeneza langu,” anasema Scholastica Mhagama (76) mwenye ulemavu wa viungo anayeishi pekee yake katika kibanda kilichoezekwa kwa nyasi.

“Nimetengeneza kabisa jeneza langu siku nikifa wanizike humu. Naomba Mungu anichukue haraka ili kuepukana na mateso haya. Nimetengwa na jamii na majirani wanashindwa kunisaidia wanadai eti mimi ni mchawi kwa sababu watoto wangu wote wanne walikufa wakiwa wadogo. Naumia sana kusingiziwa kitu ambacho sikijui,’’ anasema kwa masikitiko.

Bibi huyo anasema kuwa aliweza kutengeza jeneza hilo baada ya kupewa Sh40,000 na mfadhili mmoja.
“Tayari nilikuwa na mbao kwangu, hivyo kazi ilikuwa kumlipa kijana fedha na kumpa mbao ili anitengenezee jeneza,” anasema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates