Social Icons

Ijumaa, 20 Septemba 2013

Boko Haram wafanya mashambulizi Abuja

Vijana wanaotoa ulinzi kwa wenyeji dhidi ya Boko Haram

Vikosi vya usalama nchini Nigeria, visema kuwa vishambuliwa na wapiganaji wa kiisilamu , Boko Haram, mjini Abuja.

Vikosi hivyo vimesema kuwa watu kadhaa walijeruhiwa wakati wapiganaji hao walipowafiatulia risasi maafisa waliokuwa wanatafuta silaha haramu.
 
 Mapigano haya yanakuja siku tatu baada ya shambulio lengine lililofanywa na watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Boko Haram katika jimbo la Borno.

Mwandishi wa BBC katika eneo hilo anasema kuwa baadhi ya watu hawajulikani waliko na kuwa huenda zaidi ya watu miamoja waliuawa.

Katika siku tatu zilizopita wafanyikazi katika sekta ya afya wamekuwa wakiondoa miili ya watu waliofariki kwenye malori.
 Afisa mmoja alisema kuwa alihesabu mili themanini na saba.

Lakini kuna uwezekano mkubwa kuwa miili zaidi inaweza kupatikana katika misitu na taarifa nyingine zinasema kuwa wapiganaji hao wanaodaiwa kuwa wa Boko Haram, waliwaua zaidi ya watu mia moja arobaini baada ya kuweka vizuizi vya barabarani na kuvalia magwanda ya jeshi wakijidai kuwa wanjeshi.
Jumanne shambulio karibu na Benisheik ni kati ya mabaya mno tangu hali ya hatari itangazwe Kaskazini Mashariki mwa Nigeria Mei.

Juhudi za kumaliza wapiganaji wa kiislamu zimefanya maeneo ya mijini kuwa salama lakini jeshi haliwezi kusema kuwa limeshinda vita kwani watu wanaoishi mashambani wamo katika hatari ya kushambuliwa.
Kwa sasa ni vigumu kupata habari kwani laini zote za simu zimekatwa katika juhudi za kuwasaidia wanajeshi kufaulu katika mpango wao.

Manusura wa mashambulio hayo yanayodaiwa kufanywa na Boko Haram wanasema kuwa wapiganaji hao walikuwa wamevalia sare za jeshi.

Waliwasili kwa magari , wakaweka vizuizi kati ya Maiduguri na Damaturu na wakaanza kuwaua watu.
Waliojaribu kukimbilia misituni walifuatwa na kupigwa risasi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates