Social Icons

Jumapili, 14 Septemba 2014

CHADEMA KUMPATA MWENYEKITI LEO: MPINZANI WA MBOWE ATANGAZA KUJITOA



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo kinafanya uchaguzi mkuu wa kumpata mwenyekiti na makamu wenyeviti wake watakaokiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa mwanasiasa mkongwe wa nchini Kenya, Raila Odinga.
Mchuano katika nafasi ya uenyekiti ilitarajiwa kuwa kati ya mwenyekiti anayemaliza muda wake, Freeman Mbowe na aliyekuwa mwenyekiti wa mkoa wa Tabora wa chama hicho, Kansa Mbarouk ambaye jana alitangaza kujitoa katika kinyang’anyiro. 
Hivyo kujitoa kwa Mbarouk kuna maanisha kwamba nafasi hiyo imebakisha wagombea watatu watakaochuana kuwania kiti hicho ambao ni Daniel Luvanga na Gambaranyera Mongateo.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa akizungumzia maandalizi ya Mkutano Mkuu wa chama hicho alisema kila kitu kinakwenda sawa ikiwa ni pamoja na vikao vya Kamati Kuu na Baraza Kuu ili kuandaa ajenda na kupitia majina ya walioomba kuteuliwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.

Gazeti hili lilikuwapo katika ukumbi wa Mlimani City jijini hapa na kushuhudia wajumbe wakiendelea kujiandikisha huku Kamati Kuu ikiendelea na mkutano wake kisha Baraza Kuu ikiwa ni kuweka kila kitu katika hali ya ufanisi.

Katika uchaguzi huo kundi ambalo linatarajiwa kuwa na ushindani ni la kuwania ujumbe wa kamati kuu ambapo hadi jana waliokuwa wameomba kuteuliwa kuwania kuingia katika chombo hicho kikubwa cha uamuzi walikuwa ni 58 kati ya nafasi hizo sita za Tanzania Bara na mbili Zanzibar, huku wajumbe wake watachaguliwa kwa uwiano sawa wa kijinsia.

Mbarouk akitangaza kujitoa katika kinyang’anyiro hicho alisema hawezi kuwa miongoni mwa wanachama wanaoikiuka na kuivunja katiba ya chama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates