Social Icons

Jumamosi, 22 Novemba 2014

PHILI KUMKUMBUKA KIEMBA

Kocha wa Simba Mzambia, Patrick Phiri, ameibuka na kudai kuwa atamkumbuka kiungo wake Amri Kiemba iwapo atakamilisha dili lake la kutimkia Azam FC ambayo inamuwinda kwa mkopo.


Kiemba anadaiwa kutakiwa na Azam FC kwa mkopo, baada ya kutoelewana na uongozi wa Simba ambao ulikuwa ukimtuhumu mara kwa mara kucheza chini ya kiwango wakati akiitumikia klabu hiyo tofauti na anapokuwa na timu ya taifa, Taifa Stars.

Kutokana na hali hiyo uongozi wa Simba ulimsimamisha pamoja na wachezaji wenzake wawili ambao ni Shabani Kisiga na Haruna Chanongo.

Phiri alizungumza  akiwa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, tayari kwenda Zambia na kusema iwapo ataondoka, atamkumbuka sana kiungo huyo ambaye alifanya naye kazi akiwa Simba.

Alisema anatamani kuona anaendelea kuwa naye kwenye kikosi chake lakini wenye maamuzi ya mwisho ni viongozi wa timu hiyo.

“Kiemba ni mchezaji mzuri ambaye katika kipindi chote alichokuwa na mimi sikuwahi kugombana naye, hivyo nitammisi sana katika kikosi changu iwapo ataondoka lakini naamini kwa uwezo wake anaweza kufanya vizuri popote atakapokwenda.

“Kuhusiana na kuziba pengo lake nimeshaongea na viongozi, pia katika ripoti yangu hilo nimelizungumzia, ni matumaini yangu kuwa litafanyiwa kazi na tutampata mbadala wake,” alisema Phiri ambaye anatarajia kurejea nchini Novemba 26 mwaka huu kuendelea na majukumu yake ya kukinoa kikosi hicho chenye maskani yake mtaa wa Msimbazi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates