Social Icons

Jumamosi, 22 Novemba 2014

JAMAA ALIYEMTWANGA MKEWE TALAKA SIKU YA HARUSI




Jamaa mmoja kutoka nchini Saudi Arabia amempa talaka mkewe siku ya harusi baada ya kumuona uso wake kwa mara ya kwanza. Maharusi hao kutoka mji wa Saudia,Medinah walikubaliana kuoana pamoja na kujua kabisa hawajawahi kuonana sura zao,swala ambalo ni utamaduni mkubwa wa mataifa ya kiarabu.
Lakini wakati mwanamke huyo alipofungua kitambaa cheupe kilichopo katika shela alichokuwa amejifunika uso na kutabasamu katika kamera,mumewe alishtuka na kuondoka wa ghafla.
Mwanamume huyo alianguka na kuzirai huku wageni waalikwa wakijaribu kuingilia kati ili kutatua kilichokuwa kikiendelea. Hata hivyo Bwana harusi alisema kuwa hakuweza kumwona bi harusi kabla ya harusi yao.
'' Si wewe msichana niliyetaka kuoa,si wewe kamwe niliyedhani '' kwa hivyo nakupa talaka''alisema bwana harusi.
Na alipompa talaka bi harusi naye alianguka na kuzirai na kuifanya harusi hiyo kuwa usiku wa majonzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates