Social Icons

Jumatatu, 3 Novemba 2014

Mbeya City kuweni makini.

Wahenga walisema kuwa usiku wa dhiki huwa mrefu kuliko kawaida , msemo huu unaonekana kuwahusu zaidi wazee wa Green City aka Mbeya City ambao hii leo wameshuhudia timu yao ikipoteza mchezo wake wa tatu mfululizo katika muendelezo wa ligi kuu ya Tanzania bara akak VPL .
Mbeya City ambao hii leo walikuwa wakimalizia kiporo kilicholala siku ya jumapili baada ya mchezo wao kuahirishwa walifungwa 2-1 na maafande wa Mgambo Shooting katika mchezo uliopigwa kwneye uwanja wa Ccm Mkwakwani huko Tanga .
Kikosi cha Mgambo Jkt.
Kikosi cha Mgambo Jkt.
Mbeya City ambao msimu huu wameuanza vibaya baada ya kufanya vizuri na kuwashangaza wengi msimu uliopita waliuanza mchezo kwa kasi ya chini hali iliyowafanya kufungwa bao la kwanza mapema kwenye kipindi cha kwanza mfungaji akiwa Malime Busungu aliyefunga kwa mkwaju wa penati baada ya beki wa Mbeya City Yohana Morris kufanya madhambi kwenye eneo la hatari .
Zikiwa zimepita dakika chache baada ya kipa David Burhani kuokota mpira wavuni kwake , alijikuta akirejea kitendo kama hicho baada ya kushindwa kuzia shuti la kiungo Ali Nassor Iddi ambaye alimalizia kazi nzuri iliyofanywa na mfungaji wa bao la kwanza Malime Busungu .
Kipindi cha kwanza kiliisha huku Mgambo wakizidi kulisakama lango la Mbeya City na kama isingekuwa uzembe wa washambuliaji Mgambo wangeweza kumaliza dakika 45 za kwanza wakiwa na mabao zaidi .
Katika kipindi cha pili Mbeya City walifanya mabadiliko ya kuongeza nguvu safu ya ushambuliaji kwa kuwaingiza Saad Kipanga na Hamad Hamza Kibopile .
Mbadiliko haya yalileta uhai kwani winga Deus Kaseke aliifunia Mbeya City bao lao pekee katika mchezo huo , bao ambalo hata hivyo halikutosha kuwazuia Mgambo wasiondoke na ushindi wao wa tatu katika msimu huu .
Ushindi huu unawafanya Mgambo kuruka mpaka kwenye nafasi ya sita wakiwa wamejikusanyia pointi tisa zinazotokana na mechi tatu walizoshinda huku wakiwa wamepoteza michezo mitatu pia .
Kwa upande wa Mbeya City hali imezidi kuwa mbaya kwani wanajikuta wanapoteza mchezo wa tatu mfululizo hali ambayo itazidi kumpa ‘stress’ kocha wao Juma Mwambusi .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates