Social Icons

Ijumaa, 3 Julai 2015

Ugiriki yaombwa kusema, 'La'

Raia wa Ugiriki

Raia wengi hawataki masharti ya kubana matumizi kama yanavyopendekezwa na wakopeshaji wa Ugiriki
Waziri MKuu wa Ugiriki Alexis Tsipras amewaomba wapiga kura kupinga vitisho na kusema 'La' wakati wa kura ya maamuzi ya hapo Jumapili.
Katika hotupa fupi kwenye runinga ya taifa, Bw Tsipras amesisitiza kwamba hakuna tisho lolote la Ugiriki kufukuzwa kutoka Muungano wa Ulaya.
Amewaambia wafuasi wake kupuuza kelele za wale aliowataja kama wanaotoa vitisho.
null
Ugiriki inakumbwa na msukusuko wa kiuchumi
Hapo Jumapili wapiga kura wa Ugiriki wataamua kuunga au kukataa masharti ya kupokea mkopo kutoka kwa mashirika ya kimataifa.
Ugiriki ilishindwa kuafikiana na wakopeshaji wake wakati wa mazungumzo ya miezi kadhaa.Viongozi wa Ulaya wameonya kwamba kura ya 'La' huenda ikasababisha Ugiriki kuondoka kanda inayotumia sarafu ya Euro.
null
Benki zimefungwa Ugiriki, huku kukiwa na kiwango rasmi cha pesa wateja wanafaa kutoa
Tayari uchumi wa Ugiriki unakumbwa na msukosuko mkubwa baada ya nchi hiyo kushindwa kupata mkopo wa dharura.
Benki za nchi zimefungwa huku kukiwekwa kiwango rasmi ambacho wateja wanafaa kutoa.
Hakujafanyika mihadhara, mikubwa mjini Athens lakini mabango ya mirengo ya 'La' na 'Ndio' yametawala kote mjini Athens kila upande ukijaribu kuwashawishi wapiga kura.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates