Social Icons

Jumamosi, 28 Novemba 2015

Pellegrini:''Guardiola hanitishi''

Image copyrightPA
Image captionPellegrini
Mkufunzi wa kilabu ya Manchester City Manuel Pellegrini amesema kuwa hana wasiwasi na ripoti zinazomuhusisha mkufunzi wa Bayern Munich Pep Guardiola na kazi yake.
Guardiola alifanya kikao cha habari na waandishi siku ya ijumaa huku kukiwa na tetesi kutoka kwa magazeti kwamba ataelekea City na nyota wa Barcelona Lionel Messi.
''Ni uvumi ambao umekuwa ukiendelea katika misimu miwili na nusu sasa'', alisema Pellegrini ambaye aliajiriwa na City mnamo mwezi Juni alipoulizwa kuhusu uvumi huo.''Sina tatizo na hilo''.
Image copyright
Image captionGuardiola
Ripoti zimedai kwamba Guardiola mwenye umri wa miaka 44 amekubali kuondoka Bayern mwishoni mwa msimu huu ili kuichukua Manchester City.
Mwenyekiti Karl-Heinz Rummenigge amesema kuwa tangazo kuhusu siku za usoni za mkufunzi huyo litafanywa kabla ya mwisho wa mwaka huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates