Social Icons

Alhamisi, 26 Novemba 2015

NEY AZUNGUMZIA WENZIE.....................YEYE JE?



Umeshawai kujiuliza kwa tabia au sifa ya mtu flani angeweza kufanya kazi gani kutokana na sifa hizo. Sasa Nay wa Mitego ameweza kuzungumzia watu maarufu wenzake watano kwa jinsi anavyowajua wangeweza kufanya kazi hizi zaidi ya wanazofanya sasa hivi.
Wema Sepetu
Kwa jinsi ninavyomjua Wema nadhani angekua customer care mzuri sana kwenye kampuni yoyote na sauti yake ile angewafurahisha wateja wengi sana. Lakini pia angeweza kuwa mhudumu mzuri tu kwenye hotel flani hivi nzuri nzuri na watu wangeenda kwenye hiyo hotel kwa sababu ya Wema. Anajua kuongea na watu, smile na sauti nzuri.
JB
Huyu jamaa na ule mwili wake ni mpishi mzuri sana zaidi ya kuwa muigizaji alivyo sasa. Pia mapenzi yake kwenye kula msosi basi inaonyesha jinsi gani yeye na msosi ni marafiki kuanzia jikoni hadi mezani.
TID
Huyu jamaa ni muongeaji pia ni mcheshi sana, ukitoa kuwa msanii mzuri basi angeweza kuwa muuza chips mzuri sana maeneo ya kwao Kinondoni na banda lake lingejaa wateja wengi sana kwasababu ya kuongea kwake.
Diamond
Licha ya kufika hapo alipofika Diamond bado uswahili wake wa Tandale anao kama kawaida. Sasa napata picha huyu jamaa awe konda, itakua fujo sana kwenye hilo daladala na abiria wake. Nadhani maneno ya mtaani yatakua mengi na vichambo kama kwenye nyimbo zake..atawanyoosha abiria wake.
Adam Mchomvu
Huyu jamaa ana kipaji sana cha kuongea maneno ambayo huwezi kutegemea akaongea ghafla yani yakafurahisha na ku-make sense. Sasa Mchomvu ile kazi ya uswahilini kwetu ya kuuza dawa ya panya,mende,kunguni,viroboto angetisha sana. Hatakua na haja ya kujirekodi sauti na kile ki-speaker atakua anapiga free style tu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates