Social Icons

Jumatano, 5 Februari 2014

NAIBU WAZIRI WA FEDHA MH:MWIGULU AHITIMISHA ZIARA YAKE YA MIKOA MITATU KWA KUZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA MBEYA MJINI


Naibu Waziri wa Fedha Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na Wafanyabiashara wa Mbeya Mjini hii leo kwenye Ukumbi wa Mtenda Hotel Jijini Mbeya.Sehemu ya Wafanyabiashara wa Mbeya Mjini wakiwa kwenye Mkutano wa ndani wa Naibu Waziri wa Fedha Mh.Mwigulu Nchemba hii leo.
 
Naibu Waziri wa Fedha Mh:Mwigulu Nchemba hii leo amehitimisha ziara yake ya kikazi iliyojumisha Mikoa Mitatu(Njombe,Ruvuma na Mbeya),Ziara yake imehitimishwa kwa Kuzungumza na Wafanyabiashara wa Mbeya Mjini,Pia amekutana na Watendaji/watumishi wa Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA),Hazina ndogo Mkoani Mbeya na Ofisi ndogo ya Takwimu.
Akizungumza na Wafanyabiashara wa
Mbeya Mjini Naibu Waziri  amesema,Katika ziara yake amesisitiza kuwa Ofisi yake inatambua Mchango wa Wafanyabiashara katika Uchumi wa Nchi hii hususani ulipaji wa kodi,Hivyo katika utungaji wa Sera mbambali za ulipaji kodi na Kuinua Uchumi wa Nchi, Ofisi yake itashirikiana na Wafanyabiashara  nchi nzima kwasababu ndio wadau husika kwenye ulipaji kodi katika Taifa hili.

Pia Mh:Mwigulu ameendelea kuwaomba Wafanyabiashara kuendelea kuunga mkono matumizi ya Mashine za EFD's kwenye ukusanyaji wa kodi halisi za bidhaa/huduma husika inayotolewa.Ni muhimu kwa Watanzania kutambua mabadiriko ya mifumo ya ukusanyaji kodi nchini kwa manufaa yao na Taifa lao,Kutumia mashine za EFD's kunasaidia kudhibiti upotevu wa mapato kupitia kodi,Kunasaidia wafanyabiashara kupata makusanyo stahiki kulingana na huduma/bidhaa anazouza.
Akiwa ameambatana na Wataalamu kutoka Wizarani na Makao Makuu ya TRA,Wafanyabiashara wa Mbeya wameelimishwa kuwa Mfanyabiashara yeyote mwenye mauzo kuanzia Milioni 14 kwa Mwaka ndiye anapatwa kutumia mashine hizo,Pia wafanyabaishara wote waliosajiliwa kulipa kodi,Pia matumizi ya Mashine za EFD's zinasaidia kutunza kumbukumbu za biashara husika,Zinapunguza wizi na Ujanja wa  wauzaji wasio wenye mali.
Vilevile,Wafanyabiashara wa Mbeya wameomba serikali kuondoa ufutiliaji wa kulipa kodi kwa wachuuzi wadogowadogo,Serikali ifanyie kazi Ukusanyaji wa Kodi kwenye Viwanda,Mipakani,Viwanja vya ndege na kwenye Soko la kimataifa.Pia sheria ya Kodi ni kandamizi kwa Wafanyabiashara wa dogowadogo na faini zake ni kubwa mno kitu kinachoshawishi Rushwa kati ya Wafanyabiashara na Watendaji wa TRA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates