Social Icons

Jumatatu, 10 Februari 2014

BOSCO NTAGANDA MAHAKAMANI ICC



Ntaganda pia anatuhumiwa kwa kuwatumia wanawake kama watumwa wa ngono
Kesi ya Bosco Ntaganda anayetuhumiwa kwa uhalifu wa kivita Katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo inaanza leo katika mahakama mjini The Heague Uholanzi.
Amekana madai ya kufanya uhalifu wa kivita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo miaka kumi iliopita.
Bosco Ntaganda alijisalimisha katika ubalozi wa Marekani nchini Rwanda mwaka uliopita wakati kundi lake M23 lilipoanza kulemewa.
Ni miongoni mwa washukiwa wakuu wa ICC wanaotuhumiwa kwa kuwatumia watoto wadogo kama wanajeshi,kuwatumia wanawake watumwa wa ngono na mauaji.Chanzo BBC Swahili
Kikao cha leo kinatarajiwa kuwasaidia majaji kuamua iwapo kuna ushahidi wa kutosha kumfungulia mashitaka Ntaganda.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates