Social Icons

Ijumaa, 1 Mei 2015

Mamlaka ya Nepal yaomba usaidizi zaidi

helikopta
Mamlaka ya Nepal imeomba msaada zaidi wa helikopta kutoka kwa mataifa ya kigeni baada ya nchi hiyo kukumbwa na tetemeko baya la ardhi ambapo zaidi ya watu elfu sita waliuawa.
Serikali imesema inahitaji ndege hizo kusafirisha misaada ya dharura katika maeneo ya vijiji hususan maeneo ya milimani.
Nepal tetemeko
Pia ndege hizo zitasaidia kuwasafirisha majeruhi ili kupokea matibabu.
Kumekua na makabiliano miongoni mwa manusura wanaong'angania usafiri mdogo ambao unatolewa na serikali.
Nepal
Serikali pia imetaka maiti zote kuzikwa punde baada ya kutolewa ndani ya vivusi.
Waziri wa fedha wa Nepal , Ram Sharan Mahat, amesema nchi yake inahitaji dola bilioni mbili kukarabati nchi hiyo ambayo miundo msingi yake imeharibiwa vibaya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates