Taswira nzima ya mabasi yaendayo mikoani katika Stendi ya Ubungo.MGOMO wa madereva umeingia siku ya pili leo baada ya kuanza jana asubuhi huku wakazi mbalimbali wakiwemo wa jijini Dar wakilazimika kutembea kwa mguu kwenda kwenye maeneo yao ya kufanyia shughuli za kila siku.
Katika Kituo cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo, mabasi matatu ya Kampuni ya Shabiby Line yameripotiwa kuondoka kituoni hapo kuelekea Morogoro na Dodoma yakiwa chini ya ulinzi mkali wa eskoti ya askari polisi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni