Social Icons

Alhamisi, 24 Septemba 2015

Wengi wauawa katika mkanyagano Mecca

Watu 220 waliokuwa wakishiriki sherehe za hija wamefariki kwenye mkanyagano uliotokea katika mji mtakatifu wa Kiislamu wa Mecca, maafisa nchini Saudi Arabia wamesema.
Idara ya ulinzi wa raia nchini humo imesema kupitia Twitter kwamba watu wengine 450 wamejeruhiwa katika kisa hicho kilichotokea mji wa Mina, takriban kilomita tano kutoka mji wa Mecca.
Shughuli za uokoaji zinaendelea, idara hiyo imeongeza.
Mkanyagano huo umetokea siku ya kwanza ya sherehe za Eid al-Adha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

 
 
Blogger Templates