Amber Rose na Wiz Khalifa, wanandoa ambao wametengana hivi karibuni bado wanaonesha kuna mapenzi kati yao na sio maadui kama wengi walivyodhani.
Jumanne asubuhi, Wiz Khalifa alimtumia Amber Rose ujumbe wa kumtakia heri katika siku yake ya kuzaliwa kupitia Twitter.
“Happy Birthday Amb,” alitweet Wiz Khalifa, ujumbe uliopokelewa vizuri kwa shukurani na Amber Rose.
“Thank u Sweetheart #IstillLoveYouNoMatterWhat.” Alitweet Amber Rose.
Mwanamitindo huyo ambaye alikuwa anatumiza miaka 31 alisherehekea siku yake ya kuzaliwa akiwa na marafiki zake.
Hivi karibuni Wiz Khalifa amekuwa akionekana na wasichana warembo tofautitofauti katika maeneo ya Las Vegas na Hollywood.
|
NBAA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA TAALUMA YA UHASIBU KWA WANAFUNZI WA CHUO
KIKUU CHA MZUMBE
-
Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendelea
kutoa elimu na mafunzo kwa vyuo vikuu pamoja na shule za sekondari ikiwa na ...
Saa 6 zilizopita
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni